Uchaguzi 2020 Tunautakia heri Mkutano Mkuu wa CHADEMA, nyie ndio tumaini la wanyonge halisi

Uchaguzi 2020 Tunautakia heri Mkutano Mkuu wa CHADEMA, nyie ndio tumaini la wanyonge halisi

mimi sijapiga kura miaka mingi sana ila kwa mwaka huu nataka nikapoteze muda wangu kwa kupiga kura,ila tukiwekewa kituko wala sikanyagi.

Itakuwa wapuuzi ikifika msimu mnapandikiziwa mtu kan kwamba kama nyie hamjiwezi
 
Mkutano wenu unaoanza leo umebeba matumaini kwa Watanzania wanyonge sio wanyonge wa CCM kina MO.

Umebeba matumaini kwa wafanyakazi wa umma ambao hawajaongezewa mishahara kwa zaidi ya miaka mitano sasa.

Umebeba matumaini kwa wakulima na wafugaji ambao wamekuwa wakikopwa mazao yao na serikali ya CCM.

Mkutano unaoanza leo umebeba matumaini kwa wanafunzi wanaonyimwa mikopo na kupunguziwa mikopo yao na bodi ya mikopo licha ya kuwepo kwa mkataba.

Ni Mkutano unaowapa matumaini wafanyabiashara wanaoongezewa na kubambikiziwa kodi kubwa na TRA.

Ni Mkutano wa matumaini kwa wajasiliamali wakiwepo wamachinga na mama ntilie wanaosumbuliwa na migambo wa jiji.

Umebeba matumaini kwa wananchi wanaonyanyaswa na polisi kwa kubambikiziwa kesi na kunyimwa dhamana za wazi.

Ni Mkutano uliobeba matumaini kwa waandishi wa habari na vyombo vya habari vilivyonyimwa uhuru wa kuandika maoni huru.

Kifupi ni Mkutano wa matumaini kwa Watanzania wote.

Kila la heri Mkutano wa CHADEMA, ni mategemeo yetu kuwa mtatuletea chaguo la wananchi wanyonge.

View attachment 1524545
Safi kabisa CHADEMA.
 
Back
Top Bottom