Haya ni madhara ya mfumo dume tuliojiwekea sisi wenyewe.
Siwezi mlaumu mama peke yake, labda mama ntamlaumu 45% na jamii 55%.
FirstLady1, umeweza ona ubaya huo sababu umewezeshwa kujitambua na jamii inayokuzunguka.
Je umeangalia mazingira ya huyo mama yakoje? Kuanzia elimu, kipato, malezi aliyopata.
Ngoja niendelee kueleza kidogo.
Mwanamke akipata mimba kabla ya ndoa, jamii inamtazamaje? anahukumiwaje? Je mimba inakuwa kapata peke yake? Na je ana hata huo uwezo kwa wakati huu kumhudumia mtoto wake? Aliyezaa naye anachangia au hata anamtambua mtoto huyo? ni wangapi wako tayari kumsaidia mwanamke huyo hata kwa machngo wa mawazo chanya jinsi ya kuendelea na maisha yake?
Jamii imemwaminisha kwa kiwango gani kuwa mwanamke bila mume hajakamilika? Hapa ppenyewe utasikia mwanamke kuolewa muhimu. Na nachukulia mtu anayeweza kuingia jf angalau ana elimu hata ya fomu foo au hata kama hana uelewa ni mtu anayeweza angalau jitegemea na kuweza kuwa na kipato cha ziada cha kulipia intanet. Huyu mama amekua akiaminishwa mwanamke lazima aolewe, halafu leo ana mtoto ambaye anamzuia kuolewa, kwa nini asiondoe kikwazo chake cha kuolewa ili aolewe?
Hapa naweza uliza, ni wanawake wangapi waliowezeshwa na wametoa mimba kwa kuhofia kutoolewa kama watazaa kabla ya kuolewa? wanatofautiana na huyu? N ttfauti yao iko wapi?
Unajua huyu mama ni kiashiria(symptoms) cha kuwa kuna tatizo lakini si chanzo(cause) cha tatizo.
Kwanza jamii inabidi tukubali mfumo wetu wa maisha unatatizo na wanawake wamekuwa waathirika mara nyingi.