Aman iwe nanyi wapendwa
Husika na kichwa cha habari
Kuna wengine tumetokea familia fulan za kitata kinoma yaan za kichawi huwez amin
Mimi had kijijin kwetu wanazengo home walikuwa wanatuogopa kinoma, yaan bibi yetu upande wa baba alikuwa ni mchawi sijapata kuona watu walikuwa wanamuogopa kinoma hakuna aliyekuwa ana bisha juu yake maana akikusonta tu ilikuwa lazima ujinyee kama sio kuzimia
Alikuwa anawapa masaa tu wale ambao walikuwa wanazinguana naye, yakiisha hayo masaa aliyokupa afu ukawa bado uko hai bas we mwanaume kweli na utakuwa umezindikwa ile mbaya
siku amefariki zengo ilifurahia sana
Ni hayo tu waku wangu
Mbalikiwe na bwana
Cc mbitiyaza
LONDON BABY
Nilijua kweli familia ya kichawi, kumbe hamna kitu hapo, bibi yako alikuwa kama mwanafunzi aliye kuwa kwanza shuleni kwao ambayo ni ya mwisho kitaifa kwa ufaulu.
Kisa changu nilinyoosha mikono
Ulikuwa mwaka wa 1956 nilijikuta njia panda, nilikuwa simjui huyu jamaa nilijikuta tuu nimeingia nae kwenye mtafaruku. Aseee aliniambia kuwa kesho sitofika mwaloni tulipokuwa tunafanyia shughuri zetu wakati huo vuguvugu za uhuru zikisikika na kila mmoja akiwa anatamani kuuona huo uhuru, simanzi yangu ilikuwa kubwa kwa kutoshuhudia uhuru huo.
Aseeee mi nikameambia mzee wangu enzi hizo mkasa mzima. Mzee alinicheka tuu, mwisho wa siku akaniambia mi ni mjinga,
Baadae aliongea neno moja tuu,
Baba yake na huyo kijana atakuja kesho kuomba msamaha., nilishtuka mnoo
Jioni ilifika na nikiwa na mawazo mnoo kutoiona kesho na hasa kutouona uhuru. Asee usiku sikulala nikisubiria, ghafla niliisikia sauti sijui ilikuwa inamanisha nini, kama mda mfupi mzee alinifuata kwenye banda langu, akaniambia kesho nichague cha kuongea na mzee wa yule kijana lakini niuchunge sana ulimi wangu.
Nilipitiwa na usingizi baada ya kuongea na mzee
Kama asubuhi nikajikuta mzima na yule jamaa alikuja mitaa yetu kucheki kama kuna msiba bahati mbaya akaniona nikiwa natoa ndama.
Haikufika jioni asee hali yake ikabadilika mzee wake alikuwa mchawi kinyama ila hakujua ukweli kuhusu baba yangu. Alijigamba mnooooo mpaka tukashauriwa kuhama asiimalize familia.
Aliingia kwenye mitambo yake kuifyeka familia yetu, masikini hakuijua hii familia kilichotokea hakukiamini, walioshuhudia walisimulia alipigwa radi nakumbuka ilikuwa kiangazi cha kushangaza mzee hakushtuka kama alilijua hili. Ni kweli alilijua kabla
Yule mzee ikabidi aitishe kikao cha wachawi katika kanda ile hasa wa kutoka burundi kongo na wenyeji wao kigoma. Hizi ni kwa mjibu wa mzee wangu aliponipa taarifa nijiandae kwa kuombwa msamaha. Kikao kikiwa kati kati mmoja akauliza, tunakaa kikao lakini hakuna baraka zote kutoka kwa mkuu, huyu mzee hakuwahi kumuona mkuu wake. Ikabidi wafanye tuu kea kuwa ni dharura na mkuu atapewa taarifa ili aziwasilishe kwa bwana mkubwa.
Ndipo mzee alielezea namna alivyodhalilishwa na kuonekana sio kitu, ghafla akalitaja jina ambalo lilipaswa lishughulikiwe, ambalo ni jina langu asee
Mungu wangu kikichotokea woote walitetemeka kulisikia jina hili na kumsihi anitafute na amtafute mzee ndiye kiongozi wa afrika mashariki na kati
Aseee baada ya siku mbili nilimuona mzee nyumbani akiwa mpole mnoo
Ngoja niishie hapa