Tunakoelekea kuoga na Sabuni Pia tutaambiwa ni dhambi

Tunakoelekea kuoga na Sabuni Pia tutaambiwa ni dhambi

Kristo gani unayemsubiri kuwa atakuja?

Kristo baada ya kupaa mbinguni alisema ataleta msaidizi atakayeweka wazi na kufundisha mambo yote.

Cha msingi ni kuwa huyo roho wa Mungu ndiye Kristo mwenyewe aliye ahidi atakaa ndani yetu.

Sasa sijui unamsubiri Kristo gani, wakati yeye amesema yumo ndani yako?
Mungu baba,Mwana,Roho mtakatifu
 
nzengeli ni msabato, kwa habari ya wakatoliki, ni kweli hawaokoki, maria haokoi.
Yesu Anakuja na Wengine: Maria haokoi...

Wakatoliki:...
Nasadiki kwa Bwana mmoja Yesu Kristo, mwana wa pekee wa Mungu.
Aliyezaliwa kwa Baba tangu milele yote.
Mungu aliyetoka kwa Mungu,mwanga kwa mwanga,Mungu kweli kwa Mungu kweli.
Aliyezaliwa bila kuumbwa, mwenye umungu mmoja na Baba,
ambaye vitu vyote vimeumbwa naye.
Ameshuka toka mbinguni kwa ajili yetu sisi wanadamu na kwa ajili ya wokovu wetu.
 
Kristo gani unayemsubiri kuwa atakuja?

Kristo baada ya kupaa mbinguni alisema ataleta msaidizi atakayeweka wazi na kufundisha mambo yote.

Cha msingi ni kuwa huyo roho wa Mungu ndiye Kristo mwenyewe aliye ahidi atakaa ndani yetu.

Sasa sijui unamsubiri Kristo gani, wakati yeye amesema yumo ndani yako?
Soma pia Yohana 14:26
 
Kama kuna Roho mtakatifu/Kristo mwingine unamsubiri unamaanisha lipi? Je hakuna Kristo ndani yako leo?

Huyo unayemsubiri akija, yuke uliyenaye siku zote ataenda wapi, ama aliyepo ni feki.
Roho mtakatifu ndiye kiongozi kwa Sasa,huyo Roho mtakatifu huyaabadilisha maisha,ndiyo maana unakuta dhamiri ya usitende baya linakujia ni kazi ya Roho mkuu!
 
Baada ya Mchungaji Mch. Abiud Misholi Kutamka adharani kwamba ni Ushetani mkubwa Mlokole kushabikia mpira Mwimbaji wa nyimbo za injili na SHABIKI mkubwa wa Yanga African @Ann_annie kafunguka ya moyoni na kusema....

"Kuna Max Nzengeli na Kennedy Musonda wameokoka sasa na wanacheza mpira itakuwaje??

Mabasi yenyewe tunayopanda ni ya washirikina biashara nyingi tunakoenda kununua vitu wawekezaji ni hao hao washirikina, sadaka tunazotuma kwa wachungaji tumezipata kwa hao hao washirikina na cha ajabu wachungaji hawazikatai hizo sadaka ... Niseme tu ni Yesu tu anayetulinda".

Hivi ndivyo alivyofunguka mwimbaji wa gospel, nimemuelewa vizuri kabisa, ila mchungaji Misholi sijamuelewa kabisa.

Bila shaka tunakoelekea, hata kuoga na sabuni ya GSM tutakuja kuambiwa ni dhambi 🤔
kwa maoni yangu na matazamo wangu juu ya hili, kwanza lazima tukubaliane kuwa mpira wenyewe na asili yake haumpi Mungu utukufu, na maandiko yanasema fanyeni kila jambo kwa utukufu wa Mungu. Sasa kwenye huo mpira kuna ushirikina mkubwa wanaajiliwa waganga na mambo mengi ya kishirikina yanafanyika hayo hayampi Mungu utukufu

Pili mpira umejaa mambo ya kufuru, ufusika, pombe, lugha za matusi utazikuta uwanjani hayo hayampi Mungu utukufu

Sasa kama Mwana wa Mungu anapaswa kufanya mambo yanayompa Mungu utukufu akifanya hilo ambalo unaona kabisa kuna wengine walimiminiana risasi huko Russia, watu wana apa mpaka kuwatoa sadaka wake zao(kubet) sio sahihi.

Ukisimamia hoja ya wachungaji kupokea sadaka, wao wachungaji wanapokea tu lakini huwatolei wachungaji, ndio maana utatoa sadaka kwa wachungaji lakini utamuomba Mungu akubariki, maana yake hata sadaka zinamhusisha Mungu
 
Baada ya Mchungaji Mch. Abiud Misholi Kutamka adharani kwamba ni Ushetani mkubwa Mlokole kushabikia mpira Mwimbaji wa nyimbo za injili na SHABIKI mkubwa wa Yanga African @Ann_annie kafunguka ya moyoni na kusema....

"Kuna Max Nzengeli na Kennedy Musonda wameokoka sasa na wanacheza mpira itakuwaje??

Mabasi yenyewe tunayopanda ni ya washirikina biashara nyingi tunakoenda kununua vitu wawekezaji ni hao hao washirikina, sadaka tunazotuma kwa wachungaji tumezipata kwa hao hao washirikina na cha ajabu wachungaji hawazikatai hizo sadaka ... Niseme tu ni Yesu tu anayetulinda".

Hivi ndivyo alivyofunguka mwimbaji wa gospel, nimemuelewa vizuri kabisa, ila mchungaji Misholi sijamuelewa kabisa.

Bila shaka tunakoelekea, hata kuoga na sabuni ya GSM tutakuja kuambiwa ni dhambi 🤔
Ukiwa mabanda ya mipira ndio utajua ushabiki wa mpira ni mpango wa shetani mabanda ya mipira yametawaliwa na lugha zilizokosa staha kitu kingine ushabiki wa mipira umeliingiza kundi kubwa la watu kuingia kwenye michezo ya kamari ushabiki wa mipira ni mpango wa shetani kuwa mshabiki wa timu Fulani unakuwa umeniunga katika ibada zao huko wanakotoaga makafara kabla ya msimu haujaanza
 
Mpira ni ibada na vilabu Ni madhehebu ambapo mtu akipenda kilabu Hicho hawezi hama.
Mfano umeamua kuwa Shetani Mwekundu bhasi milele wewe ni Shetani😁
Ahaa basi ngoja jioni nikaangalie YANGA kwa umakini,..nikimuona SHETANI naacha
kuiangalia🤣🤣
 
Hawa walokole au wanaojiita walokole wamepungukiwa akili, huwezi ukaokoka kabla haujafa.

Unakufa kwanza, unahukumiwa kwa kadiri ya matendo yako, ukipenya kwenda mbinguni hapo sasa ndiyo unakua umeokoka.

Naomba muwaambie wafanye matumizi mazuri ya hizo akili finyu, kama bado zipo

Hapa umedanganya.
 
Kama yupo sahihi kwa nini hajawahi kukataa sadaka iliyotumwa kupitia ule mtandao wa washenzi Tigopesa or M-Pesa?

Wachungaji wapo speed kusambaza in public namba za kutuma sadaka ilhali watumaji ni hao hao mashrtani, upo wapi usahihi wa mchungaji?
Sijui unabisha nini na hoja yako ni ipi? Maana naona unatoka kwenye mpira na sasa unaenda kwenye sadaka via Mpesa na Tigo pesa.
 
Mpira ni ibada na vilabu Ni madhehebu ambapo mtu akipenda kilabu Hicho hawezi hama.
Mfano umeamua kuwa Shetani Mwekundu bhasi milele wewe ni Shetani😁
Ni sahihi. Nakumbuka wakati nikiwa shabiki damudamu wa Chelsea na maono niliyoyaona ya lile Simba lililoshika mkuki kwenye logo ya Chelsea kama linatema moto hivi na uhalisia wake katika ulimwengu wa Roho.

Kwa jinsi ya kibinadamu ni ngumu kukubali ila ni kweli mpira ni chukizo. Hivi ushawahinjiuliza manembo na a.k.a ya majina yanamaanisha nini?

Timu inajiita red devil, dragon, blue satan n.k
 
Kristo gani unayemsubiri kuwa atakuja?

Kristo baada ya kupaa mbinguni alisema ataleta msaidizi atakayeweka wazi na kufundisha mambo yote.

Cha msingi ni kuwa huyo roho wa Mungu ndiye Kristo mwenyewe aliye ahidi atakaa ndani yetu.

Sasa sijui unamsubiri Kristo gani, wakati yeye amesema yumo ndani yako?
Kristo atakuja mara ya pili kulichukua kanisa
 
Kama kuna Roho mtakatifu/Kristo mwingine unamsubiri unamaanisha lipi? Je hakuna Kristo ndani yako leo?

Huyo unayemsubiri akija, yuke uliyenaye siku zote ataenda wapi, ama aliyepo ni feki.
Ataondoka na huo ndio unyakuo wa kwanza, wawili watakuwa wamelala mmoja atwaliwa mmoja aachwa, wawili watakuwa shambani, mmoja atwaliwa mmoja aachwa
 
Mpira ni ushetani,

Man UTD Inaitwa timu ya Mashetani wekundu na nembo na picha za mashetani wameweka kabisa.

Chelsea ni timu ya Mashetani wa Bluu, na nembo na picha za mashetani wa Bluu zipo,

Sasa imeandikwa meditate the world of God day and night,

Sasa mlokole ulevi wake ameruhusiwa kulewa Kwa Roho MTAKATIFU, huo ulevi wa pombe au mpira wa nini?

Utakatifu ni kujiweka wakfu, kuwa special Kwa ajili ya kumtumikia Mungu.
 
Back
Top Bottom