Uchaguzi 2020 Tunasafiri na Antipas Lissu, chaguo la wengi

UTAKUJA UJE

Member
Joined
Aug 4, 2020
Posts
34
Reaction score
78
Nimeshangaa kumsikia mgombea u Rais wa chama cha mapinduzi akitumia vibaya kauli ya Mh Lissu-Rais mtarajiwa wa awamu ya sita na kipenzi cha watu,aliyoitoa akiwa Mwanza kwamba yeye Lissu hayuko tayari kupewa kazi na Magufuli, badala yake akasema hiyo kazi akawape anaowaokota majalalani.

Hapa Lissu alikuwa sahihi kwani Magufuli akiwa Singida ni kama alimdhihaki Lissu kwamba aachane na kugombea badala yake asubiri atapewa kikazi kidogo ambacho ana uwezo nacho.Hii ni dharau kubwa kwa msomi huyu nguli wa sheria,na nataka nimkumbushe Magufuli,yeye hana hati milki ya taasisi ya urais kiasi cha kumtaka Lissu asubiri kupewa kikazi kidogo.Kwa nn yy Magufuli asiachie hiyo nafasi na asubiri Lissu ampe japo nafasi ya kuzibua mchanga kwenye madaraja makubwa?

Kauli ya Lissu ya kutaka Magufuli awape kazi anaowaokota jalalani imerejea alichowahi kusema Profesa Kabudi kwamba anamshukuru Magufuli kwa kumtoa jalalani na kumpa hiyo kazi ya kuteuliwa.Watanzania wote tulisikia na Magufuli anatakiwa kujua kwamba SISI WATANZANIA SIYO WAJINGA!

Nimemshangaa leo akiwa Mkoani mara anaitumia ndivyo sivyo kauli ya Lissu kwamba aliwaita watumishi wote ni majalala. Bila aibu akawataja wateule wake wengi, walimu, waganga, maaskari nk. Magufuli usitupotoshe, nadhani kwa matendo yako unatakiwa kupewa kauli kali zaidi ya hizo kwa maana umetutesa sana Watanzania tulio wengi.

Kituko kingine alichofanya mh Magu ni pale aliposema kwamba ataongeza mishahara ya watumishi kabla hajamaliza muda wake. Ni kichekesho kweli!We unajuaje utaendelea kuongoza? Na kama unajua utaendelea kuwa Rais,kampeni unafanya za kazi gani?Kipindi chako cha miaka mitano kimeisha na sasa wewe ni mgombea huna uhakika wa kushinda ndo maana unatafuta huruma tu!Nafikiri wapenda haki kote dunia wanapaswa kuungana kukukataa kwa nguvu zote!Miaka mitano kila mmoja analia,ukiongezewa miaka mitano si utaua Watanzania wote?Hapana,tumechoka,inatosha,kapumuzike ulikojijengea uwanja wa ndege,TUNASAFIRI NA ANTIPAS LISSU TUNDU,Chaguo la wengi,chaguo la Mungu.HATUDANGANYIKI,SASA,BAAAAAAAASI!
 
Awamu ya Kwanza kakataa kuajir wala kuongeza mishahara wakat bad anauhitaji wa kupata awamu ya pili je tukimpa awamu ya pil ataajiri kweli na kuongeza mishahara wakat ndo awamu ya mwsho hana cha kupoteza baada?

SINA CHAMA WALA SIPIGI KURA
 
Awamu ya Kwanza kakataa kuajir wala kuongeza mishahara wakat bad anauhitaji wa kupata awamu ya pili je tukimpa awamu ya pil ataajiri kweli na kuongeza mishahara wakat ndo awamu ya mwsho hana cha kupoteza baada?

SINA CHAMA WALA SIPIGI KURA
Hapa alikosea sana ...tatizo mbishi japo anafanya mambo makubwa kapuuzia watumishi na ajira mpya
 
Mkuu punguza jaziba, unatukana daktari mshono haujatolewa nyuzi!
.
Hivi Magu alivyo popular wa ukweli akashinda kihalali kwa kishindo, utasingizia tume imekwapua matokeo?

Ninakushauri safari hii jiandae kisaikolijia, maana dalili za ushindi mnono kwake zipo dhahiri.

Halafu hili la majalala pia nawe umelikuza mno ama umelitafsiri ndivyo sivyo.

Palamagamba mwenyewe aliwahi kulitolea ufafanuzi tamko lake hilo huku akinukuu vifungu vya biblia kwamba hakumaanisha jalala unalotafsiri wewe leo kwa kutokujua ama kwa makusudi.

Kila mwanasiasa ana staili yake ya uongozi hapa duniani na pia binadamu hatujaumbwa kwa ukamilifu.

Maana hata huyo unayempigia debe mheshimiwa Lisu akitawala hawezi kuridhisha kila mtu, naye atalaumiwa pia tena sana tu.

Nyerere mwenyewe muasisi, leo anasifiwa kwa utawala bora, lakini alitawala kwa fimbo ya chuma na yeye aliwahi kukiri wazi wazi, sembuse Munghwaye!

Kwa waAfrika tulivyo, siwezi kumsifia mtu kwa kubet nini atakacholifanyia taifa eti kwa tu kanadi propaganda hizi dhaifu.

Aheri huyu Magu tumemuona, Taifa analisongesha kwa kasi inayotarajiwa.

Wewe ulivyo mbinafsi unalalamikia mshahara, je sisi wakulima tumeongezewa bei ya mazao, na kwa thread yako hii sisi unatuweka kundi gani?

Kwa taarifa yako, huyu ndiyo rais bora kabisa kuwahi kutokea Tanzania na nchi nyingi barani Afrika kama mfano na dunia kwa ujumla wake, kila mahali wanamlilia kuwa aheri angelikuwa ni rais wao kwa jinsi anavyoliletea taifa la Tz maendeleo yenye kuonekana.

Mimi si mpiga kura mzuri, lakini kwa thread kama hizi, zitanifanya siku hiyo ya trh 28 potelea kwa mbali nami niende nikasongamane ili kuongeza nguvu, maana sasa ngebe zinataka kuzidi kudadadeki.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na liroho lake libaya, apambane na halii yake
 
Hao walimu, waganga, mapolisi, wanajeshi? Usalama, ma- Rc na MaDC wanamuona kama kichekesho anataka kujitetea tu. Kauli ya Lissu iko wazi na ya Kabudi ilikuwa wazi.

Mzee amekosa majibu anatafuta vichaka.

Watanzania sio wajinga
 
Magu ana upopula gani?? Ukiachana na nguvu ya Polisi na usalama ana upopula gani?? Nakwamimbia tu pale ccm angeruhusu fomu zaidi ya moja tu asingechomoka.
 
Hapa alikosea sana ...tatizo mbishi japo anafanya mambo makubwa kapuuzia watumishi na ajira mpya
Alijifanya mjuaji sana. Yaani yeye alivyowapa vyeo mademu zake na wapiga mapambia akina Makonda, Mnyeti, Gambo et al akaona amemaliza.
 
Awamu ya Kwanza kakataa kuajir wala kuongeza mishahara wakat bad anauhitaji wa kupata awamu ya pili je tukimpa awamu ya pil ataajiri kweli na kuongeza mishahara wakat ndo awamu ya mwsho hana cha kupoteza baada?

SINA CHAMA WALA SIPIGI KURA
We kweli mcheza kamari.
 
Huyu mzee ni muongo mnoo alafu ana udikteita mkubwa sana,anajiona yeye ni bora Sana duniani kuliko mtu yeyote,hana huruma na sio mnyenyekevu kanisani anaenda kuahadaa watu .
 
Watanzania wote wangewaza kama Mimi magu angepumzishwa safari hii.Ndio kuna mambo mazuri kayafanya, lakini kuna mambo mabaya zaidi kayafanya awamu yake ya kwanza.Haki za watu zimekanyagwa hakuna mfano. Wafanyakazi wamepuuzwa kiasi cha kutosha, wafanyabiashara ni kilio. Wakulima usiseme.kutekana ndo balaa.Tunaomba ajaribu mwingine
 
Magu ana upopula gani?? Ukiachana na nguvu ya Polisi na usalama ana upopula gani?? Nakwamimbia tu pale ccm angeruhusu fomu zaidi ya moja tu asingechomoka.
U popular asiwe nao kwa nini, anao sana tu.

Kwa sisi vizurula, hali halisi tunaoina kila kona tunakotembelea nchini.

Sema kuna kitu anakikosea: kuendelea kuvumilia figisu za wasimamizi wa uchaguzi na pia kudharau mchakato wa katiba mpya.

Hayo mawili angelimalizana nayo mapema kabisa, maana yanampunguzia 'marks' zake halali na kuuchafua utawala wake.

Mimi ninapenda sana uchaguzi ulio huru, wazi na haki.

Mfumo walioutumia kwenye kura za maoni, ungeliboreshwa ukatumika na kwenye uchaguzi mkuu ningelifurahi sana, maana kuna watu wangelikosa pa kupumulia na ngebe zingelikatwa mazima.

Yaani box iwe ni marufuku kubebwa kwenda kuhesabiwa mahali nje ya kituo, biashara iishie hapo hapo chini ya usimamizi wa mawakala wakilindwa na 'wasalama' na matokeo kubandikwa hapo hapo vituoni.

Nakala za kura zihifadhiwe kwa ushahidi na kukiwa na malalamiko iwe ni rahisi ku recount na wahusika timu nzima kama itabainika wamechezea matokeo wachukuliwe hatua madhubuti za kukomesha upumbafu wao.

Kulealea huu uozo, rafu zisizo za lazima zitafanyika na lawama zitamwangukia yeye, maana tumeona kwenye chaguzi zilizopita, ukiwemo wa serikali za mtaa.

Lakini kama kwa kupendwa kihalali, Magufuli anapendwa sana tu na ategemee ushindi mnono kuliko ule wa 2015.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acheni mihemko isiyo na maana! Huu ni uchaguzi wa muujiza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…