#COVID19 Tuna la kujifunza; Mama Mghwira mwaka alijitangaza kuumwa Corona na kupona, lakini mwaka huu...

#COVID19 Tuna la kujifunza; Mama Mghwira mwaka alijitangaza kuumwa Corona na kupona, lakini mwaka huu...

mngony

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2012
Posts
5,555
Reaction score
6,972
Japo ukweli unabaki wewe mwenyewe ndio unawajibika kwa afya yako, hivyo wewe ndio muamuzi wa jambo lolote kuhusiana na afya yako na wala mtu mwingine asikuchagulie linalohusiana na afya yako

Kufutia kuumwa kama tulivyoambiwa na familia ugonjwa wa changamoto ya kupumua, Mama yetu Mghwira Mungu alimpenda zaidi siku kadhaa nyuma, lakini tukumbuke mwaka jana mwezi wa nne wakati wa wimbi la pili alijitangaza kuumwa na hatimae kupona corona na hata kutoa wimbo kushukuru Mungu.

Screenshot_20210726-204841_Twitter.jpg








Lakini mwaku huu, wimbi la tatu la maambukizi ameumwa tena lakini Mungu alimpenda zaidi

Nitoe pole kwa familia, ndugu na wote walioguswa

Japo sio vizuri lakini tunajifunza kuwa kama umri umeenda sana, au una magonjwa ya muda mrefu kama vile Sukari na mengine yenye kudhoofisha mwili na kupunguza kinga ni vizuri ukachukua tahadhari kubwa kadri uwezavyo kwa sababu ukishakuwa katika hiyo hali ni rahisi kuumwa sana na hata ikatokea ukapona maana yake wimbi likija tena uwezekano wa kupata na kuumwa sana( kupata numonia ya corona) unakuwa uko palepale, tena inakuwa hatari zaidi kwa sababu athari za corona kufika kwenye mapafu huwa ni zinabaki muda mrefu hata baada ya kupona

Kama uko katika hayo makundi hatarishi, achana na hizi siasa chagua mwenyewe mustkabali wa afya yako chukua tahadhari mwenyewe, usije ukachukua ushauri wa mtu mwenye 20s to 40s ambaye shida yeyote kiafya ambaye akipata maambukizi anaishia na kifua na labda na homa siku 3 anapona ukafata wewe mwenye 40s na kuendelea huku ukiwa na magonjwa kama sukari n.k

Tukumbuke haya maambukizi yataendelea kuja wimbi baada ya wimbi, yanakuja yanasambaa kwa kasi na kuathiri wengi baadae hali inatulia na kuanza tena kwa hiyo ni suala muda mrefu

Wewe uliye kundi hatari chukua tahadhari zote hata ukiona kuchanja ni muhimu kwako chanja ukiona haina acha. Na wengine ambao hatuko kundi la hatari tuwalinde walio kundi hatari
 
Huyo mama amekufa kwa mengi...corona yaweza kuwa ni njia tu.

Ila mtambue hizi kazi hasa za uteuzi kuwa mguu sawa tu. Ndiyo maana viongozi wengine huwa hawazipeleki familia zao katika makazi yao ya uteuzi.

Alichofanyiwa huyu mama sio utumishi wa kuheshimiana.
 
Tukumbuke haya maambukizi yataendelea kuja wimbi baada ya wimbi, yanakuja yanasambaa kwa kasi na kuathiri wengi baadae hali inatulia na kuanza tena kwa hiyo ni suala muda mrefu

Kwa hio mkuu hii Hali ya mawimbi yunaendayo mpaka wimbi la ngapi?
 
Tukumbuke haya maambukizi yataendelea kuja wimbi baada ya wimbi, yanakuja yanasambaa kwa kasi na kuathiri wengi baadae hali inatulia na kuanza tena kwa hiyo ni suala muda mrefu

Kwa hio mkuu hii Hali ya mawimbi yunaendayo mpaka wimbi la ngapi?
Siwezi kujua mpaka la ngapi Mkuu
 
Huyo mama amekufa kwa mengi...corona yaweza kuwa ni njia tu.

Ila mtambue hizi kazi hasa za uteuzi kuwa mguu sawa tu. Ndiyo maana viongozi wengine huwa hawazipeleki familia zao katika makazi yao ya uteuzi.

Alichofanyiwa huyu mama sio utumishi wa kuheshimiana.
Mama aliomba kupumzika, muda tu kwa ajili ya kutunza afya yake. Hatujui alikuwa na shida gani maana ni mambo binafsi ika huenda changamoto za afya yake zimechangia kuwa 'vulnarable' kwa shida za kupumua
 
Kuhusu afya nasikia huyu mama alikuwa mbishi sana, angeweza kulazimisha kipi atibiwe na kipi asitibiwe mbele ya Daktari, nasikia toka kitambo amekuwa na ugomvi binafsi na Hospitali fulani kubwa huko huko Kaskazini japokuwa kila akizidiwa alikuwa akilazwa kwenye hospitali hiyo hiyo na kutibiwa fresh. Safari hii alipoumwa hakwenda kutibiwa pale (huenda ilitokea tu kwa bahati au alikwepa kimakusudi).

Huenda wenye hiyo Hospitali wanasikitika kwa kuwa amefariki lakini kichini kichini wanashukuru kuwa mauti haukumkuta akiwa Hospitalini kwao, maana yangezushwa maneno.
 
Kuhusu afya nasikia huyu mama alikuwa mbishi sana, angeweza kulazimisha kipi atibiwe na kipi asitibiwe mbele ya Daktari, nasikia toka kitambo amekuwa na ugomvi binafsi na Hospitali fulani kubwa huko huko Kaskazini japokuwa kila akizidiwa alikuwa akilazwa kwenye hospitali hiyo hiyo na kutibiwa fresh. Safari hii alipoumwa hakwenda kutibiwa pale (huenda ilitokea tu kwa bahati au alikwepa kimakusudi).

Huenda wenye hiyo Hospitali wanasikitika kwa kuwa amefariki lakini kichini kichini wanashukuru kuwa mauti haukumkuta akiwa Hospitalini kwao, maana yangezushwa maneno.
Bora angeenda kcmc angeweza kupona sio mount meru huduma zake huwa ni duni sana hospital inayotegemewa kaskazini ni hyo kcmc, pia inabidi kuacha ubishi na kusikiliza wataalamu wa afya kwa tahadhari zaidi
 
Mkuu inavyoonekana korona haitoi kinga ya kutosha, tulitarajia mtu akishaugua akapona abaki na kinga kwa muda mrefu walau mwaka mmoja kama ilivyo kwa mafua ya kawaida. Wengi ni mashahidi kuna watu wanaweza kukwambia hawajaugua mafua zaidi ya miaka mitano, yote hiyo ni kinga ya muda mrefu ambayo mwili unatengeneza dhidi ya mafua. Sasa kama mtu aliyepona korona hawezi kuwa na kinga angalau ya mwaka mmoja maana yake ni kwamba chanjo ya korona haiwezi kuwa na msaada wowote zaidi ya kujidunga sumu mwilini...........nafikiri tumeelewana.
 
Back
Top Bottom