Tumuombe Mwenyezi Mungu

Tumuombe Mwenyezi Mungu

Vumilika

JF-Expert Member
Joined
Mar 5, 2017
Posts
1,748
Reaction score
2,127
Amani iwe nanyi,

Kwa kuwa tumemaliza uchaguzi na umepitia katika hali ya kushangaza pale matokeo yalipotangazwa kuona chama tawala kikishinda katika chaguzi zote za uraisi, ubunge na udiwani kwa "kishindo", ni vyema tukajifariji kwa pande zote zilizoshinda na kushindwa kwa haki kwa Kumuomba Mwenyezi Mungu ili atujaaliye amani na upendo katika maisha yetu. Lakini tukumbuke dhulma haina nafasi katika jamii ya wapenda haki na amani.

Uchaguzi huu umeonyesha jinsi gani mfumo wetu wa demokrasia ulivyo na dosari, na dhahiri shahiri hakutakuwa na upinzani wa kweli ndani ya nchi hii, hivyo basi ni bora turudi kwenye mfumo wa chama kimoja ili tuweze kueleweka ni jinsi gani tunataka mfumo wetu wa utawala uwe, hii si dalili nzuri kwa nchi kama yetu ya Tanzania kwani tunaweza tukakaribisha machafuko na uvunjifu wa amani ambayo ni jambo pekee tunalojivunia nalo.

Hivyo basi tuombe sana tena sana, kuliko tulivyo omba wakati wa Corona ili tuepushwe na dhambi hii ya dhulma. Aameen.
 
Sio kuomba tu, bali tusome na kutafakari maneno ya Mungu, kutoka huko tutapata hekima, maarifa, busara na utu wa kujua haki na wajibu wetu hapa duniani. Nina imani mcha Mungu hawezi kumnyima haki yeyote binadamu mwenzie.
 
Sio kuomba tu, bali tusome na kutafakari maneno ya Mungu, kutoka huko tutapata hekima, maarifa, busara na utu wa kujua haki na wajibu wetu hapa duniani. Nina imani mcha Mungu hawezi kumnyima haki yeyote binadamu mwenzie.
Ni kweli uyasemayo lakini ni wachache ndiyo wenye kuyasoma na kuyatafakari maneno ya Mungu.
 
Mambo yote shwari, ondoeni wasi wasi...



Cc: mahondaw
Leo inabidi tuzidishe maombi kwani kesho huenda kuna baadhi ya ndugu zetu wakawa wametangulia mbele ya haki au mahospitalini au mahabusu au majumbani mwao wakiwa na maumivu. Hivyo tuzidishe maombi.
 
Leo inabidi tuzidishe maombi kwani kesho huenda kuna baadhi ya ndugu zetu wakawa wametangulia mbele ya haki au mahospitalini au mahabusu au majumbani mwao wakiwa na maumivu. Hivyo tuzidishe maombi.

Naimani hatutafikia huko...


Cc: mahondaw
 
Ninaikumbuka safari ya wana wa Israel jangwani (kiimani zaidi manake sikuwepo wakati huo) pale ambapo walimlilia Mussa na kumlalamikia kwa kuwatoa Misri walipoishi na kuwaleta jangwani na kuwasababishia mateso.
Safari ile kiimani haina tofauti kabisa na safari tunayoipitia Watanzania, ambao tulimlilia sana Mungu tukimuomba atupatie mtu atakayetuvusha toka “Misri” na kutupeleka nchi ya ahadi ya maziwa na asali.
Naifananisha safari ile kwa sababu zifuatazo. Watanzania wengi tunaamini kuwa nchi yetu imebarikiwa sana, tuna kila kitu kinachopasa kutufanya tuwe Taifa tajiri na lenye uchumi mkubwa. Lakini bado sisi ni masikini wa kutupwa. Tulilalamika sana kwa tawala zilizopita hasahasa tawala ya “mzee wa bata” ambaye tulimkosoa kwa tabia zake za kula bata kupindukia na kusahau kuijenga nchi. Mtu tuliyemuona legelege na dhaifu asiyeweza kukemea maovu na kulifanya Taifa liwe shamba la bibi ambalo kila aliyepita karibu yake hakuacha kuingia na kujichumia matunda kisha kwenda zake.
Sasa Mungu katujibu kilio chetu na kutuletea mtu “mkali” mtu asiye na lelemama, mwenye msimamo thabiti wa kukemea si maovu tu bali hata kuwachukulia hatua wale wote wenye nia mbaya.
Lakini kama walivyokuwa wana wa Israel, mbali na kuletewa Musa aliyeweza watoa Misri na kuanza nao safari ya kuelekea Kaanani, bado walifikia mahali wakaanza mlalamikia na kusema ni bora wangebaki Misri utumwani na si kuwaleta jangwani ili wafe kwa njaa na baridi kali. Wakasahau kabisa dhamira yao iliyo kuu mbele yao ya kuondoka utumwani na kuelekea nchi ya ahadi ya Kaanani iliyojaa maziwa na asali.
Vivyo hivyo kwa nchi yetu, tunapitia katika kipindi ambacho watu wengi wanalalamika na kuona kama “Musa” wa sasa anatuletea shida na hali ngumu mpaka tunaikumbuka “Misri” ya mzee wa bata. Tunapaswa kuikumbuka safari ile ya wana wa Israel na kutambua ya kwamba hakuna mazuri yanayofikiwa kirahisi, hakuna furaha inayokuja kirahisi pasi na mahangaiko tena wakati mwingine kujitoa sadaka kwa ajili ya wengi. Hata Musa mwenyewe ambaye aliteuliwa kuwatoa wana Israel utumwani na mahangaiko yote aliyokumbana nayo njiani bado hakuiona nchi ya ahadi.
Lakini jambo hili linanipa faraja wakati mwingine kwani linafanana sana na ile safari, na ninaamini kuwa kwa sasa tuko jangwani lakini kwa HAKIKA tutavuka salama, misukosuko na maumivu ya sasa ipo siku yatakwisha na labda watoto au wajukuu wetu wataifikia Kaanani nchi ambayo baba na babu zao tulitaabika ili wafike.
 
Ninaikumbuka safari ya wana wa Israel jangwani (kiimani zaidi manake sikuwepo wakati huo) pale ambapo walimlilia Mussa na kumlalamikia kwa kuwatoa Misri walipoishi na kuwaleta jangwani na kuwasababishia mateso.
Safari ile kiimani haina tofauti kabisa na safari tunayoipitia Watanzania, ambao tulimlilia sana Mungu tukimuomba atupatie mtu atakayetuvusha toka “Misri” na kutupeleka nchi ya ahadi ya maziwa na asali.
Naifananisha safari ile kwa sababu zifuatazo. Watanzania wengi tunaamini kuwa nchi yetu imebarikiwa sana, tuna kila kitu kinachopasa kutufanya tuwe Taifa tajiri na lenye uchumi mkubwa. Lakini bado sisi ni masikini wa kutupwa. Tulilalamika sana kwa tawala zilizopita hasahasa tawala ya “mzee wa bata” ambaye tulimkosoa kwa tabia zake za kula bata kupindukia na kusahau kuijenga nchi. Mtu tuliyemuona legelege na dhaifu asiyeweza kukemea maovu na kulifanya Taifa liwe shamba la bibi ambalo kila aliyepita karibu yake hakuacha kuingia na kujichumia matunda kisha kwenda zake.
Sasa Mungu katujibu kilio chetu na kutuletea mtu “mkali” mtu asiye na lelemama, mwenye msimamo thabiti wa kukemea si maovu tu bali hata kuwachukulia hatua wale wote wenye nia mbaya.
Lakini kama walivyokuwa wana wa Israel, mbali na kuletewa Musa aliyeweza watoa Misri na kuanza nao safari ya kuelekea Kaanani, bado walifikia mahali wakaanza mlalamikia na kusema ni bora wangebaki Misri utumwani na si kuwaleta jangwani ili wafe kwa njaa na baridi kali. Wakasahau kabisa dhamira yao iliyo kuu mbele yao ya kuondoka utumwani na kuelekea nchi ya ahadi ya Kaanani iliyojaa maziwa na asali.
Vivyo hivyo kwa nchi yetu, tunapitia katika kipindi ambacho watu wengi wanalalamika na kuona kama “Musa” wa sasa anatuletea shida na hali ngumu mpaka tunaikumbuka “Misri” ya mzee wa bata. Tunapaswa kuikumbuka safari ile ya wana wa Israel na kutambua ya kwamba hakuna mazuri yanayofikiwa kirahisi, hakuna furaha inayokuja kirahisi pasi na mahangaiko tena wakati mwingine kujitoa sadaka kwa ajili ya wengi. Hata Musa mwenyewe ambaye aliteuliwa kuwatoa wana Israel utumwani na mahangaiko yote aliyokumbana nayo njiani bado hakuiona nchi ya ahadi.
Lakini jambo hili linanipa faraja wakati mwingine kwani linafanana sana na ile safari, na ninaamini kuwa kwa sasa tuko jangwani lakini kwa HAKIKA tutavuka salama, misukosuko na maumivu ya sasa ipo siku yatakwisha na labda watoto au wajukuu wetu wataifikia Kaanani nchi ambayo baba na babu zao tulitaabika ili wafike.
Musa alikuwa akizungumza na Mungu na alikuwa akiwaombea wana wa Izraeli ili watoke katika maisha ya kidhalimu chini ya utawala wa Farao na kwenda katika nchi ya ahadi, kwa bahati mbaya Musa aliwaokoa na Farao lakini hawakuweza kufikia lengo lao na wakaishi jangwani. Tatizo letu sisi watanzania hatuna kiongozi mwenye kuzungumza na Mungu, ndiyo maana tunataka kumuomba Mungu ili tuweze kufika katika Tanzania iliyo na mito ya maziwa na asali. Lakini kwa sasa amani ni muhimu.
 
Amani iwe nanyi,

Kwa kuwa tumemaliza uchaguzi na umepitia katika hali ya kushangaza pale matokeo yalipotangazwa kuona chama tawala kikishinda katika chaguzi zote za uraisi, ubunge na udiwani kwa "kishindo", ni vyema tukajifariji kwa pande zote zilizoshinda na kushindwa kwa haki kwa Kumuomba Mwenyezi Mungu ili atujaaliye amani na upendo katika maisha yetu. Lakini tukumbuke dhulma haina nafasi katika jamii ya wapenda haki na amani.

Uchaguzi huu umeonyesha jinsi gani mfumo wetu wa demokrasia ulivyo na dosari, na dhahiri shahiri hakutakuwa na upinzani wa kweli ndani ya nchi hii, hivyo basi ni bora turudi kwenye mfumo wa chama kimoja ili tuweze kueleweka ni jinsi gani tunataka mfumo wetu wa utawala uwe, hii si dalili nzuri kwa nchi kama yetu ya Tanzania kwani tunaweza tukakaribisha machafuko na uvunjifu wa amani ambayo ni jambo pekee tunalojivunia nalo.

Hivyo basi tuombe sana tena sana, kuliko tulivyo omba wakati wa Corona ili tuepushwe na dhambi hii ya dhulma. Aameen.
Aamen
 
Musa alikuwa akizungumza na Mungu na alikuwa akiwaombea wana wa Izraeli ili watoke katika maisha ya kidhalimu chini ya utawala wa Farao na kwenda katika nchi ya ahadi, kwa bahati mbaya Musa aliwaokoa na Farao lakini hawakuweza kufikia lengo lao na wakaishi jangwani. Tatizo letu sisi watanzania hatuna kiongozi mwenye kuzungumza na Mungu, ndiyo maana tunataka kumuomba Mungu ili tuweze kufika katika Tanzania iliyo na mito ya maziwa na asali. Lakini kwa sasa amani ni muhimu.

Musa alikuwa akizungumza na Mungu na alikuwa akiwaombea wana wa Izraeli ili watoke katika maisha ya kidhalimu chini ya utawala wa Farao na kwenda katika nchi ya ahadi, kwa bahati mbaya Musa aliwaokoa na Farao lakini hawakuweza kufikia lengo lao na wakaishi jangwani. Tatizo letu sisi watanzania hatuna kiongozi mwenye kuzungumza na Mungu, ndiyo maana tunataka kumuomba Mungu ili tuweze kufika katika Tanzania iliyo na mito ya maziwa na asali. Lakini kwa sasa amani ni muhimu.

Nikukumbushe tu, hawakuishia jangwani bali walifika Kaanani ingawa aliyewafikisha hakuwa Musa bali Yoshua.
Kwa zama hizi Mungu hajidhihirishi kama wakati wa Musa bali anazungumza na watu wake kupitia unabii, ndoto ama ujumbe toka kwa mtumishi wake. Hivyo basi tuendelee kumuomba na tupunguze malalamiko dhidi ya “Musa” tuliyepewa kwani dhamira yake ni njema kabisa
 
Nikukumbushe tu, hawakuishia jangwani bali walifika Kaanani ingawa aliyewafikisha hakuwa Musa bali Yoshua.
Kwa zama hizi Mungu hajidhihirishi kama wakati wa Musa bali anazungumza na watu wake kupitia unabii, ndoto ama ujumbe toka kwa mtumishi wake. Hivyo basi tuendelee kumuomba na tupunguze malalamiko dhidi ya “Musa” tuliyepewa kwani dhamira yake ni njema kabisa
Basi tumsubiri Yoshua ili atufikishe Kaanani, kazi ya "Musa" imeshakwisha.
Maombi ni muhimu.
 
Back
Top Bottom