Uchaguzi 2020 Tunatukanwa kwakuwa tumeona yaliyofanywa na Magufuli

Uchaguzi 2020 Tunatukanwa kwakuwa tumeona yaliyofanywa na Magufuli

kudamademede

Member
Joined
Jan 1, 2020
Posts
62
Reaction score
241
Ukipita mtandaoni kwenye kurasa zinazoendeshwa na vyama vya upinzani katika kipindi hiki cha kampeni, utaona mambo makubwa mawili.

Jambo la kwanza utaona majigambo kwamba wanapendwa na kila mtu na kwamba Oktoba 28 watashinda!! Jambo pili utakaloliona ni matusi makubwa yakielekezwa kwa kila mtu atakayeonekana anaipenda CCM.

Hii inatuma message mbaya sana na ya hatari kwa kila anayeipenda Tanzania. Lakini basi mngetukana kila mtu mkawaacha watumishi wa Mungu. Kumtukana mtumishi wa Mungu kwasababu anaonekana anapenda na kuyasifia mambo aliyoyafanya Magufuli ni kitendo kibaya sana.

Huku kurasa zikiendelea kutukana, viongozi wa vyama vya upinzani wanaonekana mstari wa mbele kuweka maoni yao (comments) kubariki matusi hayo. Watanzania na wazalendo, hawa wanaotukanwa ndio wanaoliombea taifa letu, ndio wanaunda kamati ya amani, ndio watahudhuria uapisho wa rais wetu.

Hata kama mnajua hamtashinda, msitukane viongozi wetu wa dini na kulifanya taifa letu kuonekana halina Mungu. Nashauri hii tabia isitishwe mara moja na tunaomba viongozi wa dini kote nchini kutoyumbishwa kwasababu ya matusi na vitisho vinavyotolewa na wapinzani.

Kama kufurahia maendeleo ya nchi ndio mtutukane basi tutawaonesha kuwa fimbo ya kuwapigia tarehe 28 iko kwenye nyumba za ibada ambazo sisi ndio viongozi wake.

Askofu Jonathan Mwakatobe
TAG Temeke
 
Amekufanyia wwe labda hakuna atukanwae kwa mazuri. Maendeleo ya vitu ni lzm yaguse kuendeleza watu
 
Ijue kwanza kazi ya mtumishi wa Mungu ndio uongee.Mtumishi wa Mungu haufangamani na Utawala dhalimu unaomkosea Mungu kwa kuzivunja amri kumi za Mungu.
 
Kuna Mtumishi wa Mungu anaeua watu? Anaeteka watu??? Anaebambikia watu kesi na kupiga risasi?

Acheni kumchafua Mungu kwenye huyo mjinga wenu na mnafiki
 
Askofu Bwana asifiwe,nimesikitika sana na mada yako hii,Ina maana katika hii miaka mitano ya utawala huu unakubaliana na matendo mabaya yaliyofanyika,unataka kutuaminisha kuwa matendo ya ukatili yaliyofanywa ilikuwa sawa.

Lissu alipopigwa risasi ilikuwa sawa, Aliphonce mawazo aliuwawa kikatili,hakuna kesi.watu wamepotea kwenu ni sawa.kwa hiyo flyover Ndo muhimu kuliko damu za watu zilizopetea.OK ila biblia inasema nyakati za mwisho uovu utaongezeka.
 
It is doubtful if your are really a bishop. You seem to be a politician. Aren't you?
 
Huyu naye atakuwa askofu wa wajinga kama alivyo Gwajima, aache upuuzi huwezi kumkumbatia muuaji ukakata upendwe na watu labda mashetani,
 
There are some powerful people in our country trying to make it difficult for us to vote for Tundu Antipas Lissu. You know why? Because they know when we vote, things change.
 
Back
Top Bottom