Tunajifunza nini kuhusu kutimuliwa kwa Jeanine Mabunda kama Spika wa Bunge la Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo?

Tunajifunza nini kuhusu kutimuliwa kwa Jeanine Mabunda kama Spika wa Bunge la Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo?

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Hapo jana ya tarehe 11/12/2020 tulipata taarifa kuwa Bunge la Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo limepiga kura ya kutokuwa na imani naye Spika wao wa Bunge, Jeanine Mabunda kwa namna anavyoliendesha Bunge hilo kwa upendeleo na kujiegemeza kwa Rais Mstaafu, Joseph Kabila, pamoja na chama chake.

Nchi yetu Tanzania tunajifunza nini kuhusu kutimuliwa kwa Spika huyo wa Bunge la Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo?

Ni dhahiri kuwa yapo mengi tunayoweza kujifunza kwa Bunge hilo jinsi lilivyosimamia kanuni zake na kumwona Spika huyo wa Bunge kuwa hafai na hivyo kumpigia kura za kukosa imani naye.

Hapa nchini kwetu tunaye Spika ambaye ameamua kuikanyaga kanyaga Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977
kwa kuwakumbatia wale wabunge wa viti maalum wa Chadema.

Ni sharti la kikatiba kuwa mbunge yeyote anapovuliwa uanachama wake na chama chake, basi hatua inayofuata ni kwa Spika kuiandikia barua Tume ya uchaguzi kuieleza kuwa nafasi hizo za ubunge ziko wazi, kwa hiyo ufanyike mchakato mwingine wa kuziziba nafasi hizo.

Tumepata taarifa toka kwa kiongozi wa Chadema, John Mrema, zilizothibitisha kuwa chama hicho kilishapeleka barua kwa Spika wa Bunge, Job Ndugai, tarehe 29/11/2020 kuhusu maamuzi ya Kamati Kuu ya Chadema, kuwavua uanachama wabunge hao akina Halima Mdee.

Swali tunalopaswa kumuuliza Spika Ndugai ni kwanini anashikwa na "kigugumizi" na hataki kutekeleza sharti hilo la kikatiba kwa kumwandikia barua Mkurugenzi wa Tume, kumjulisha kuhusu kupokea kwake barua hiyo ya Chadema?

Hivi kuna tofauti gani katika uendeshaji wa Bunge kati ya Spika Ndugai na mwenzake Jeanine Mabunda wa Congo aliyetimuliwa kazi kuhusu upendrleo wake kwa Rais mstaafu Joseph Kabila na Chama chake?

Hivi Spika Ndugai ambaye anaonyesha upendeleo wa wazi kabisa kwa Rais Magufuli na chama chake cha CCM, na kuikanyaga kanyaga Katiba ya nchi yetu ni kwanini basi Bunge la nchi yetu lisipange kupiga kura ya kumng'oa kwenye nafasi hiyo ya U-Spika?
 
Tofauti ni kwamba, rais wa jamhuri ya muungano ni JPM, ambaye ni rais jiwe kweli kweli. Ndugai anafuata katiba au matakwa ya JPM?
 
Yaani CHADEMA ni wajinga no offense, unategemea Ndugai aende dhidi ya matakwa ya CCM na Mwenyekiti wake, hivi unajua hata huyo Spika wa Congo ametimuliwa sababu ya kuwa upande tofauti na Rais wa nchi yake, mna ndoto za kitoto kama vile mpo katika fantasy world.
Tinachosema ni kuwa Spika Ndugai aliapa kuitii na kuiheshimu Katiba ya nchi, kabla hajaanza kutumikia madaraka hayo, ni kwanini basi anaikanyaga kanyaga Katiba hiyo kwa kutotaka kuitii Katiba hiyo inayomwambia kuwa mbunge yeyote anapovuliwa uanachama wake na chama kilichomdhamini ubunge wake, automatically anakuwa amevuliwa ubunge wake?
 
Tofauti ni kwamba, rais wa jamhuri ya muungano ni JPM, ambaye ni rais jiwe kweli kweli. Ndugai anafuata katiba au matakwa ya JPM?
Hivi Spika wa Bunge aliapa kumtii Rais Magufuli au aliapa kuitii na kuiheshimu Katiba ya nchi?

Jibu utakalopata ndiyo argument yangu kuwa ni kwanini Spika Ndugai hatufai kwenye nafasi hiyo ya U-Spika na hivyo anapaswa ang'olewe
 
Hapo jana ya tarehe 11/12/2020 tulipata taarifa kuwa Bunge la Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo limepiga kura ya kutokuwa na imani naye Spika wao wa Bunge, Jeanine Mabunda kwa namna anavyoliendesha Bunge hilo kwa upendeleo na kujiegemeza kwa Rais Mstaafu, Joseph Kabila, pamoja na chama chake....
Ukiondoa Terms limits ambayo nayo iko shakani, Uganda, DRC na Burundi wanatuzidu mbali tu kidemokrasia.

Tena watapiga hatua kubwa sana huku wakituacha sisi na na demokrasia yetu ya Genge dogo la watu kubadilishana madaraka.
 
Hivi Spika wa Bunge aliapa kumtii Rais Magufuli au aliapa kuitii na kuiheshimu Katiba ya nchi?

Jibu utakalopata ndiyo argument yangu kuwa ni kwanini Spika Ndugai hatufai kwenye nafasi hiyo ya U-Spika na hivyo anapaswa ang'olewe
Unakosea kutokujua kuwa ni "system" nzima imeamua kwenenda kwa matakwa binafsi na sio lazima kufuata sheria au katiba endapo maslahi ya system yatafifia. Kiburi kikizidi hata Sheikh anaweza ingia msikitini na rainyboot!!
 
Hata Spika mstaafu Pius Msekwa, ambaye ni mwanachama mwenzie wa CCM, alishalitolea ufafanuzi suala hili.

Bila unafiki wala kupepesa macho alisema, ubunge wa kina Halima Mdee ulikoma Mara tu baada ya maamuzi yale ya Kamati Kuu ya Chadema, na maamuzi hayo kuyaweka hadharani.

Ninachomuuliza Spika Ndugai ni kwanini basi anawang'ang'ania kina Halima Mdee?
 
Yaani CDM ni wajinga no offense, unategemea Ndugai aende dhidi ya matakwa ya CCM na Mwenyekiti wake, hivi unajua hata huyo Spika wa Congo ametimuliwa sababu ya kuwa upande tofauti na Rais wa nchi yake, mna ndoto za kitoto kama vile mpo katika fantasy world.
acha matusi . ongea facts.

kwenye bunge la Congo DRC kuna wabunge wangapi cha chama cha rais alieko madarakani na wangapi wa chama cha Joseph Kabila?

tuanzie hapo kwanza ili tuone kama ulichosema kina mashiko? kwamba wabunge wa bunge la Congo wana ushabiki wa kisiasa?
 
Hapo jana ya tarehe 11/12/2020 tulipata taarifa kuwa Bunge la Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo limepiga kura ya kutokuwa na imani naye Spika wao wa Bunge, Jeanine Mabunda kwa namna anavyoliendesha Bunge hilo kwa upendeleo na kujiegemeza kwa Rais Mstaafu, Joseph Kabila, pamoja na chama chake....
Ni suala la muda tu. Huyu mgogo lazima ang'oke. Hakuna Katiba ya Kongwa hapa.
 
Hapo jana ya tarehe 11/12/2020 tulipata taarifa kuwa Bunge la Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo limepiga kura ya kutokuwa na imani naye Spika wao wa Bunge, Jeanine Mabunda kwa namna anavyoliendesha Bunge hilo kwa upendeleo na kujiegemeza kwa Rais Mstaafu, Joseph Kabila, pamoja na chama chake...
Keep cool time will tell them
 
Hapo jana ya tarehe 11/12/2020 tulipata taarifa kuwa Bunge la Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo limepiga kura ya kutokuwa na imani naye Spika wao wa Bunge, Jeanine Mabunda kwa namna anavyoliendesha Bunge hilo kwa upendeleo na kujiegemeza kwa Rais Mstaafu, Joseph Kabila, pamoja na chama chake....
Job Ndugai ana bahati bunge limekuwa rasmi tawi la chama
 
Hawana lingine zaidi ya kutengeneza kijimgogoro ndani ya CDM ili kuwatoa kwenye kuyasema yakwenye uchaguzi kwamba haukua uchaguzi Bali uchafuzi kingine hawa mazuzu wanajua sana kuihadaha jamii yetu ikisha hadaika tayari jambo linapata mashabiki inakua imetiki wanaendelea kutafuna Mali zetu huku tukidanganywa na vijimiladi vya mikopo ya hao tunaoaminishwa kwamba ni mabeberu .
 
Hawana lingine zaidi ya kutengeneza kijimgogoro ndani ya CDM ili kuwatoa kwenye kuyasema yakwenye uchaguzi kwamba haukua uchaguzi Bali uchafuzi kingine hawa mazuzu wanajua sana kuihadaha jamii yetu ikisha hadaika tayari jambo linapata mashabiki inakua imetiki wanaendelea kutafuna Mali zetu huku tukidanganywa na vijimiladi vya mikopo ya hao tunaoaminishwa kwamba ni mabeberu .
Kwanza hata sielewi mchango wa Mwanasheria Mkuu wa serikali, Dkt Adeladus Kilangi, hapo Bungeni ni UPI?

Kwa kuwa ninavyojua Mimi ni kuwa Mwanasheria- Mkuu wa serikali jukumu lake kubwa hapo Bungeni ni kutoa ufafanuzi katika masuala ya kisheria kwa Spika na Bunge lake kwa ujumla wake.

Sasa inashangaza kuona Mwanasheria- Mkuu wa Serikali akimtazama na kushikwa na "kigugumizi" bila kumwambia Spika Ndugai kuwa anakosea kwa kuwakumbatia wabunge wa viti maalum, ambao chama chao cha Chadema kimeshatangaza rasmi kuwavua uanachama wao
 
Kwanza hata sielewi mchango wa Mwanasheria Mkuu wa serikali, Dkt Adeladus Kilangi, hapo Bungeni ni UPI?

Kwa kuwa ninavyojua Mimi ni kuwa Mwanasheria- Mkuu wa serikali jukumu lake kubwa hapo Bungeni ni kutoa ufafanuzi katika masuala ya kisheria kwa Spika na Bunge lake kwa ujumla wake.

Sasa inashangaza kuona Mwanasheria- Mkuu wa Serikali akimtazama na kushikwa na "kigugumizi" bila kumwambia Spika Ndugai kuwa anakosea kwa kuwakumbatia wabunge wa viti maalum, ambao chama chao cha Chadema kimeshatangaza rasmi kuwavua uanachama wao
Ieleweke kwamba kilangi ni ndugu yetu yupo pale so kwa kua ni mwanasheria hapana yupo hapo kwakua ni msukuma pia kasoma na Mobutu wa nzega sory buseresere.
 
acha matusi . ongea facts.

kwenye bunge la Congo DRC kuna wabunge wangapi cha chama cha rais alieko madarakani na wangapi wa chama cha Joseph Kabila?

tuanzie hapo kwanza ili tuone kama ulichosema kina mashiko? kwamba wabunge wa bunge la Congo wana ushabiki wa kisiasa?
Ila anachoongea huyu jamaa kina ukweli fulani,wapenda mabadiriko nchini hasa vyama vya siasa wasitegemee chochote kupitia mfumo huu wa utawala au bunge hili.

Ukimwangalia ndugai usoni amekaa kinafiki nafiki sawa na maneno yake

Yaani ukiambiwa ni msomi unaeza usikubali.
Kati ya viongozi utopolo tulionao nchi hii ndugai no,1. Yaani hata jiwe ana nafuu.

Huyu spika sijui familia yake ina hali gani kitabia!!.
Mke sijui anaishi nyumbani kwake au kwa wengine

TUNA SPIKA AU TUNA MAITI?
 
Hapo jana ya tarehe 11/12/2020 tulipata taarifa kuwa Bunge la Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo limepiga kura ya kutokuwa na imani naye Spika wao wa Bunge, Jeanine Mabunda kwa namna anavyoliendesha Bunge hilo kwa upendeleo na kujiegemeza kwa Rais Mstaafu, Joseph Kabila, pamoja na chama chake....
Sawa, Endelea itawezekana tu Mkiweza kuruhusu Mwenyekiti wa Chama chenu aache kuibadilisha katiba ili awe Mwenyekiti wa kudumu. Nyani kweli haoni kundule
 
Congo hakuna nchi pale, kila mbunge kala kitita, Jose Kabila hana ubavu wa huo mkwanja. Bongo ni ngumu kuwanunua wabunge kwa sababu ya uzalendo na mifumo yetu imara
 
Back
Top Bottom