Tumuombee dua Prof. Janabi aishi maisha marefu, kinyume chake mafundisho yake yatapuuzwa, Taifa litaangamia kwa vitambi

mdukuzi

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2014
Posts
20,925
Reaction score
51,688
Mimi binafsi Sijawahi kuelewa mafundisho ya Prof Janabi,ni kama hataki tufe au hataki tufurahie maisha.

Yaani mtu eti Marufuku kula milo mitatu mara usile nyama nyekundu,juice,chaoati nk

Sasa ili mafundisho yake yakubalike tumuombee kwa Mungu atoboe miaka 90+ kinyume chake mimi na vichwa ngumu wenzangu tutaanza kula supu chapati saba kila siku tukishushia juice,soda ,maana tutajua alikuwa anatudanganya

Live longer Prof
 
Ni kweli uyasemayo ila naomba kuuliza kizushi, hivi kuna mtu kweli anafuata ushauri wa huyu Dk?
 
Yeye mwenyewe afya yake haisomeki utafikiria anashindia kashata
 
Hii kitu huwa nasema... Japo anayoongea ni kweli kabisa. Likimkuta yeye binafsi haimaanishi anayoyahubiri na kuyaishi si ya kweli.

Nimefanya extra restrictive diet anayoongelea. Ni ngumu, ina matokeo mazuri kiafya, ila inaua social life kabisa.

Nilikosa nidhamu ya kuifanya long term
 
Sasa kuna faida gani kuishi ikiwa social life imekufa?
 
Sio rahisi
 
Ukila utakufa na usipo kula utakufa pia. Furaia maisha yenyewe mafupi. Kaburini hakuna chakula
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…