Leo GENTAMYCINE natoa angalizo kwa wale ambao huko maofisini au katika maeneo mengine mnapokuwa na vyeo vya manaibu (makamu) wa ubosi mkiona wakubwa zenu wanakosea au wanaharibu muwe mnasema mapema au mnaachia ngazi kuliko kuendelea kuwa nao kiutendaji.
Halafu, ama wakistaafu kazi au wakifa ndiyo mnakuja kutuonyesha 'kimafumbo' kuwa mlikuwa hamkubaliani 'kimaamuzi' kwani wenye akili kubwa tutawatafsiri nyie si tu ni wanafiki bali pia mna 'vielementi' vya uchawi pamoja na vya ufitini pia.
Ninaamini message sent and delivered.
Kuna story moja sijui ina ukweli kiasi gani.
Kruschev alichukua madaraka baada ya Stalin kufariki, siku moja kwenye kikao ndani ya chama, Kruschev akapiga sana madongo kwa Marehemu Stalin. Kuna member mmoja akamwandikia swali Kruschev, "Mbona hukusema haya wakati Stalin yupo madarakani?". Baada ya swali kufika kwa Kruschev, alipolisoma akauliza "ni nani ameandika hili swali nimpe jibu lake?", kila mtu akapiga kimya. Akauliza tena, kila mtu kimya. Akawaambia, natumaini mmepata jibu.
Moral of the story, courage sio kitu chepesi, kwenye hizi nchi zetu zisizojali haki, Mamlaka ni kama bulldozer, na wewe ni papai tu. Watu kama kina Lissu na Mdude ni wachache sana, kwamba unafuatiliwa, unatekwa, unapigwa ,unaumizwa na bado unakuwa mwiba sio kazi ndogo. Kwani Ulimboka yupo wapi?
Unasema ukiona mkubwa anaharibu "sema" au "achia ngazi", yaani unaamini Vice President au Prime Minister anaweza sema dhidi ya mkubwa wake au unadhani anaweza kujiuzuru? Hiyo ni theory, practically that can never happen, labda sio hapa Tanzania.
Unamkumbuka yule Katibu Mkuu wa CCM aliyeona mambo yanaharibika "akasema ukweli", aliishia wapi?