Tuna chochote cha kujifunza toka Eurozone?

Tuna chochote cha kujifunza toka Eurozone?

Kigarama

JF-Expert Member
Joined
Apr 23, 2007
Posts
2,492
Reaction score
1,230
Ilikuwa ni Oktoba 19 mwaka 2009 wakati waziri Mkuu mpya wa serikali ya Ugiriki George Papandreou's alipotangaza kuwa Nakisi kwenye bajeti ya serikali yake itakuwa kubwa kuliko ilivyofikiriwa awali na nakisi hiyo itafikia asilimia 20 (20%) ya pato zima la taifa (GDP). Hapo ndipo mserereko wa uchumi wa Ulaya ulipoanza kushika kasi hadi kuweka kituo kwenye kufilisika kwa Mabenki ya Cyprus na kuparaganyika kwa ajira na uchumi wa nchi hiyo.

Kama taifa la Tanzania na mshirika mwenza kwenye kuanzishwa kwa sarafu ya pamoja ya Afrika Mashariki tuna chochote cha kujifunza toka Jumuiya ya Ulaya? Tumeweka mikakati gani ya kukabiliana na hatari kama zinazotokea kwenye nchi zinazotumia sarafu ya Euro (Euro zone)?

Chumi zetu zina uwezo wa kuanzisha sarafu ya pamoja au ni tamaa tu za kutaka sifa za kisiasa? Sera zetu za kifedha ziko imara kiasi gani na Benki zetu kuu ziko imara vya kutosha kwa sasa kusimamia ubadilishanaji, usafirishaji na uzungushaji wa fedha pamoja na usimamizi wa mikopo na riba toka kwenye tasisi za kifedha?
 
Kuna vitu tanzania tunaweza kujifunza in three key areas,

Suala la umoja wa kiuchumi ni tatizo kama hatujaweka misingi ya vp policies (nikimaanisha Monetary na Fiscal Policies) zinaweza kuwanufaisha wanajumuiya ndani ya umoja huo. Hili ni la msingi kwani Tanzania iko mbio kujiunga na nchi jirani kuunda jumuiya ya Afrika mashariki. Sasa bila ya kuwa makini kwenye policies husika tunaweza kujikuta katika matatizo huko mbeleni.

Suala jengine la kujifunza kutoka Eurozone ni ubaya wa kukopa. Mheshimiwa rais wetu ametuambia yeye haoni tatizo kukopa. But Tatizo la kukopa huwa halianzi siku moja au mwaka mmoja bali huanzia mbali. Zaidi huanzia pale ambapo nchi inapoanza kushindwa kulipa madeni yake. Tuchukulie mfano tunapokuwa tumeshaelemewa na madeni serikali itakuwa haina jinsi zaidi ya kuanza kutafuta njia kuwabana wananchi wake ili iweze kuyalipa madeni yake. Vile vile madeni huchangia kwa kiasi kikubwa kushuka kwa thamani ya sarafu ya nchi kwa sababu ya wasiwasi wa uhai wa uchumi wa nchi na mfumuko wa bei unaosababishwa na kushuka kwa sarafu ya nchi na hivyo kufanya bei za vitu kupanda (Mfano hai ni Greece, ambapo serikali ilipoelemewa hali ya maisha ikawa ngumu na ni ngumu hadi sasa na athari za madeni waliyokopa miaka 2000-2005 zimeanza kuwaumiza miaka ya 2009-hadi sasa).

Suala jengine tunaweza kujifunza ni kuwa corruption and tax evasion sio sifa au ujanja. Hii ni kwasababu mfano nchi kama Greece wananchi wengi walikuwa wanapenda kuevade tax ili wawe na hela nyingi. Vile vile corruption na bureaucracy imesababisha serikali kuwa na gharama kubwa za uendeshaji serikali kuliko mapato (Tanzania tunaweza pia kujifunza kutoka kwenye hili). Kubana matumizi sio dhambi ni moja ya njia ya kujidhibiti kipato. Serikali zisizo makini huwa haziwezi kubana matumizi matokeo ni kuelemewa na mzigo wa gharama (Hata Marekani nayo imeanza kubana matumizi). Tanzania uendeshaji wa serikali umekuwa mkubwa na wa kutisha na matumizi ya uendeshaji wa baadhi ya taasisi ni wa kusikitisha (Mfano matumizi ya V8 au V10 kama magari ya wakurugenzi na mawaziri ni mzigo usio na msingi kwani yako magari madogo yenye kuweza kufanya kazi kama hayo mfano Rav-4, Suzuki Escudo etc).

Naomba niishie hapo nitarudi nikiwa na muda kuchangia wacha niwaage.
 
Uzoefu wetu kwa nchi yetu hii pendwa ni kuwa suala linaloitwa kujifunza ni msamiati ambao mara nyingi sana hauonekani katika utendaji wake.

Toka maafa ya kiuchumi ya Greece 2009, wachumi wetu na wazalendo mbalimbali wameasa speed ya kuelekea shirikisho kuwa tuwe waangalifu na masuala tutakayoamua kuyaweka kwenye shirikisho hilo...

Na hadi kuna mda kumekuwa na shaka kuwa hii kasi huenda inasukumwa na mataifa makubwa na hii ndio shaka kuu, kama kasi hii ya muunganiko inasukumwa na wakubwa wa dunia itakuwa ngumu sana kwa watawala wetu kujifunza hata waone hatari gani....

Sisi kama taifa hata bila jicho la kiuchumi inaonekana wazi kuwa mifumo yetu ya fedha haijakaa sawa sana, wote tunakumbuka ni majuzi tu USD ilifika 1900 na kukawa na shinikizo (japo dogo kama kawaida yetu) kuwa Gavana wa BOT awajibike ila nayo ilipita kama upepo tu!
 
Kijakazi, Mchambuzi, jouneGwalu, Mdondoaji na Mchambuzi nakushukuruni sana kwa kuchangia!!

Hali kama ya Cyprus ambapo ukubwa wa benki kifedha ulizidi ukubwa kifedha uchumi wa nchi ya Cyprus mara saba zaidi, kwa hapa kwetu hatutafika huko?

Kila Jambo lina sababu, na hivyo kuna sababu kwa nini sisi tuko jinsi tulivyo!

Ninachomaanisha ni kwamba ni kwa nini tuko hapa tulipo kama jamii, ni kwa nini tunashindwa kwenda mbele kama jamii nyingine!

Kuna sababu kwanini sisi tulitawaliwa na kuuzwa Utumwani na watu wengine, kuna sababu kwa nini mpaka leo tunaendelea kuuza nchi yetu na Ardhi yetu kwa Wageni, na ndio maana mimi nasema tatizo letu Tanzania SIYO CCM au sijui Kiongozi fulani, bali ni SISI wenyewe kama Jamii! Unaweza kufikiri labda nimetoka nje ya Mada lkn najaribu tu kuelezea ni kwa nini tunashindwa kutatua Matatizo hata yale madogo kabisa!

Umeongelea kuhusu Sarafu Moja na Jumuiya ya Afrika Mashariki, Viongozi wetu wanakwenda kusaini Mikataba wasiyoielewa, Kwa nini? Jibu lake ni moja tu, ni kwamba Viongozi wetu ni kama sisi tulivyo pia hawaoni umuhimu wa kusimamaia Maslahi ya Nchi kama sisi tu tulivyo ktk maisha yetu ya kila siku, na Watanzania wengi pia wangefanya hivyo hivyo na kuchukua maamuzi hayo hayo wanayochukua Viongozi wetu!

Hivyo watu watapiga kelele Wanavyotaka, watalaumu wanavyotaka, watabadilisha Viongozi wananvyotaka, watabadilisha Vyama wanavyotaka, lkn mwisho wa siku hakuna Jipya hata ulete Katiba sijui ya wapi!
 
Nilitaka kuona kama kuna uwiano kiasi gani kwenye kuuza na kununua (Balance of payment) Bidhaa nje ya nchi kwa nchi wanachama wa Afrika Mashariki.

Kwa maana kwa EU ni Ujerumani yenye uchumi Imara ndiyo inabeba zigo lote la kutikisika kwa uchumi kwa kanda hiyo na yenyewe ilikuwa Kilongola (Pioneer) wa kuacha kutumia sarafu yake (Deutschmark) ili kuhamasisha nchi nyingine kujiunga na sarafu ya Umoja wa Ulaya (Euro) jee kwa Afrika Mashariki ni nchi gani itaibeba sarafu ya umoja?
 
Hali kama ya Cyprus ambapo ukubwa wa benki kifedha ulizidi ukubwa kifedha uchumi wa nchi ya Cyprus mara saba zaidi, kwa hapa kwetu hatutafika huko?

Kinachotokea ni kuwa "Uovu/ubovu hutawala kwa watu wema/wenye hekima/busara kukaa kimya au kufanya kama hayawahusu"

Kama Cyprus walikuwa na kitu cha kuwapa kiburi kiasi hicho, ni afadhali zaidi je tujiulize sisi nje ya baadhi ya viongozi kuwa na ndoto za kuwa marais wa jumuia ya africa mashsriki je ni kipi cha ziada kipo kwenye nchi hizo mahususi Tz, tuna nini??

Wananchi wasio na nguvu za mitaji na utoshelevu kwenye soko japo la mikoa yao tu.....

Sekta binafsi isiyo na uwezo wa japo kukidhi huduma kwa wateja tu...

Sekta isiyo rasmi iliyokubwa na kuparaganyika kabisa kiasi cha kupoteza tija kwenye sura ya maendeleo endelevu ya nchi in long and short run!!

Africa kuna mambo asee.
 
jouneGwalu sioni kama kuna watu kwa umakini kabisa wanajadili taathira ya asilimia zaidi ya 98 ya Ardhi yetu kutopimwa, jee maisha ya baadaye ya watanzania yatakuwaje. Hivi kiasi kikubwa namna hiyo cha ardhi kutokupimwa tafsiri yake ni nini, madhara yake kwa watanzania ni yepi? Wanasema eti hawatahusisha Ardhi kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki. Hawa si wanajidanganya!?
 
Mkuu Kigarama

Kabla sijaanza kuchangia ningetoa ombi kwako mada kama hizi ni vyema na haki kama ungewaalika vichwa vya ukweli wa JF ili tuweze kupata michango yao maridhawa kwa heshima na kwa ruksa yako naomba kuwaalika wafuatao Nguruvi3,
JokaKuu, Mzee Mwanakijiji Mchambuzi sweke 34, Jasusi, Pasco, Ab-Titchaz, Mkandara, EMT, Kichuguu, Mwita Maranya, Matola, Ritz, Kabonde, Zakumi, Ogah, Rutashubanyuma, Mag3, AshaDii, Katavi, zumbemkuu ...........

Mkuu Kigarama yapo mambo mengi sana tunayoweza kujifunza kuhusiana na kuyumba kwa kwa uchumi kwa baadhi ya nchi za umoja wa nchi za ulaya.

Ifahamike wazi nchi mwanachama wa EAC ni masikini kwa vigezo vyote ukizilinganisha na nchi za ulaya,hata yale mataifa yenye uchumi mdogo(mbovu) barani ulaya bado ya nguvu kubwa za kiuchumi GDP ukiinganisha na mataifa mengi ya Afrika.Serekali zetu za kiafrika Tanzania na EAC zikiwemo hazina mipango ya muda mrefu na kati ya kukuza uchumi(Fiscal Policy & Monetary policy). That is how funds are allocated taxation policies,government spending, funds distribution throughout each segment of economy and control the supply of money.

Nchi mwanachama wa EA hazina sera zilizobuniwa na wataalamu wake zinazolenga kuwakomboa jamii kubwa ya wananchi wake, badala yake mataifa yote ya Afrika mashariki yanafuata sera za WB & IMF. Kwa hakika policies za WB na IMF hazijawahi kuondoa umasikini mahali popote duniani. Nchi za Asia pamoja na kufuata baadhi ya sera za IMF na WB bado zilikuwa na policies zao za ndani ambazo zililenga kuziondoa katika umasikini kwa kuangalia mazingira ya nchi zao.

Nchi zote mwanachama wa EA zinaendesha serekali kwa kukopa lakini kwa viwango tofauti. Nchi kama Rwanda inakopa lakini fedha zake nyingi zinaelekezwa kwenye Investments wakati Tanzania fedha nyingi zinapelekwa kwenye mishahara, posho, safari za viongozi, semina, ununuzi wa magari ya kifahari kwaajili ya viongozi wakuu, pensheni kubwa kubwa kwa viongozi wakuu ie Rais, waziri mkuu, mawaziri, makatibu wakuu,wakuu wa mashirika ya umma, wakuu wa vitengo mbali mbali na hili limetokea huko Ugiriki. Uchaguzi wa Kenya uliambatana na matumizi makubwa ya fedha pasipo sababu za msingi fedha zilizotumika wakati wa uchaguzi zingelekezwa kujenga nchi.

Ufisadi unatafuna mataifa mengi ya Afrika hasa Tanzania. Tumeona na kushuhudia wezi wa mali za umma wakipeta mitaani bila kuchukuliwa hatua stahiki. Wengine wakipewa uongozi utafikiri uhalifu walioufanya ni jambo jema.

Nafikiri bado mataifa ya EA hayajafikia kiwango cha uchumi uliotengema kuhimili sarafu moja. Nchi kama Burundi inashindwa kutoa hata michango kwaajii ya shughuli za uendeshaji wa jumuiya sasa litakapokuja suala la sarafu moja uenda tukazalisha Ugiriki nyingine.

Unapokuwa na sarafu moja maana yake ni pamoja na kiwango cha kukopa baina ya nchi wanachama kuwa kimoja kilichokubaliwa. Je, Tanzania tuna nidhamu ya kutosha katika matumizi ya uendeshaji wa serekali. Je, viwango vya kukopa tutaviweza au tumezoea kumwamrisha Prof Ndullu achapishe fedha hovyo.
 
Last edited by a moderator:
Ngongo umefanya uchambuzi mzuri sana. Unamaanisha kwamba kuanzisha sarafu moja ya Afrika Mashariki ni jambo la Uendawazimu!?
 
Kijakazi, Mchambuzi, jouneGwalu, Mdondoaji na Mchambuzi nakushukuruni sana kwa kuchangia!!

Hali kama ya Cyprus ambapo ukubwa wa benki kifedha ulizidi ukubwa kifedha uchumi wa nchi ya Cyprus mara saba zaidi, kwa hapa kwetu hatutafika huko?

Kuhusu cyprus, it is the after math or domino effect of the Greek crisis. Cyprus banks waliwekeza sana kwenye kukopesha Ugiriki na ilipoamuliwa kuwa Benki kuu ya ulaya kufuta madeni benki za cyprus zimejikuta zimeumia kibiashara kutokana na kiwango cha uwekezaji kwenye sekta ya fedha ya ugiriki.

Inasemekana Cyprus encountered a loss of Euro 24 Bill. Vile vile mzunguko wa fedha za kigeni kwenye uchumi wa Cyprus ni mkubwa kuliko mzunguko wa uchumi wa Cyprus. Hilo ni tatizo ambalo linaweza kuleta mtikisiko kwani kinachoonekana ni kwamba fedha za watu ni nyingi kuliko fedha zinazotokana na serikali. Kwa maana hiyo benki kuu ya Cyprus haiwezi kuzinasua benki za biashara pindi zikiwa zimefilisika.

Tunajifunza kitu gani katika hili ni kuwa Cyprus ilikubali masharti ya monetary union ya EU pasina kufahamu athari zake kwenye uchumi wake. Hili likasababisha balooning of the banking system na capital inflows in the banking sector but at the expense of a little growth kwenye sector nyenginezo za uchumi kama uzalishaji na kadhalika.

Tanzania ni vema tukawa waangalifu, kwenye sarafu pamoja na umoja wa kiuchumi. Maswali ya kujiuliza ni je sarafu ikiwa moja inaathari gani kwenye purchasing power ya shilling? Ina athari gani kwenye cost of living nk. Tusipokuwa makini tunaweza kuungana sarafu halafu tukaishia kuongeza mfumuko wa bei nchini, gharama za kuishi zikapanda na pia tukaua hata vile viwanda vyetu vidogo vilivyobakia.

Ndio sababu nilishawahi kusema zamani kwenye mada ya muungano wa afrika mashariki kuwa Tanzania ni vema ikawa kama Uingereza tuuungane kwenye mambo tunayoyaona tutafaidika na sio kila kitu. Tutaumia !
 
Mkuu Kigarama haswa, EU sasa inabebwa na Germany kwa kiasi kikubwa na hili si kwamba wamependa ila wanajua walifanya kosa waliopokubali dutchmark ife kwa faida ya euro kitu ambacho UK walikikataa.

France na Italy nazo zinawajibika kwa kiasi chake usisahau hapo hapo uchumi wa Italy unayumba wakati huo huo Italy ni nchi ya tatu kwa kuwa na uchumi mkubwa Ulaya.

Usisahau Norway na mafuta yake haikutaka kuburuzwa na umoja wa ulaya sisi tuna gesi, ardhi, madini tunaonekana tunaburuzwa na Kenya, Rwanda, Burundi ambazo zinaukosefu mkubwa wa ardhi.

Ngongo umefanya uchambuzi mzuri sana. Unamaanisha kwamba kuanzisha sarafu moja ya Afrika Mashariki ni jambo la Uendawazimu!?
 
Mada nzuri sana!

Tunayo mengi ya kujifunza kama ifuatavyo :
1. Mikopo isipotumika na kurudisha faida ni hasara kwa nchi
2. Ni muhimu tu-expanda foreign reserve capacity yetu. Hii itatusaidia kuwa na uwezo wa kuagiza bidhaa muhimu nje ya nchi na kubakiza kiwango stahiki kwa ajili ya matumizi ya baadaye na uwekezaji

Nitarudi baadaye
 
Ngongo umefanya uchambuzi mzuri sana. Unamaanisha kwamba kuanzisha sarafu moja ya Afrika Mashariki ni jambo la Uendawazimu!?

Kuwa na sarafu mmoja,

Kunaweza kuwa na faida na vile vile hasara. Tanzania inaweza kuwa kwenye hasara zaidi kwa vile hatuna viwanda vya kutosha, window of developing into the petro-chemical sector (mafuta na gesi), uwezo wa sekta ya benki na fedha kukua, large population na amani ya muda mrefu. Hivyo tusiangalie tu hasara labda tufanye comparative of benefits and loss.

Ila mtazamo wangu unaweza kuungana na Ngongo ya kwamba Tanzania stands to loose in the currency union. Naweza kuwa siko sahihi but huo ni mtazamo wangu.
 
These are some of the arguments put forward against Britain joining the Euro


Currency unions have collapsed in the past. There is no guarantee that EMU will be a success. Indeed the Euro may be a recipe for economic stagnation and higher structural unemployment if the European Central Bank pursues a deflationary monetary policy for Europe at odds with the needs of the domestic UK economy.

It is quite possible that the monetary union will not be sustainable; countries that discover themselves to be in difficulty may cancel their membership and re-establish an independent currency and an inflationary monetary policy. The example of Ireland’s departure from the sterling currency area suggests that leaving a currency union is beneficial, rather than joining one.

In theory, a currency union can offer economic benefits – but only under fortunate circumstances. The lack of exchange rates removes a very effective mechanism for adjusting imbalances between countries that can arise from differential shocks to their economies. History demonstrates that well-chosen devaluations can help an economy out of difficulties – the UK should retain this option.

In a recession, a country can no longer stimulate its economy by devaluing its currency and increasing exports.

The EMU is a step in a process that will cut Europe off from the rest of the world. It is bureaucratically motivated – a further advancement for European policy makers.

Entry would mean a permanent transfer of domestic monetary autonomy to the European Central Bank implying giving up flexibility on exchange rates and short-term interest rates. Domestic monetary policy would no longer be able to respond flexibly to external economic shocks such as a rise in commodity price inflation.

The UK is thought to be more sensitive to interest rate changes than other EU countries – in part because of the high scale of owner-occupation on variable-rate mortgages in the UK housing market. Joining a currency union with no monetary flexibility requires the UK to have more flexibility in labour markets and in the housing market. The UK rented sector is too small to be a flexible substitute for owner-occupation. The UK has instituted within the Bank of England a very effective apparatus for managing interest rates. The EMU will remove this policy lever, along with removing the opportunity for exchange rate policy.

Substantial fiscal transfers will be needed for poorer countries within the EU along with a more activist European Regional Policy to reduce structural economic inequalities. The UK might not feel able to afford such large-scale intra-European transfers.

The lack of any coordination between European monetary policy, emerging from a committee of central banks, and European fiscal policy, emerging from a committee of finance ministers, will further lessen the possibility for alleviating local economic difficulties. This can be shown with the South-North migrations of millions of American and Italian citizens in the early years of their currency unions.

The Euro will not be an optimal currency area – the European economies have not converged fully in a real structural sense and at some stage in the future, there is a fear that excessively high interest rates will be set because of an inflationary fear in one part of the zone which is unsuited to another area.

There are economic costs and risks arising from losing the option to devalue the domestic currency in order to restore international competitiveness. This might lead to growing social dislocation and rising economic inequality within the European Union.

There are fears about which countries might dominate the workings of the Central Bank and the effects on monetary policy within Europe if there are different inflation psychologies between member nations.

There are obvious structural differences within the countries of Europe so, even if EMU begins in a state of convergence, economic shocks, such as crisis of supply of primary products, will lead to imbalances and there will be no mechanism to restore the balance.

Since there will only be a Europe-wide interest rate, individual countries that increase their debt will raise interest rates in all other countries. EU countries may have to increase their intra-EU transfer payments to help regions in need.

It may prove more difficult to sustain a currency union than to begin one. The EC tax revenue is only 1.5% of the gross domestic product, which is an insufficient basis for an effective system of re-distributive taxation. In the event of differential prosperity within Europe there can be no confidence that the more fortunate countries will permit a greater degree of re-distribution. For so long as the UK market structures remain susceptible to bouts of inflation, the move to a low European interest rate regime could prove to be very damaging.

There is no reason why the UK should not continue to attract foreign capital inflows even if initially outside the new currency arrangement.

Adjusting to a new European currency will involve substantial costs for businesses and banks. Adjustment to economic divergence by migration of labour or capital will be costly; there is no clear EC commitment to relieving these costs.

There are almost no instances in modern times of a newly formed fixed exchange rate regime surviving for more than five years.

See more: What are the arguments for and against joining the Euro
 
jouneGwalu sioni kama kuna watu kwa umakini kabisa wanajadili taathira ya asilimia zaidi ya 98 ya Ardhi yetu kutopimwa, jee maisha ya baadaye ya watanzania yatakuwaje. Hivi kiasi kikubwa namna hiyo cha ardhi kutokupimwa tafsiri yake ni nini, madhara yake kwa watanzania ni yepi? Wanasema eti hawatahusisha Ardhi kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki. Hawa si wanajidanganya!?

Mkuu wangu hapo awali nilivyoanza kuutazama mjadala huu nilidhani umelenga sana kwenye uchumi wa kifedha hivyo nikaweka kando kuguswa kwangu na suala la ardhi.....

Kwenye bold nyekundu naomba uambatanishe na hoja za wabunge juu ya ugawaji wa holela wa ardhi kwa mikataba ya mda mrefu kwa wawekezaji isiyo na tija ya maana sana, hili ni zaidi ya Janga.....

Nafasi yetu katika jumuia kama tukiingia kichwakichwa hivi ni wazi kuwa tutapigwa bao sababu majirani zetu wengi kwao ardhi ni suala la vita kwa kunyang'anyana tofauti na kwetu......

Najua kuna watu watakuja na data za kutoka wizarani hapa juu ya zoezi la upimaji wa ardhi ili tu kutughiribu kuwa serikali inafanya kazi lakini kiukweli na kiuhalisia kinachoendelea ni uhuni tu raia wa kawaida tu tunaweza kutoa ushuhuda jinsi hata kupata kiwanja cha makazi kilichopimwa ilivyokuwa songombingo.
Nimewahi kujaribu kupigania viwanja vya Kibada, nilikesha pale Temeke ila holla!!!

Vikaja viwanja vya Kibaha eti hadi wanatangaza kwenye radio viwanja ambavyo idadi yake haizidi elfu 5.... huu ni zaidi ya uhuni.

Nimechukulia hiyo kama mifano tu kuonyesha kuwa kinachojazwa kwenye karatasi za wizara ni tofauti sana na hali halisi mtaani na kwa wananchi wa kawaida au umwite mjasiriamali mdogo ambaye kesho inabidi aboreshe mtaji kwenda sokoni kushindana kwenye jumuia.

Baada ya hayo machache unaweza kuona wazi kuwa hicho kitu cha kwenye bold bluu ni hakionekani kama kipo kwenye nchii yetu ambapo utawala umeamua kupeleka mambo utafikiri wamewasiliana na shetani na amewahakikishia kuwa sisi ndio kizazi cha mwisho kuwa baada ya sisi basi hii nchi TZ itakuwa imefutika na hamna atakaye baki..... inasikitisha sana
 
Mkuu jouneGwalu hapo ndipo utamkumbuka Nyerere.

Safu ya uongozi wa sasa watazama leo kesho itajijua yenyewe. Tazama migogoro ya kidini tulisema tangu mwanzo wanasiasa wanatumia dini lakini ipo siku yatawageuka leo udini uko wazi sababu ni watawala.
 
Suala la kuwa na single currency katika EAC linachukuliwa kirahisi sana. Labda tungejiuliza nini kiliua EAC currency Board mwaka 1966.

Kwa wenzetu wa Ulaya, hilo wamejaribu lakini inavyoonekana limeleta tatizo sana. Waingereza walikataa single currency kwa uhafidhina lakini sasa hivi inaonekana waliona mbali.

Inaweza kuwa ni ‘happy accident' kwamba walitaka ku-maintain status ya Queen na traditional na sasa inaonekana kuwa kama werevu.

Hata hivyo mdororo wa uchumi Ulaya unawaathiri vilivyo. Kuna proposal ya D. Cameron kuwa UK ijitioe katika UE kwasababu inakuwa victim wa uzembe wa wengine.

So far nchi inayo ''baby seat'' wengine ni German ambayo nayo kuna internal pressure kuwa haiwezi kuwa mlezi wa nchi zisizo wajibika.

German inafanya hivyo kwa kuzingatia vitega uchumi vyao ambavyo kuiacha nchi kama ukgiriki kuanguka kiuchumi itawaathiri wao wenyewe.

Kitu kizuri ni kuwa hizi nchi za Ulaya zina uwezo wa ku-bail out nchi zisizojiweza. Kwetu sisi sote ni wapitisha bakuli WB na IMF.

Nchi moja itakapokuwa katika matatizo nani ataokoa jahazi? Hapo kama si kusambaratika sijui itakuwaje.

Mimi nilidhani kuwa kabla ya kuwa na single currency tulipaswa tuwe na institutions imara kwanza. Tuwe na uwiano wa kodi, tuimarishe usafiri, tuwe na health system pamoja na eduction ambazo zinasimama kwanza zenye.

Tunapaswa tuwe na strong Central bank zitakazokuwa na mkakati wa kuangalia uchumi kwa pamoja kwanza kabla ya kuingiza single currency.

Sasa hivi tunatatizo la visa kwa nchi hizi na halionekani kupata ufumbuzi, it's unlikely issue kama ya single currency inaweza kuwa practical at the moment.

Ulya bado tatizo lipo kuna Greece, Cyprus, Spain, Italy zipo katika hali mbaya.

Kama ulivyosema Kigarama tunajifunza nini kutokana na hili
 
Kuna mambo kadhaa ambayo tunaweza kujifunza kutoka eurozone. Ningependa zaidi kutumia matukio ya Cyprus kufafanua. Kwanza, ni muhimu tukaelewa kwamba kinachoendelea nchini Cyprus ni collapse ya mfumo wa fedha/banking system kutokana na fedha nyingi kutoweka katika mzunguko, hali ambayo imeathiri availability of credit/mitaji to finance businesses ambazo ni key katika kutengeneza ajira katika taifa, kuchangia kuongezeka kwa kwa mapato ya ndani taifa kupitia income and corporate taxes, na pia kuongeza pato la la taifa (GDP). Cyprus imeathirika katika maeneo yote haya matatu. Kuna mambo kadhaa ambayo tunaweza kujifunza lakini kwa sasa nitajadili machache:

Kwanza, hii ni ‘wake up call na reminder’ kwamba hoja ya Zitto bungeni mwaka jana (2012) kuhusu fedha chafu ma madhara yake katika uchumi ilikuwa ni hoja muhimu sana kwa maana ya kwamba mzunguko mkubwa wa fedha nchini Tanzania ni aidha wa fedha chafu au fedha zisizo rasmi au vyote kwa pamoja. Fedha za namna hii ni vigumu kuzidhibiti na zina tabia ya umalaya kwa maana ya kwamba zina hama hama kutokana na tamaa na uwoga, kwa mfano leo hii tunaweza kuwa na fedha nyingi sana ambazo zinajenga magorofa na kutoa ajira kwa watu, lakini kesho, just out of speculation hata za kizushi, fedha hizi zinaweza kutoweka katika mzunguko na kupelekea kuanguka kwa mfumo mzima wa fedha ndani ya taifa;

Kwahiyo, kinachoendelea nchini Cyprus ni meltdown ya mfumo wa kifedha/kibenki; je nini kimechangia sana? Tufahamu kwamba Cyprus ni moja ya nchi maarufu za kutunza fedha za mafisadi, fedha nyingi haramu na matajiri wakwepa kodi kwa ujumla kutoka sehemu mbalimbali duniani – offshore accounts, hivyo fedha zake nyingi zilizokuwa katika mzunguko zilitokana na fedha hizi “Malaya”; Nyingi ya fedha hizi zilikuwa zikiwekezwa katika Sokola Hisa - Stock Exchange ya Cyprus kama Portfolio Investments; Tukumbuke kwamba kuna aina mbili ya financial flows (investments) kutoka katika nchi moja kwenda nyingine– Kwanza ni Foreign Direct Investments (FDI) ambapo wawekezaji uenda kuwekeza katika ujenzi wa viwanda, migodi, na makampuni mbalimbali ya kuzalisha bidhaa na kutoa huduma; aina ya pili ya foreign financial flows ni Foreign Portifolio Investments (FPI) ambapo matajiri halali, mafisadi, wauza madawa ya kulevya n.k na wakwepa kodi uingiza fedha zao katika uchumi husika na kujiingiza katika mchezo wa kutengeneza faida haraka hasa kwa kununua na kuuza hisa katika soko la hisa (stock exchange) ndani ya uchumi/taifa husika;

Foreign Portifolio Investments (FPI) ni fedha Malaya kama nilivyojadili, na ni fedha za mguu mmoja ndani, mguu mmoja nje kutokana na mazingira yake kutawaliwa na uwoga, tama na kila aina ya uchafu, kwahiyo speculation zozote hata ambazo hazina msingi kama vile tetesi kuhusu hatua za serikali husika kuja na masharti magumu ya kudhibiti feddha chafu, au tetesi kuhusu machafuko ya kisiasa n.k, hupelekea wenye fedha za namna hii kufanya maamuzi ya kuzihamisha over night hivyo kuzitoa kutoka katika mzunguko wa kifedha ndani ya uchumi husika na kuzipeleka kwingine; sasa kama uchumi wa nchi husika unategemea sana fedha za namna hii katika mzunguko wake wa fedha, kinachofuata ni disaster katika mfumo na mzunguko wa ndani wa fedha; Lesson nyingine hapa ni kwamba Financial inflows nzuri na zenye maana kwa uchumi legelege kama wetu au uchumi wa taifa kama Cyprus ni zile za FDIs- Foreign Direct Investments ambazo zinaenda kuwekeza katika uanzishwaji wa makampuni, biashara ambapo jobs get created, hivyo kuchangia ongezeko la makusanyo ya kodi na GDP ya nchi; Fedha zinazoingia kwa mtindo wa FDI hazibabaishwi na ‘mere speculations’ kama fedha Malaya za FPI;

Suala jingine ambalo ambalo ningependa kulijadili linahusiana zaidi na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ambayo baadhi ya wadau humu wameijadili katika muktadha wa mada husika. Katika hili, pengine kutoka kwangu zaidi ni pendekezo kwamba tunapoongelea East Africa Monetary Union/Sarafu Moja katika jumuiya ya afrika mashariki, nadhani muhimu tukafanya hivyo kwa kulenga zaidi katika uchambuzi wa fursa na changamoto zilizopo katika muungano wa kiuchumi (economic integration) in a holistic manner (sio kivipande vipande), huku tukitambua kwamba muungano wa kiuchumi baina ya nchi wanachama husika popote pale hupitia hatua nyingi – kuna hatua za mwanzo na hatuo za mwisho, huku kila hatua ikitoa fursa, faida, hasara zake na changamoto zake; Hivyo ndivyo tutaweza kuwa na mjadala wa maana juu ya wapi tunataka kwenda n.k; Tatizo lililopo ni kwamba kuna utamaduni wa watawala fulani fulani katika Jumuiya yetu wa aidha ya kuzuia a speedy process kutoka hatua moja ya economic integration kwenda hatua nyingine kwa sababu za kizalendo, lakini pia wapo wanaofanya hivyo kwa sababu za kisiasa; Vilevile wapo baadhi ya watawala ambao wana harakisha mchakato wa muungano wa kiuchumi kutoka hatua moja hadi nyingine kwa sababu za kizalendo, na pia wapo ambao wanafanya hivyo kwa sababu za kisiasa; Lakini mbaya zaidi ni kwamba tunarudi katika tatizi lile lile ambapo POLITICS IS SUPREME TO EVERY COMMON SENSE AND RATIONALITY, INCLUDING ECONOMICS;

Kama nilivyosema hapo awali, muungano wa kiuchumi hufuata hatua kadhaa, na hatua hizi zipo saba, huku kila moja ikiwa na fursa zake, faida zake, hasara zake na changamoto zake; Kwahiyo katika muktadha wa EAC huku tukizidi kujifunza kutoka Eurozeone experience, nadhani ni muhimu tukatumia framework ya mchakato wa muungano wa kiuchumi kujadili fursa, faida, hasara na changamoto za kila hatua za mchakato husika, kama vile Monetary Union n.k. Hatua za mchakato wa muungano wa kiuchumi ni kama ifuatavyo:

Awali kabisa ni Preferential Trade Area (PTA); PTA ni ‘ a trade block’ baina ya nchi wanachama ambapo nchi husika hupeana upendeleo katika eneo la kodi za bidhaa Fulani Fulani watazokubaliana (sio bidhaa zote), lengo hasa ikiwa ni kupunguziana viwango vya kodi katika bidhaa husika ili to stimulate trade, jo creation, GDP, n.k; Swali linalofuata ni je – ni watanzania wangapi wenye uelewa juu ya jinsi gani PTA imekuwa ‘in effect’ katika EAC na je inawapa fursa gani? Faida gani? Hasara gani? Changamoto gani? Pia je, Serikali ina mikakati gani ya kulinda uchumi wetu dhidi ya economic shocks zinazoweza kujitokeza?

Hatua ya Pili ni Free Trade Area (FTA) ambayo nayo ni ‘a trade block’ baina ya nchi husika; FTA ina elements za PTA lakini FTA inaenda mbali zaidi kwani nchi wanachama hukubaliana kufuta kabisa kodi, import quotas katika bidhaa na huduma nyingi watazokubaliana (sio zote); Swali linalofuatia ni kwamba je - ni wananchi wangapi wenye uelewa juu jinsi gani FTA imekuwa in effect katika EAC na je inawapa fursa gani? Faida gani? Hasara gani? Changamoto gani? Pia je, Serikali ina mikakati gani ya kulinda uchumi wetu dhidi ya economic shocks zinazoweza kujitokeza?

Hatua ya tatu ya muungano wa kiuchumi ni ‘Customs Union’ – hapa nchi wanachama wanakubaliana kwa pamoja kuweka viwango sawa vya kodi kibiashara dhidi ya mataifa ambayo sio wanachama wa trade block yao; Hii hufanya mataifa nje ya trade block yenu yasibague wanachama wengine kutokana na wengine katika trade block yenu kuwa na viwango vikubwa vya kodi kwani kwa kawaida, nchi nje ya trade block yenu watakimbilia nchi zenye viwango vidogo vya kodi and vice versa holds; katika hili, iwapo Tanzania na nchi za SADC au EAC wangeamua kuwa na viwango sawa vya kodi, lakini hasa kukataa upuuzi wa tax exemptions kwa wawekezaji wanazopewa kwa miaka mitano (mfano rejea jinsi gani mahoteli makubwa yanavyobadili majina kila baada ya miaka mitano), tungekuwa katika nafasi bora zaidi kiuchumi. Swali linalofuata ni je – watanzania wangapi wanaelewa fursa, hasara, faida na changamoto za mfumo huu katika jumuiya yetu ya Afrika Mashariki? Pia je, Serikali ina mikakati gani ya kulinda uchumi wetu dhidi ya economic shocks zinazoweza kujitokeza?

Hatua ya nne ni Common Market au Single Market – katika hili, kunakuwa na common policies za uendeshaji biashara na regulations katika uendeshaji biashara, lakini hasa uzalishaji; Hapa pia kunakuwa na free movement ya factors of production (Labor, Capital, Services na Enterprises) baina ya wanachama wa trade block husika; Lengo kuu hapa ni kuondoa kila aina ya vikwazo vya kibiashara baina ya nchi wanachama vinavyotokana na jiografia (mipaka), kodi, technical /standards requirements n.k; Swali linalofuata ni je – watanzania wangapi wanaelewa fursa, hasara, faida na changamoto za mfumo huu katika jumuiya yetu ya Afrika Mashariki? Pia je, Serikali ina mikakati gani ya kulinda uchumi wetu dhidi ya economic shocks zinazoweza kujitokeza?

Hatua ya Tano ni Economic & Monetary Union – huu ni mchanganyiko wa hatua zote za awali hapo juu PLUS uanzishaji wa sarafu moja (common currency); Swali linalofuatia ni je - watanzania wangapi wanaelewa fursa, hasara, faida na changamoto za mfumo huu katika jumuiya yetu ya Afrika Mashariki? Pia je, Serikali ina mikakati gani ya kulinda uchumi wetu dhidi ya economic shocks zinazoweza kujitokeza? Monetary Union ni moja ya mijadala mikali hivi sasa ndani ya EAC…

Hatua ya Sita ni Fiscal Union – hatujafikia hatua hii lakini hapa maana yake ni muungano wa fiscal policies (kodi na matumizi ya mapato ya kodi) baina ya wanachama ambapo maamuzi kuhusu ukusanyaji kodi na matumizi ya fedha za walipa kodi yanakuwa centralized kupitia Benki Kuu moja that serves all members; mfano mzuri ni Federal System ya USA – FRB; Swali linalofuatia ni je – tukija fikia huko, watanzania wangapi wanaelewa fursa, hasara, faida na changamoto za mfumo huu katika jumuiya yetu ya Afrika Mashariki? Pia je, Serikali ina mikakati gani ya kulinda uchumi wetu dhidi ya economic shocks zinazoweza kujitokeza?

Hatua ya mwisho ni Full Integration ambayo inahusiana zaidi na Political Integration; Swali linalofuata ni je - watanzania wapo tayari kwa hili? Na ni wangapi wanaelewa fursa, hasara, faida na changamoto za hatua hii katika jumuiya yetu ya Afrika Mashariki?

Kwa mtazamo wangu, nadhani tukitumia framework hii kujadili lessons from EU kwa jumuiya yetu yaAfrika mashariki, tutakuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kuelewa juu ya faida, hasara, changamoto na fursa mbalimbali za kiuchumi zinazotukabili sasa na zitazotukabili baadae katika muktadha huu wa EAC, hivyo kutupatia fursa nzuri zaidi ya kuja na mikakati mbalimbali ya kukabiliana na changamoto husika kwa ajili ya maendeleo yetu na ya vizazi vijavyo;
 
Back
Top Bottom