Kwa siku za karibuni Serikali ilitangaza kushuka kwa bei ya nishati ya mafuta. Jambo hili lilifurahisha sana watumiaji wa nishati ya mafuta lakini liliwakasirisha sana wenye vituo vya mafuta.
Kwa sasajinsi inavyoonekana, wenye vituo vya mafuta kama vile wana mgomo baridi. Vituo vingi ukitaka kununua mafuta unaambiwa kuwa mafuta yamekwisha lakini wakati mafuta yakiuzwa kwa bei ya zamani yalikuwa hayakosekani kwenye vituo. Wengine wanasema kuwa wanayaficha wakitarajia Serikali itapandisha bei ya nishati kuanzia tarehe 1 Julai, 2020.
Kipaumbele cha mfanyabiashara ni kupata faida kubwa, hivyo tunaiomba Serikali itupie macho juu ya tatizo hili la ukosefu wa nishati ya mafuta.
Kwa sasajinsi inavyoonekana, wenye vituo vya mafuta kama vile wana mgomo baridi. Vituo vingi ukitaka kununua mafuta unaambiwa kuwa mafuta yamekwisha lakini wakati mafuta yakiuzwa kwa bei ya zamani yalikuwa hayakosekani kwenye vituo. Wengine wanasema kuwa wanayaficha wakitarajia Serikali itapandisha bei ya nishati kuanzia tarehe 1 Julai, 2020.
Kipaumbele cha mfanyabiashara ni kupata faida kubwa, hivyo tunaiomba Serikali itupie macho juu ya tatizo hili la ukosefu wa nishati ya mafuta.