Wapendwa watanzania wenzangu, nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ( salamu maalum aliyoiasisi Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan na ambayo kiitikio ni "Kazi iendelee").
Mimi huwa napenda sana jinsi Malkia wa Uingereza (kwa sasa Qween Elizabeth) anavyopendwa na kuheshimiwa sana na watu wake. Ukiangalia hafla mbalimbali anazohudhuria Malkia unaona kabisa ukuu wake unavyojidhihirisha.
Sisi Tanzania kwa mipango yake Mungu mwenyewe tumebahatika kuwa na Rais mwanamke Mh. Mama yetu Samia Suluhu Hassan. Mimi binafsi nafarijika sana nikimuangalia na kumsikiliza Mama Samia. Ni Rais lakini ni Mama kabisa yaani ana upendo wa dhati kabisa wa mama na ana nia ya dhati ya kuiongoza nchi yetu kwa amani na kwa kuzingatia utawala wa sheria.
Ukifuatilia historia ya Mama Samia utaona kabisa ni Mwanamke mpambanaji na amefanikiwa sana katika mambo mengi. Unaweza kuona kabisa kwamba hadi wakati anakuwa Makamu wa Rais na hatimaye Rais wetu, alikuwa anajitosheleza kwa kila kitu kiuchumi, kijamii na kisiasa.
Mimi naamini Mama hayuko kwenye kile kiti kutafuta chochote (kiuchumi, kijamii na kisiasa) maana vyote amejitosheleza. Hivyo, naamini yuko pale ili kuongoza nchi hii ipate maendeleo zaidi na watanzania tuishi kwa furaha bila hofu.
Nawasihi sana watanzania wenzangu tumpe Rais wetu "treatment" kama ile anayopewa Malkia wa Uingereza. Hebu ona hapa kwa mfano
Vitabu vya dini vinatuambia mamlaka za duniani hutoka kwa Mungu, hivyo tuziheshimu mamlaka hizo. Rais ni alama kuu ya nchi. Tumheshimu sana Rais wetu.
Namuoba Mungu ampe Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan afya njema kimwili, kiakili na kiroho ili aendelee kuiongoza na kuiletea maendeleo Tanzania yetu.
Nawatakia Mapinduzi Day njema wapendwa.
Mimi huwa napenda sana jinsi Malkia wa Uingereza (kwa sasa Qween Elizabeth) anavyopendwa na kuheshimiwa sana na watu wake. Ukiangalia hafla mbalimbali anazohudhuria Malkia unaona kabisa ukuu wake unavyojidhihirisha.
Sisi Tanzania kwa mipango yake Mungu mwenyewe tumebahatika kuwa na Rais mwanamke Mh. Mama yetu Samia Suluhu Hassan. Mimi binafsi nafarijika sana nikimuangalia na kumsikiliza Mama Samia. Ni Rais lakini ni Mama kabisa yaani ana upendo wa dhati kabisa wa mama na ana nia ya dhati ya kuiongoza nchi yetu kwa amani na kwa kuzingatia utawala wa sheria.
Ukifuatilia historia ya Mama Samia utaona kabisa ni Mwanamke mpambanaji na amefanikiwa sana katika mambo mengi. Unaweza kuona kabisa kwamba hadi wakati anakuwa Makamu wa Rais na hatimaye Rais wetu, alikuwa anajitosheleza kwa kila kitu kiuchumi, kijamii na kisiasa.
Mimi naamini Mama hayuko kwenye kile kiti kutafuta chochote (kiuchumi, kijamii na kisiasa) maana vyote amejitosheleza. Hivyo, naamini yuko pale ili kuongoza nchi hii ipate maendeleo zaidi na watanzania tuishi kwa furaha bila hofu.
Nawasihi sana watanzania wenzangu tumpe Rais wetu "treatment" kama ile anayopewa Malkia wa Uingereza. Hebu ona hapa kwa mfano
Vitabu vya dini vinatuambia mamlaka za duniani hutoka kwa Mungu, hivyo tuziheshimu mamlaka hizo. Rais ni alama kuu ya nchi. Tumheshimu sana Rais wetu.
Namuoba Mungu ampe Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan afya njema kimwili, kiakili na kiroho ili aendelee kuiongoza na kuiletea maendeleo Tanzania yetu.
Nawatakia Mapinduzi Day njema wapendwa.