Nan alikwambia kwamba wachawi si wa mungu? Wakati yeye mungu hao wachawi ndo kawaumba na kuwapa huo uwezo wa kichawiTubarikiwe na Bwana yupi sasa..maana wachawi na Mungu ni tofauti
young kilimanjaro
Ahahahaha mkuu umetisha tutakupa cheo uwe mwenyekiti wetu na mshana atakuwa katibu mkuuNilijua kweli familia ya kichawi, kumbe hamna kitu hapo, bibi yako alikuwa kama mwanafunzi aliye kuwa kwanza shuleni kwao ambayo ni ya mwisho kitaifa kwa ufaulu.
Kisa changu nilinyoosha mikono
Ulikuwa mwaka wa 1956 nilijikuta njia panda, nilikuwa simjui huyu jamaa nilijikuta tuu nimeingia nae kwenye mtafaruku. Aseee aliniambia kuwa kesho sitofika mwaloni tulipokuwa tunafanyia shughuri zetu wakati huo vuguvugu za uhuru zikisikika na kila mmoja akiwa anatamani kuuona huo uhuru, simanzi yangu ilikuwa kubwa kwa kutoshuhudia uhuru huo.
Aseeee mi nikameambia mzee wangu enzi hizo mkasa mzima. Mzee alinicheka tuu, mwisho wa siku akaniambia mi ni mjinga,
Baadae aliongea neno moja tuu,
Baba yake na huyo kijana atakuja kesho kuomba msamaha., nilishtuka mnoo
Jioni ilifika na nikiwa na mawazo mnoo kutoiona kesho na hasa kutouona uhuru. Asee usiku sikulala nikisubiria, ghafla niliisikia sauti sijui ilikuwa inamanisha nini, kama mda mfupi mzee alinifuata kwenye banda langu, akaniambia kesho nichague cha kuongea na mzee wa yule kijana lakini niuchunge sana ulimi wangu.
Nilipitiwa na usingizi baada ya kuongea na mzee
Kama asubuhi nikajikuta mzima na yule jamaa alikuja mitaa yetu kucheki kama kuna msiba bahati mbaya akaniona nikiwa natoa ndama.
Haikufika jioni asee hali yake ikabadilika mzee wake alikuwa mchawi kinyama ila hakujua ukweli kuhusu baba yangu. Alijigamba mnooooo mpaka tukashauriwa kuhama asiimalize familia.
Aliingia kwenye mitambo yake kuifyeka familia yetu, masikini hakuijua hii familia kilichotokea hakukiamini, walioshuhudia walisimulia alipigwa radi nakumbuka ilikuwa kiangazi cha kushangaza mzee hakushtuka kama alilijua hili. Ni kweli alilijua kabla
Yule mzee ikabidi aitishe kikao cha wachawi katika kanda ile hasa wa kutoka burundi kongo na wenyeji wao kigoma. Hizi ni kwa mjibu wa mzee wangu aliponipa taarifa nijiandae kwa kuombwa msamaha. Kikao kikiwa kati kati mmoja akauliza, tunakaa kikao lakini hakuna baraka zote kutoka kwa mkuu, huyu mzee hakuwahi kumuona mkuu wake. Ikabidi wafanye tuu kea kuwa ni dharura na mkuu atapewa taarifa ili aziwasilishe kwa bwana mkubwa.
Ndipo mzee alielezea namna alivyodhalilishwa na kuonekana sio kitu, ghafla akalitaja jina ambalo lilipaswa lishughulikiwe, ambalo ni jina langu asee
Mungu wangu kikichotokea woote walitetemeka kulisikia jina hili na kumsihi anitafute na amtafute mzee ndiye kiongozi wa afrika mashariki na kati
Aseee baada ya siku mbili nilimuona mzee nyumbani akiwa mpole mnoo
Ngoja niishie hapa
Mkuu hapana, mshana jrAhahahaha mkuu umetisha tutakupa cheo uwe mwenyekiti wetu na mshana atakuwa katibu mkuu
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu acha kunishawishi bakini na uchawi wenuNan alikwambia kwamba wachawi si wa mungu? Wakati yeye mungu hao wachawi ndo kawaumba na kuwapa huo uwezo wa kichawi
Sent using Jamii Forums mobile app
Hakuna anayekushawishi hapa we mpare lakin hata wachawi wametoka kwa munguMkuu acha kunishawishi bakini na uchawi wenu
young kilimanjaro
Nan kakwambia kuwa mimi nina chuki na king kibaNdo maana una chuki na king kiba kumbe ni uchawi
Lakin mkuu kwa hayo maelezo yako hapo juu unatosha kabisa kuwa mwenyeketi wetu humu ndanMkuu hapana, mshana jr
Huyu anaroho ya kichawi lakini anashindana mno na anahangaika namna ya kuikimbia japo huwa anatumiwa huku akiwa hajuwi, huyu yuko kwenye utumwa mkuu na yupo kwa sababu za msingi.
Anaifanya shughuri ya kichawi huku akiwa hajui na anaichukia mnoo.
Kwa sasa anapambana sana na nafsi yake mkuu
Mimi siwezi kuwa mwenye kiti kwani hua nina mdomo CHAFU mnoo kiyu ambacho mwenyekiti wa shughuri hizi hafai kamwe, labda niwasaidie kigooo kuna bint mmoja humu anastahili sana kwani yeye bado moto wa kichawi anao
Kwa mimi haiwezekani kwani niko kwenye harakati za kulikimbia hili pepo mkuu
Duh mkuu huyo babu yako alikuwa kiboko nan kaachiwa mikoba kweenye ukooUkweli Babu yangu kwa Baba, alikuwa mtata sana yule mzee, na mimi ndiyo nilipewa jina lake, nakumbuka matukio machache sana ya yule mzee,
Kwanza alikuwa kila jioni akienda kulewa lazima apigane, na alikuwa anawatukana matusi yanguoni na maudhi mengi hajali na sasa walikuwa wanamsubiri njiani wamfundishe adabu. Yule mzee bwana alikuwa anakita fimbo yake chini. Anaisimika. Sasa jamaa watapigana na iyo fimbo mpana mzee anaingia nyumbani kaisha lala. Alfajiri wanakuja kushituka mtu hayupo na walikuwa wanapigana wenyewe.
Yule mzee alikuwa hapishani na nyoka. Kila nyoka lazima anamchukua anamleta nyumbani anamfuga, siku moja nimetoka shule mchana nikaenda kwa bibi, jikoni nipewe chakula. Bibi akaangalia nikae wapi kanielekeza nikalie mfuko ile ya mbolea , sasa kumbe mle kwenye mfuko kuna chatu, kina nikikaa natereza najitengeneza nakaa ten, hivyo hivyo, mwisho bibi akaona napata shida akaniuliza kulikoni , akasea alaaa kuna vitu vya babu yako humo. Basi akanipa kigoda alichokuwa amekalia yeye akakaa chini. Nilipomaliza kula nikataka kuona mle kwenye mfuko kuna nini, bibi kanikatalia, utoto bwana ! Alivyojipindua bibi nikacheki bwana ,duuuu. Nikatoka baruu.
Siku nyingine bwana wakaja watu kuiba ng'ombe, maana babu alikuwa na ng'ombe hawapungui elfu mbili , na aliwafahamu wote kwa rangi, na aliwapa majina, kulingana na mazingira ya kuzaliwa, basi kuamka asubuhi bwana ng'ombe wameibwa madume kadhaa, baba wadogo wakamwambia babu wawafuate, babu kasema waacheni watarudi wenyewe, kama muujiza vile bwana. Wale ng'ombe walirudi mbio za ajabu wamenyenyua mikia juu juu, haikwisha wiki wale wezi wakaja kujieleza wenyewe,
Nacho sikitika yule babu hakuniachia utaalamu, yaani acha tuu, wakati anakufa alikuja kuniaga. Akalia sana akaniambia maneno machache, ninayakumbuka hata leo, lakini nilikuwa mdogo sikuweza kuelewa anamaanisha nini wakati ananiaga. Nilikuwa form one.
Babu kaondoka na ujuzi wake, ningeachiwa mngenikoma.Duh mkuu huyo babu yako alikuwa kiboko nan kaachiwa mikoba kweenye ukoo
Sent using Jamii Forums mobile app
Nan alikwambia kwamba wachawi si wa mungu? Wakati yeye mungu hao wachawi ndo kawaumba na kuwapa huo uwezo wa kichawi
Sent using Jamii Forums mobile app