Tunauza au tunanunua umeme?

Tunauza au tunanunua umeme?

Nchi yangu hii ni lini Viongozi watakuwa Wakweli.
Kwenye Kununua apo lazima watu wapige Dili yale yale Ya Richmond
Leo rais Samia amesema wapo kwenye mchakato wa kusaini mkataba ili tununue umeme kutoka kenya kwa ajili ya watu wa Kaskazini..
Sasa najiuliza kuna haja gani ya kununua umeme nchi jirani wakati tunatengeneza umeme wa zaida.?
Wajuzi wangekuja kutuelezea vzuri hii imekaaje kaaje​
 
Tutauza na kununua, ila tutakaouza utakuwa mwingi kuliko tutakaonunua, hivyo net effect itakuwa tumeuza.

Kanuni za kihasibu zimezingatiwa 😂😂😂
Tunauza Toka 2013 😃😀😀😀
20250309_175041.jpg
 
Hata kama huna shida na mayai, ukiona jirani yako ana mayai mengi na yamakaribia kumharibikia si unamuungisha tu?

Huo si ndio ubinaadamu na ujirani mwema? Au sio kijana Lucas Mwashambwa

Ila viongozi wa hii nchi 😂
 
Kuwaelewa CCM inapaswa uwe umefyatuka Akili,tofauti na hapo utakaribisha tatizo la afya ya akili!
Kweli kabisa mtani wangu. Haiingii akilini Eti sisi tuna zalisha umeme zaidi ya mahitaji yetu, na zilikuwepo habari kuwa mradi wa gread ya taifa inayojengwa kupitia mikoa ya Singida kuelekea kaskazini ita ungana na mtandao wa Kenya means tutawauzia umeme. Tanesco acha ujinga twambie status ya hali ya umeme Tanzania. Hauwezi kuwa na ziada ya kitu halafu ukanunua kama hicho toka duka jingine.
 
Leo rais Samia amesema wapo kwenye mchakato wa kusaini mkataba ili tununue umeme kutoka kenya kwa ajili ya watu wa Kaskazini..
Sasa najiuliza kuna haja gani ya kununua umeme nchi jirani wakati tunatengeneza umeme wa zaida.?
Wajuzi wangekuja kutuelezea vzuri hii imekaaje kaaje​
Tuna-UZNUA.
 
Mini natania tu mkuu.

Serikali ya Tanzania hata pale inapofanya jambo sawa ni vigumu kuitetea, kwa sababu inafanya mambo kwa usiri mkubwa.
Exactly naamini kabisa kwenye hili kuna kitu wananchi tumefichwa iwe kwa wena au kwa ubaya kuna jambo.
 
Kwanini sasa wakati tunazalisha wakutosha?
Shida kubwa umeme .....sio kama nyanya....kujenga miundo mbinu hadi unapotaka kuuza zaidi miaka 5.....je gharama zako na bei ina ushindani? Ethiopia wako Kenya long time umeme uko km 200 kutoka mpalani mwetu...easy kuleta na bei yao iko chini zaidi.....soma hapa

Ni kweli nchi ina umeme wa kutosha lakini haina maana kwasababu umeme upo wa kutosha basi unaweza kuupeleka popote pasipo kufanya tathmini!

Iko hivi umeme kutoka vyanzo vikuu vya umeme wa uhakika Rufiji na mikoa mingine ukitaka kuusafirisha kwenda mikoa ya kaskazini unakuwa unazungumzia mradi wa wastani wa 800km ~900Km

Gharama za kusafirisha umeme kwa umbali huo ni kubwa mno ukilinganisha na kuuchukulia hapo kenya .
Wanaposema umeme wa Ethiopia haina maana uko huko Ethiopia! Ni uko hapo jilani kenya wastani wa km 250km~300km tu

Hivyo ukichukulia gharama za kuusafirisha umeme kwa wastani 50mil kwa kila span moja ( nguzo moja hadi nyingine) hapa tutazungumzia wastani wa span elf 8000 hadi 9000 endapo utaamua kuutoa mikoa ya rufiji!

Soma Pia: Rais Samia: Serikali itanunua Umeme nje maalum kwa Mikoa ya Kaskazini

Mbali na gharama hizo mradi mkubwa kama huo unahitaji kulipa watu fidia na kuchepusha miundombinu itayoingiliana hapo katikati ya mradi!

Miradi ya mabomba ya mafuta yaliyopita ardhini yatalazimisha kubadilisha span badala ya kupitisha umeme juu ya bomba ushushwe chini (underground) ili kuepusha muingiliano wa frequency za umeme na zile za bomba la mafuta! Yote hayo yanapaisha gharama za mradi!

Muda wa kuujenga mradi mkubwa kama huo unaweza kuchukua miaka siyo chini ya mitano!

Upotevu wa umeme hapo katikati (power losses) kwa umbali huo ni Mkubwa ukilinganisha na faida utayovuna ukiuufikisha mikoa husika ya kaskazini!

Yote tisa hata kama umeme upo lakini kama jilani ana bei rahisi kuliko za nchi yetu kwanini kujichosha ilihali kwa jilani anao umeme karibu na ni bei nafuu zaidi?

Ambao hawajaelewa naomba kutoa mfano huu!
 
Back
Top Bottom