Tunaitaka TAKUKURU kufanya uchunguzi, kwanini watia nia Ubunge tunatozwa laki nne hadi sita?

Tunaitaka TAKUKURU kufanya uchunguzi, kwanini watia nia Ubunge tunatozwa laki nne hadi sita?

Mtarban

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2015
Posts
3,858
Reaction score
5,101
Habari wana jukwaa,

Awali ya yote niombe kueleza kuwa huwa napenda kukosolewa kwa Hoja pale mtu atakaposema kuwa nimeongea sivyo au nimedanganya. Ninafahamu kuwa humu wamo ambao wameweka nia kwa ngazi ya ubunge na hivyo baadhi tayari wanafahamu kinachoendelea kuhusu nilichokiandika hapa chini.

Mimi ni miongoni mwa watu ambao wanatarajia kuingia katika kinyanganyiro cha ubunge kupitia Chama cha Mapinduzi katika uchaguzi ujao.

Tukiwa kabisa bado tuko katika hatua za awali za maandalizi ya uchukuaji wa fomu, yapo maelekezo ambayo yametolewa na uongozi ambayo yatapaswa kutekelezwa na wale wote waliotia nia au watakaoingia katika kinyanganyiro ndani ya chama.

Mojawapo ya maelekezo haya ni kwamba kila mwanachama atakeyechukua fomu ya kugombea ubunge, mbali na kulipia laki moja, pia atapaswa kulipia kiwango cha ziada kunzia laki tatu na kuendelea (pesa hii inatofautiana kulingana na eneo au Jimbo).

Tumejaribu kuhoji kwa Nini tulipie pesa ambayo haipo katika kanuni za chama, majibu tuliyoambiwa ni kwamba pesa hii haiwezi kuwekwa hadharani kwa mstakabari wa chama, na kwamba pesa Hizi zitatumika moja kwa moja katika kuendeshea mikutano ya wajumbe.

Sina nia mbaya na chama changu, lakini ni vyema kukawa na uwazi katika hili, kwani chama chetu ni chama ambacho kimejipambanua katika kupambana na ufisadi na rushwa, na hivi karibuni mambo Kama haya tumeyashuhudia katika vyama pinzani, na iweje leo yatokee katika chama chetu?

Ni Imani yangu kuwa TAKUKURU watafanyia kazi suala hili na watakuja na majibu sahihi.

Wasalaam.
 
Kwahiyo unataka upewe bure fomu na wajumbe wajisafirishe au wakuombe rushwa.
 
Habari Wana jukwaa!
Awali ya yote niombe kueleza kuwa huwa napenda kukosolewa kwa Hoja pale mtu atakaposema kuwa nimeongea sivyo au nimedanganya. Ninafahamu kuwa humu wamo ambao wameweka Nia kwa ngazi ya ubunge na hivyo baadhi tayari wanafahamu kinachoendelea kuhusu nilichokiandika hapa chini.

Mimi Ni miongoni mwa watu ambao wanatarajia kuingia katika kinyanganyiro Cha ubunge kupitia chama Cha mapinduzi katika uchaguzi ujao...
CCM sio chama cha MAKABWELA, iko hivyo tangu muda mrefu.
 
Haa kama laki 3 ya mara moja tu inakushinda sasa hv, hufai kuwa mbunge, sbb ukiwa mbunge ukipata hela ndio utakuwa unashughulikia biashara zako tu na kuwatia umaskini wananchi.
 
Hujamuelewa mleta mada. Anataka na hizo laki tatu za ziada ziwe rasmi kama ilivyo hiyo laki moja ya fomu.
Mikoa na wilaya inatofautiana kimapato na kigharama umbali nk Kuna wilaya Kama handeni wajumbe hutoka umbali mno Huwezi linganisha na wilaya Kama za dar es salaam
 
Haa kama laki 3 ya mara moja tu inakushinda sasa hv, hufai kuwa mbunge, sbb ukiwa mbunge ukipata hela ndio utakuwa unashughulikia biashara zako tu na kuwatia umaskini wananchi.
Kwahiyo unataka pesa ya kula na familia yake ajenge madaraja na kuchonga barabara za wananchi?
 
Habari wana jukwaa,

Awali ya yote niombe kueleza kuwa huwa napenda kukosolewa kwa Hoja pale mtu atakaposema kuwa nimeongea sivyo au nimedanganya. Ninafahamu kuwa humu wamo ambao wameweka nia kwa ngazi ya ubunge na hivyo baadhi tayari wanafahamu kinachoendelea kuhusu nilichokiandika hapa chini...
Hiki ni chama cha matajiri(CCM) mkuu jaribu bahati yako kupitia TLP
 
Haa kama laki 3 ya mara moja tu inakushinda sasa hv, hufai kuwa mbunge, sbb ukiwa mbunge ukipata hela ndio utakuwa unashughulikia biashara zako tu na kuwatia umaskini wananchi.

Hakuna sehemu nimesema kuwa imenishinda Bali nataka sheria zifatwe. Hakuna kanuni inayomtaka mtia Nia atoe laki tatu nje ya laki moja ya kuchukua fomu. Hapa Kuna upigaji
 
Kwahiyo unataka upewe bure fomu na wajumbe wajisafirishe au wakuombe rushwa.
Kama chama kinataka Waliotia Nia ndo Wawasafirishe wajumbe Basi Basi katiba ya chama ingetamka wazi, otherwise Ni upigaji Kama ilivyo kwa michango ya vyama vingine
 
Back
Top Bottom