mpimamstaafu
JF-Expert Member
- Jul 18, 2018
- 4,445
- 4,707
Hakika inasikitisha sana TFF na Klabu zetu zinapowatelekeza Wachezaji wake walioliletea Taifa na Vilabu zetu wakati wanacheza mpira.Mchezaji Allan Shomari alikuwa Mchezaji mahiri wa Klabu ya Yanga na Timu ya Taifa.Mchezaji huyu amepoteza uwezo wa kuona hali ambayo inamfanya ashindwe kuendesha maisha yake na familia yake.Mchezaji huyo amekuwa akiomba omba misaada ili iweze kumsaidia.Tunaishauri TFF na YANGA viangalie namna ya kumsaidia Mchezaji huyu,kumbukeni alivyoisaidia Timu ya Taifa na Klabu ya Yanga.Mbona hivi karibuni Mh.Rais alimsaidia Mchezaji Peter Tino kwanini na nyie TFF msimsaidie Allan Shomari na wachezaji wengine waliolitumikia Taifa letu?Vivyo hivyo kwa Vilabu vyetu Viwakumbuke japo mara moja Wachezaji waliovichezea miaka ya nyuma kwani walijitoa.