Tunaitaka TAKUKURU kufanya uchunguzi, kwanini watia nia Ubunge tunatozwa laki nne hadi sita?

Tunaitaka TAKUKURU kufanya uchunguzi, kwanini watia nia Ubunge tunatozwa laki nne hadi sita?

Zile zilikuwa zama za upigaji. Awamu hii hatuwezi kuruhusu upigaji wa namna hii
Unaishi nchi gani wewe? Kumbe ndio sababu unatapatapa hapa kulipishwa laki sita ya kugombea Ubunge kupitia CCM? Hivi kuna awamu ambayo imewahi kufanya matumizi ya kufuru na STAREHE ya zaidi ya Trilioni 2.5 kwa kipindi kisichozidi miaka minne tu, kuliko hii?

Ukiendelea na hayo mawazo yako mgando ya kutaka KUSIFIA na KUTUKUZA tu, Ubunge utausikia redioni tu. Mark my words poor young man.
 
tatizo lako unafikiri ccm ni chama cha wakulima na wafanyakazi! hiii ilikuwa enzi za mwalimu. kalaghabao!
 
Watu wanajua kupiga hela kwa hiyo Kama watia Nia wako 10 means 3M kwenye Jimbo moja
Na Kama mkoa una majimbo Saba ko inakua watia Nia 70 ambao watachangia kiasi kisichopungua 21M
Hujaweka idadi ya mikoa yote Tanzania nzima
Aseeee CCM wako na hela Sana
 
Hakuna sehemu nimesema kuwa imenishinda Bali nataka sheria zifatwe. Hakuna kanuni inayomtaka mtia Nia atoe laki tatu nje ya laki moja ya kuchukua fomu. Hapa Kuna upigaji

Hakikisha hiyo pesa ya ziada inakuwa na maelezo Ina lipwa kwa kazi gani na hakikisha wanakupa na risiti ya malipo... Bila hivyo huo utakuwa Ni utakatishaji wa pesa.
 
Mtoa mada anabezwa lakini taarifa anayotoa ni nyeti na wahusika inabidi wafuatilie. Mtoa mada unaweza kuongeza nyama kwa kuongeza taarifa za ziada za Wilaya na Jimbo ili wahusika wakusaidie.
 
Mleta mada Ni Chadema CCM asingeandika hivyo hajataja hata ni wapi hizo ndizo tabia za chadema
 
Kwahiyo unataka upewe bure fomu na wajumbe wajisafirishe au wakuombe rushwa.

Mnaleta siasa za kupuuzi, wanachama wenu wanaamini kuwa nyie ni watu safi kumbe majizi matupu. Toeni maelezo hiyo hela inayozidi laki ni ya nini. Maana Takukuru mmewatuma kufanya siasa chafu kwa cdm, kuwa kuna hela wabunge walichanga hivyo zitolewe maelezo. Kama mmeweza kuwatuma Takukuru kwa cdm, onyesheni mfano nyinyi wa kutoa maelezo wa pesa za ziada ni za nini fullstop.
 
Haa kama laki 3 ya mara moja tu inakushinda sasa hv, hufai kuwa mbunge, sbb ukiwa mbunge ukipata hela ndio utakuwa unashughulikia biashara zako tu na kuwatia umaskini wananchi.

Acha maelezo ya kijinga, anataka kujua laki 3+ ni ya nini, maana laki 1 ni ya fomu. Hajasema hawezi kulipa laki 3, ila iwekwe wazi ni ya nini, kama ile inayowafanya wahuni wa Takukuru wakashinde kwenye ofisi za cdm. Mnapoanza kucheza siasa chafu, lazima mjue hazina mwisho mwema.
 
Mnaleta siasa za kupuuzi, wanachama wenu wanaamini kuwa nyie ni watu safi kumbe majizi matupu. Toeni maelezo hiyo hela inayozidi laki ni ya nini.
chadema mwenzio huyo mzushi kama nyie wenyewe huoni hata hajaandika ni wapi hataji hata eneo huyo ni chadema mwenzenu kama nyie mliosema mliibiwa kura za uraisi uchaguzi mkuu mkiambiwa tajeni hata kituo kimoja cha kura mlichoibiwa hamtaji
 
TAKUKURU Ni chombo huru ambacho kinaweza kumhoji mtu yeyote yule

Hapa ndio itakuwa wazi zaidi kuwa takukuru imegeuka kuwa taasisi ya kutumikia siasa chafu.
 
chadema mwenzio huyo mzushi kama nyie wenyewe huoni hata hajaandika ni wapi hataji hata eneo huyo ni chadema mwenzenu kama nyie mliosema mliibiwa kura za uraisi uchaguzi mkuu mkiambiwa tajeni hata kituo kimoja cha kura mlichoibiwa hamtaji

Unapopanic zingatia matumizi ya koma na nukta. Lijualikali alisema cdm waliiba kura, alitaja ni vituo vingapi na idadi ya kura zilizoibwa? Unataka huyu mjumbe ataje ni wapi ili mumfuatilie na lile kundi lenu la watu wasiojulikana?

Hizo kura za urais hata tofauti ya baadhi ya vituo iliwekwa, na tofauti ya jumla kuu pia iliwekwa, na nyuzi zaidi ya moja ziko humu jukwaani. Hata hivyo ukifahamu wizi wa kura, kuna mahakama ya kupeleka madai ya kura za urais?
 
Mleta mada Ni Chadema CCM asingeandika hivyo hajataja hata ni wapi hizo ndizo tabia za chadema
Jikite kwenye mada. Harafu kuwa CCM hakunizuii kukosoa ujinga unafanyika ndani ya chama.
 
Back
Top Bottom