Tunamuhitaji Mohammed Hussein

Tunamuhitaji Mohammed Hussein

homeless1

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2020
Posts
427
Reaction score
950
1.Hakuna beki tatu Tanzania mwenye kuufikia au hata kuukaribia uwezo wa Mohammed Hussein hilo naomba wanasimba wenzangu tulijue.

2. Ni mchezaji mwenye uwezo mkubwa sana kiasi kwamba tukimpoteza itatubidi twende nje kumtafuta kiasi kwamba tutakua tunaongeza gharama na ubahatishaji usio na maana imagine Zimbwe anaondoka anakuja beki toka nje uwezo anazidiwa na hata Yasin Mustafa

3. Simba tuna wachezaji wa kigeni zaidi ya 10 tena wenye uwezo mkubwa kiasi kwamba tutahitaji kuwabakisha sasa tukishindwa kumuongezea mkataba Zimbwe itatubidi tuongeze rundo la wachezaji toka nje, itafaa nini wakati uwezo wa zimbwe hakuna mwanamichezo asoujua.

4. ukifuatilia jinsi Simba anacheza utagundua kuna mchango mkubwa sana wa Zimbwe yaani mkubwa mno sio kwenye kuzuia, kumiliki, kushambulia au hata kupunguza presha za wachezaji wengine, Zimbwe anatu offer vitu vingi mno.

5. Kawa kwenye kipindi Simba inapitia kipindi kigumu kiuchumi mpaka sasa, kwanin uongozi usimpe offer nzuri kipindi hiki uwezo wa kiuchumi upo.

6. Ni captain msaidizi tena aso na majivuno wala dharau na ana nidhamu ya hali ya juu,wachezaji wengine watauchukuliaje uongozi wa Club kama wakishindwa kumbakisha Zimbwe.

7. Hakuna mchezaji mkubwa kuliko Simba lakin niukweli Zimbwe akiondoka tutayumba na Sisi mashabiki tutawazingua kama mkileta mchezaji ambae hatupi anachotupa Zimbwe.

8. Zimbwe kwa macho ya kawaida hayupo tayari kuondoka Simba lakini anahitaji maslah kwa sababu mpita kwake ni maisha hasa ukizingatia anaona kabisa Uongozi unaweza kufikia mahitaji yake.

9. Mashabiki wa kweli wa Simba hatuyawaelewa Zimbwe akiondoka labda aende Club kubwa kupita Simba.

NB : Malizaneni na Zimbwe tuwe na Amani
 
kabla meneja hajaropoka akishiriana na rafiki yake shaffih dauda zimbwe alisema simba wamepishana naye shilingi milioni 2 tu, alitaka mshahara between 8-10 millions a month na signing fee ya 70 milioni, simba wakakubali ila signing fee wakasema wanatoa 68 millions
kesho yake klabu ikatukanwa vya kutosha kwenye media na meneja muhuni na shafih dauda naye akaporomosha kebehi za kutosha kwa CEO wa team.

Hata akipewa makataba mpya haina maana atacheza kwa kinyongo maana meneja wake analalamika kijana wake haitwi ofisini kwa MO kunywa kahawa na kupiga picha, ujinga mtupu.

Siyo vibaya akachukue milions 100 ya yanga na mshahara wa milions 10 kila mwezi kule atathaminika, kuhusu namba tatu yupo gadiel michael atakuja Luhende wa kagera au Bryson wa KMC inatosha.
 
Huyo Meneja wake anamharibu njaa inamsumbua tu! Kama vipi asipewe mkataba sidhani kama anajifunza kitu kutoka kwa Singano...!??!!
 
Hizo biashara tu ili Zimbwe apandishiwe dau kama ilivyo kwa Chama,ila 100% haendi popote atabaki Simba.

Ila na msifu wakala wake Zimbwe ana akili anajua kuwajambisha Simba ili mchezaji wake apewe dau kubwa.
simba wakimuongezea mkataba nitawadharau sana siyo kujambishwa WAMEDHARAULIWA SANA kujambishwa tushajambishwa na chama,hata kagere alishawahi kujambisha kwamba zamalek wanamtaka mara team ya la liga inamtaka leo kuna manula na meneja wake jemedari said wanajambisha kwamba kuna dau la mshahara milioni 18 kwa mwezi pale sudan lakiini ushawahi kuona mgogoro wa kibwege kama wa zimbwe?
HERRY MZOZO NA SHAFFIH DAUDA WAMETUKERA SANA NI DHARAU KUBWA KWA KLABU ,DAUDA ALIFANIKIWA KUIDHALILISHA SIMBA 2015 ISSUE YA SINGANO NAONA KARUDI TENA, KUMUONGEZA MKATABA ZIMBWE ITAKUWA NI UDHAIFU MKUBWA SANA KWA SIMBA
 
Ni kweli ana kiranga lakini tusiwe na hasira hadi kumuacha Zimbwe
Huyo Meneja wake anamharibu njaa inamsumbua tu! Kama vipi asipewe mkataba sidhani kama anajifunza kitu kutoka kwa Singano...!??!!
 
Kama ni kweli huo ndo utani sasa wanashindwaje hizo 2m
kabla meneja hajaropoka akishiriana na rafiki yake shaffih dauda zimbwe alisema simba wamepishana naye shilingi milioni 2 tu, alitaka mshahara between 8-10 millions a month na signing fee ya 70 milioni, simba wakakubali ila signing fee wakasema wanatoa 68 millions
kesho yake klabu ikatukanwa vya kutosha kwenye media na meneja muhuni na shafih dauda naye akaporomosha kebehi za kutosha kwa CEO wa team.

Hata akipewa makataba mpya haina maana atacheza kwa kinyongo maana meneja wake analalamika kijana wake haitwi ofisini kwa MO kunywa kahawa na kupiga picha, ujinga mtupu.

Siyo vibaya akachukue milions 100 ya yanga na mshahara wa milions 10 kila mwezi kule atathaminika, kuhusu namba tatu yupo gadiel michael atakuja Luhende wa kagera au Bryson wa KMC inatosha.
 
Kama ni kweli huo ndo utani sasa wanashindwaje hizo 2m
unajua maana ya negotiation mkuu? sasa simba wameshindwa meneja keshasema yanga kuna milions 100 za kusaini na milions 10 kwa mwezi mara south africa kuna milions 23 mshahara kwa mwezi wansubiri nini sasa?si waondoke kelele ziiishe?
Of all people yaani back up ya kupigisha SHORT ni shaffih dauda?yule mhaya ana dharau sana watu wameghafilika sana kwa kweli waende tuuuu tena dauda atamsaidia sana kama alivyomsaidia Ramadhani singano
 
Kama ni kweli huo ndo utani sasa wanashindwaje hizo 2m
Yaani mkuu hata mimi nashangaa kwahiyo wakamuacha mchezaji atoke kabisa ofisini kisa milion 2 tu why wasingempa hiyo Mil.70 na suala lingekuwa limeisha ina maana wao wanashaka Zimbwe Jr hastahili hilo dau na mshahara wa mil 8 kwa mwezi
 
Yaani mkuu hata mimi nashangaa kwahiyo wakamuacha mchezaji atoke kabisa ofisini kisa milion 2 tu why wasingempa hiyo Mil.70 na suala lingekuwa limeisha ina maana wao wanashaka Zimbwe Jr hastahili hilo dau na mshahara wa mil 8 kwa mwezi
keshahsaini mkataba mpya
zimbwe.JPG
 
Zimbwe anaenda Yanga kuungana na Shaaban Juma wa As Vita. Huku Zimbwe anapiga 3 kule Shaabani Juma ana piga 2
 
Majina huwa yanajirudia sana.

Mohammed Hussein alikuwa mchezaji wa zamani sana miaka ya 90s.

Erasto Nyoni pia naye alikuwa mchezaji miaka ya 90s.
 
Nahodha Msaidizi wa Simba Mohammed Hussein 'Zimbwe Jr' ameongeza mkataba kuendelea kukipiga na mabingwa hao wa nchi

Wiki hii Zimbwe Jr alikuwa gumzo sana kweny..
Soma zaidi hapa : Zimbwe yupo sana Msimbazi
 
unajua maana ya negotiation mkuu? sasa simba wameshindwa meneja keshasema yanga kuna milions 100 za kusaini na milions 10 kwa mwezi mara south africa kuna milions 23 mshahara kwa mwezi wansubiri nini sasa?si waondoke kelele ziiishe?
Of all people yaani back up ya kupigisha SHORT ni shaffih dauda?yule mhaya ana dharau sana watu wameghafilika sana kwa kweli waende tuuuu tena dauda atamsaidia sana kama alivyomsaidia Ramadhani singano
Singano alifanyeje kaka
 
Singano alifanyeje kaka
umesahau sakata la 2015 dauda alimepeka azam,kaenda mazembe kaonekana garasa kapelekwa nkana kawa kituko kumbuka nkana kwa sasa inakaribia kushuka daraja angalau ambokile anapata nmba hapo nkana..sasa alikuwa keshamgeukia zimbwe ila hela si ishatoka atakuwa kalipwa chake baada ya kumtukana CEO na team ya simba
 
simba wakimuongezea mkataba nitawadharau sana siyo kujambishwa WAMEDHARAULIWA SANA kujambishwa tushajambishwa na chama,hata kagere alishawahi kujambisha kwamba zamalek wanamtaka mara team ya la liga inamtaka leo kuna manula na meneja wake jemedari said wanajambisha kwamba kuna dau la mshahara milioni 18 kwa mwezi pale sudan lakiini ushawahi kuona mgogoro wa kibwege kama wa zimbwe?
HERRY MZOZO NA SHAFFIH DAUDA WAMETUKERA SANA NI DHARAU KUBWA KWA KLABU ,DAUDA ALIFANIKIWA KUIDHALILISHA SIMBA 2015 ISSUE YA SINGANO NAONA KARUDI TENA, KUMUONGEZA MKATABA ZIMBWE ITAKUWA NI UDHAIFU MKUBWA SANA KWA SIMBA
Nilikuwambia umeona,kwenye mpira haya ni mambo ya kawaida,club inajambishwa ili itoe dau kubwa.
 
Back
Top Bottom