Tunakoelekea kuoga na Sabuni Pia tutaambiwa ni dhambi

pombe ni haramu,hata kwa maarifa /elimu ya dunia..(watu wangu wana angamia kwa kukosa maarifa).
 

Attachments

  • images - 2024-10-04T154527.536.jpeg
    35.6 KB · Views: 2
Unajua Mungu ameweka pombe kwa ajili ya kuleta furaha baada ya kazi ngumu? Au hakuna andiko linalounga mkono pombe?
andiko ninalofahamu kuhusu kutumika pombe ilitumika kama dawa ya tumbo na kidonda.Kama mtu anatumia pombe kujitibu tumbo au vidonda ni sawa kama amefunuliwa kufanya hivyo au ni moja ya matibabu ya ugonjwa wake.LAKINI sifahamu andiko kwenye biblia linalohamasisha watu wanywe pombe au wawe walevi.sifahamu.
 
kuhusu FURAHA tunatakiwa tufurahi katika BWANA na yote tunayoyafanya tufanye kwa utukufu wa Mungu.
kuhusu matumizi ya pombe kuondoa STRESS au msongo wa mawazo ,SAYANSI YA AFYA inakataa pombe sio dawa ya kukuondolea msongo wa mawazo na kukuletea AMANI ya nafsi au FURAHA.sio kweli kwamba pombe inaondoa stress.
 
mkuu hapo unakuwa mwanafunzi wake, na ni kweli unakuwa upande wake. suala la kuokoka sasa ni mpaka uvumilie hadi mwisho ndo uokoke
tayari kuwa upande wake unakuwa umeokolewa kutoka kwenye milki ya mkuu wa giza, unakuwa huru kutoka kwenye vifungo vya ibilisi, sasa kinafuata baada ya hapo ni kuvumilia kukaa upande wake mpaka mwisho anapokuja, kwa sababu ibilisi hatakuwa tayari kupokonywa mateka wake
 
kwanza pombe inaharibu maini na mapafu, kuna lecture wangu alifariki kwasababu ya unywaji wa pombe kali, na wanywaji wanajua ila wanajitoa akili
 
kuoga oga kila mara kunapunguza kinga ya mwili - wataalam tiba.
 
sawa mkuu ,tuendelee kujifunza maandiko ili kujua nini kinatakiwa au tuseme utaraibu upoje
 
Unathibitisha ni namna gani bado mchanga kwenye bible.

Point yako ni mwili uvae kutokufa yaani Uzima....

Mwili unavaa kutokufa pale tu unapomwamini Kristo na kabla ya kumwamini Kristo wewe unakua ni mfu hata kama unapumua.

Biblia sehemu nyingi ikiwa inazungumzia kufa siyo kufa huku kwa kawaida kuacha kuvuta pumzi.

Kifo kinachozungumzwa ni Mauti inayosababishwa na Dhambi (unaweza kuwa unatembea barabarani lakini umekufa kwa sababu ya dhambi)

Uzima unaozugumziwa ni Uzima tunaopata baada ya kamini neema ya Kristo iondoayo au ishindayo dhambi na mauti.

Kwahiyo unapomwamini Kristo hapohapo unafufuka kutoka katika mauti ndani ya dhambi, na unaingia Uzimani ndani ya Kristo.

Yn 6:51 SUV
[51] Mimi ndimi chakula chenye uzima kilichoshuka kutoka mbinguni; mtu akila chakula hiki, ataishi milele. Na chakula nitakachotoa mimi ni mwili wangu, kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.


Hizo habari za siku ya Mwisho utapewa mabawa upae kwenda mbinguni utasubiri sana.
Mbinguni ipo ndani yako, ukiamini neema ya Kristo ufalme wa Mungu unahamia kwako yaani baba na mwana wote wanakaa ndani yako na wala huwezi kufa kamwe.
 
Dkt Janabi mtaalamu wa afya anasema;

Kula wali, Ugali na chapati kila siku ina madhara ndani ya mwili inapelekea kupata kisukari na Magonjwa ya figo.
Kuharibu afya ni pamoja na kupata kitambi cha Wali na (supu + chapati 2)

Kuvaa suruali ni kusahihisha uumbaji jinsi Mungu alivyokuumba.

Sijui akili mnaziachaga wapi mnapokuja kusema kuvaa hereni na kusuka ni dhambi wakati kuvaa nguo mnaita utakatifu.

Kubeti siyo Dhambi. Dhambi ni kutomwamini Kristo tu hakuna dhambi nyingine zaidi ya hiyo.
 
1.)anachosema/elimu anayofundisha Dr Janab ni sahihi kabisa na ni sayansi ukitaka ushahidi wa hilo upo na unaweza hata ku search/ku google madhara ya kula kuzidi kiasi mahitaji ya mwili.Kula kwa wingi vyakula vinywaji vya sukari(wanga),mafuta,chumvi,pombe ,sigara,energy drinks,juisi za matunda badala ya matunda yenyewe,fast food chips vyakula vya kukaanga na mafuta,kutokufanya mazoezi au kushughulisha mwili,vyakula vya viwandani kusindika,GMO genetic modified organisms mazao vyakula vya kisasa,mbegu za mazao au wanyama ndege kisasa,kuku ,mayai ya kisasa zilizochakachuliwa vinasaba GMF/GMO
pollutions mbalimbali na athari za utandawazi mapinduzibya viwanda na athari zake katika afya ,hiyo ni kweli ni fact ukitaka ushahidi google utaupata hiyo ni sayansi,nampongeza na kumshukuru dr janabi kwa kazi nzuri anayoifanya ya kutuelimisha elimu ya afya sisi wana jamii.
2)Kuvaa suruali katika context ya kiroho kiimani imani ya kikristo na msingi wa mafundisho ya imebainisha bayana MWANAMKE ASIVAE MAVAZI YAMPASAYO KUVAA MWANAUME kadhalika mwanaume asivae mavazi yampasayo kuvaa mwanamke.
Kijamii naaadili inategemea ila nimeshuhudia baadhibya maeneo wanawake waliovaa nguo za kubana au hasa suruali au wanaume waliovaa milegezo au mwanaume avae gauni la kike.Imeonekana kama ni ukosefu wa maadili,hata baadhibya sehemu kuzuiwa kupata huduma.Na pia watu wanaovaa mavazi yasiyokuwa na maadili au staha au heshima wanatafsiriwa kuwa ni watu wasio na maadili.
3)HERENI KUSUKA MAPAMBO biblia imekataza ipo mistari mingi tafuta utaona hata ukigoogle utaipata
na baadhi ya mapambo yamekuwa yana roho za uharibifu na mengine asili yake yametoka kwa falme za giza ma yamewaingiza watoto wa Mungu katika vifungo.Eneo hili ndio limekamata wengi hata baadhibya wake za watumishi wa Mungu ,wachungaji na halikemewi kabisa ,wahubiri hawakemei wakiogopa watapoteza waumini LAKINI UKWELI UNAPASWA KUSEMWA.Wachungaji wanaojua ukweli wa neno lakini hawa huburi kwa waimini wao kwa vile wanaogopa kuwaudhi wata daiwa roho za watoto wa Mungu zitakazopotea motoni kwa sababu ya mapambo hiyo hereni inaweza ikakuzuia kuongia mbinguni,mawigi na maurembo mengine.
4)Kuvaa nguo tunaita utakatifu (kwamba kuvaa nguo nin sahihi ama sio sahihi,hili halihitaji ufafanuzi)
4)KUBETI NI DHAMBI
5)Kumwamini Yesu kristo pekee bila kufuata mafundisho na kuacha dhambi nyingine zote haitakusaidia chochote.IMANI BILA MATENDO IMEKUFA HAIFAI KITU.
 
Kuelewa kwa jambo fulani ama kutokuelewa ni maamuzi ya muhusika anaeeleweshwa, unazani ni jambo rahisi kumuachisha au kumkataza mtu jambo ambalo liko kwenye damu.
Inabidi uendelee kumwambia ili ajue kwamba hicho alichoruhusu kitawale mpaka kwenye damu yake ni kirusi kimpelekacho upotevuni
 
Ndiyo. Maana yatupasa kutafuta maarifa kila uchwao, kusoma chuo cha biblia au kuijua biblia pekee haitoshi. Ni vyema kupata maarifa zaidi na zaidi ili unapofanya reference uwe na hakika kwa kile usemacho na kukinena kwa uthabiti
 
Kwa muktadha wa namba moja hapo juu kula wali na ugali kwa wingi ni dhambi? Kwa sababu vina athari hasi?

Kama siyo dhambi kula ugali kwa wingi, basi hata kunywa Pombe kwa Wingi siyo dhambi badala yake utaharibu mwili wako tu.

Biblia inasemaje kuhusu mwili...
Yohana 6
63. Roho ndiyo itiayo uzima, mwili haufai kitu; maneno hayo niliyowaambia ni roho, tena ni uzima.

Wewe kama hunywi pombe kwa kigezo cha kumfurahisha Mungu unajidanganya.
Kama unatamani kuangalia mpira lakini unajizuia kwa kigezo cha kumfurahisha Mungu bado umelala.

Mungu yupo ili akufurahishe wewe, siyo wewe kumfurahisha Mungu.
 
2)Kuvaa suruali katika context ya kiroho kiimani imani ya kikristo na msingi wa mafundisho ya imebainisha bayana MWANAMKE ASIVAE MAVAZI YAMPASAYO KUVAA MWANAUME

3)HERENI KUSUKA MAPAMBO biblia imekataza ipo mistari mingi tafuta utaona hata ukigoogle utaipata
Je unajua kuwa biblia imekataza hata kuchonga pembe za ndevu zako?

Unajua kuwa biblia imekataza kulima mazao mawili tofauti kwenye shamba moja?

Unajua kuwa biblia imekataza kuvaa nguo material tofauti e.g chupi ya Cotton na gauni la nylon?


Ukiendelea kusoma Bible kijinga namna hiyo bado una safari ndefu. Kaa chini tafuta mwalimu upya.

YouTube, Christian-StackExchange kote huko utapata maarifa mapya.
 
mwalimu mpya tunayetakiwa kumtafuta ni ROHO MTAKATIFU ,tukiongozwa na Roho mtakatifu atatusaidia kujua ukweli,na kuishi katika kweli.
 
Hapa tukubaliane kutokubaliana,sisi wanadamu tunatakiwa tuishi tukimtii na tukimpende Mungu halafu kwq kufanya hivyo Mungu atatubariki,atatupendezesha.Kusudi la sisi kuumbwq ni ili tumpende na kumpendezesha Mungu na pia tupendane sisi kwa sisi wanadamu.UPENDO tumpende Mungu na kumtii,tupendane wanadamu sisi kwa sisi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…