Tunamaliza mwaka 2021 taifa limegawanyika na CCM imegawanyika

Tunamaliza mwaka 2021 taifa limegawanyika na CCM imegawanyika

Usichokijua ni kwamba CCM ina wanachama zaidi ya milioni 15 na kila mwanachama analingana na mwingine kwenye ujenzi wa chama hivyo inapotokea mwanachama mmoja au wawili wameamua kuasi hiyo ni sehemu ndogo sana ya kuweza kuleta uharibifu wa kupelekea tishio kwa CCM
Wewe ndiyo umelala usingizi mzito! Kuna chama chenye wanachama milioni15? Wekeni tume huru muone.
 
ACT ina uafadhali kidogo, japo kinapigwa vita na wanywa gongo wa chama kile kisichopenda umoja wa kitaifa, ambacho kazi yake ni kususia kila jambo lenye manufaa kwa taifa.
Kuna mzee mmoja alishawajibu, wamechanganyikiwa
 
As long as majeshi bado ni matiifu kwa raisi, "then bado ccm ni moja na taifa bado ni moja". Hiyo ndo nguvu ya mshikamano wetu kama taifa........
 
Danganya wa huko kwenu. Wajuvi wa mambo tunajua kwamba chama kina watu wasiozidi 50 tu ambao ndiyo kauli na minyukwno yao inqbadili upepo wa siasa ndani ya chama. Wengine mnafuata midundo tu. Siku hao 50 wakiamua kugawana fito hakuna chama hapo.
Watu 50 ni wengi sana.

Kama utakumbuka CC wakati wa uchaguzi wa 2015 ilikuwa na wajumbe 32.

Mkiti JK akaja na majina matano, BKM, JYM, JPM, ARM na ASA

Wajumbe watatu wa CC (Nchimbi, Kimbisa na Sofia Simba) walimgomea mkiti kwanini aje na majina 5 badala ya wote waliochukua fomu wajadiliwe.

Bila shaka kuna watu wachache sana ambao wana nguvu kubwa ya ushawishi na muono wa mambo yaendeje. Wengine wanawaita "deeo state" who knows.

Cha msingi tuombe Mungu kuwe na utulivu, kama watu wanabishana kwa hoja basi maisha yaendelee, isifikie ile hali ambayo JK alisema sio rahisi watu kuachiana glass za vinywaji.

Nadhani mijadala ya tukope au tusikope, na kama tunakopa tunawekeza kwenye nini ili tupige hatua haraka kama nchi, hii mijadala ina tija kwa kupanua ufahamu, tumejua ni kiasi gani tunadaiwa na debt threshold ikoje kwetu (Tanzania).

Tutakiane heri za Mwaka mpya 2022, tuishi kwa ku-debate ila tubaki tukiheshimiana pasi kutwezana au kuwabagaza wale ambao tunatofautiana kwa hoja.
 
Watu 50 ni wengi sana.

Kama utakumbuka CC wakati wa uchaguzi wa 2015 ilikuwa na wajumbe 32.

Mkiti JK akaja na majina matano, BKM, JYM, JPM, ARM na ASA

Wajumbe watatu wa CC (Nchimbi, Kimbisa na Sofia Simba) walimgomea mkiti kwanini aje na majina 5 badala ya wote waliochukua fomu wajadiliwe.

Bila shaka kuna watu wachache sana ambao wana nguvu kubwa ya ushawishi na muono wa mambo yaendeje. Wengine wanawaita "deeo state" who knows.

Cha msingi tuombe Mungu kuwe na utulivu, kama watu wanabishana kwa hoja basi maisha yaendelee, isifikie ile hali ambayo JK alisema sio rahisi watu kuachiana glass za vinywaji.

Nadhani mijadala ya tukope au tusikope, na kama tunakopa tunawekeza kwenye nini ili tupige hatua haraka kama nchi, hii mijadala ina tija kwa kupanua ufahamu, tumejua ni kiasi gani tunadaiwa na debt threshold ikoje kwetu (Tanzania).

Tutakiane heri za Mwaka mpya 2022, tuishi kwa ku-debate ila tubaki tukiheshimiana pasi kutwezana au kuwabagaza wale ambao tunatofautiana kwa hoja.
Mungu iokoe TZ
 
Back
Top Bottom