Tunawekwa katika madaraja ya kibaguzi.

Tunawekwa katika madaraja ya kibaguzi.

talentbrain

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2009
Posts
1,187
Reaction score
760
Mi nadhani hatuna malengo mazuri kwa taifa hili, walianza na kuwabeba wanawake, wakawekewa vigezo vya chini, mara wakawekewa viti maalum, mwisho wakasema wapewe uspika na wakapewa. Hawakuishia hapo wakaja kwenye elimu ya juu, ikawa si kufaulu tu mitihani bali combination ambapo bila kutafakari wakazishusha hadhi baadhi ya combination. Hawakuishia hapo wakaleta ujinsia, mara kwenye mikopo wakaja waliosomea private na government, hawakuridhika sasa wa NACTE wametengwa na kwakuwa tumezoea kubaguana sasa habari ya mjini ni kufiwa na wazazi wote ili upewe mkopo. Je, sisi wenye wazazi masikini tuwauwe wazazi wetu?
 
Mi nadhani hatuna malengo mazuri kwa taifa hili, walianza na kuwabeba wanawake, wakawekewa vigezo vya chini, mara wakawekewa viti maalum, mwisho wakasema wapewe uspika na wakapewa. Hawakuishia hapo wakaja kwenye elimu ya juu, ikawa si kufaulu tu mitihani bali combination ambapo bila kutafakari wakazishusha hadhi baadhi ya combination. Hawakuishia hapo wakaleta ujinsia, mara kwenye mikopo wakaja waliosomea private na government, hawakuridhika sasa wa NACTE wametengwa na kwakuwa tumezoea kubaguana sasa habari ya mjini ni kufiwa na wazazi wote ili upewe mkopo. Je, sisi wenye wazazi masikini tuwauwe wazazi wetu?

Napingana na wewe katika baadhu ya maeneo;

1.kuhusu kupendelea wanawake (si busara kusema hivo),jamii zetu za kiafrika zilikua na desturi za kuundergrade wanawake,kitu ambacho ni tofauti na haki za binadamu.Kwahiyo affirmative actions kama kuwapa nafasi kwenye sekta za uongozi,elimu,kazini,siasa nk nk ili kupunguza gender discrimination...

2.kuhusu elimu ya juu si vyema kusema kuwa baadhi ya michepuo imeshushwa hadhi, ni kwamba baada ya kuona kuwa kuna uhitaji mkubwa wa wanasayansi,michepuo ya sayansi ilipewa vipaumbele ili kuwapa motisha wanafunzi wasome hayo masomo....

3.kuhusu nikopo,nahisi nchi yetu haina uwezo wa kuwapatia wanafunzi wote hiyi mkopo,so inabidi ichaguo baadhi ya wanafunzi watakaonufaika na hiyo mikopo,,hapa ni hekima zaidi kuwapa wale wenye uhitaji,swali la kujiuliza ni;
Ni vipi utawatambua hao wenye uhitaji mkubwa wa mkopo...??
 
Naheshimu mawazo yako Paparazzi.

Unapowapa nafasi kundi fulani ni dhahiri unawanyima wengine haki hiyo. Kwa hekma yangu sifa za pamoja ndizo zingeamua nani awe nani na nani asomee nini.
Mwanzo ilijulikana kuwa mkopo ni kwa wale wasioweza kujisomesha ila sasa imekuwa kwa waliosomea au wataosomea taaluma fulani. Na sasa tumekwenda mbali na kufikia kuwaona yatima ndio masikini na wenye uhitaji zaidi ya wenye wazazi.
Kuhusu uhaba wa bajeti wewe ndo unasema au serikali imesema? Kwanini wengine wapewe 100% na wengine not secured? Kama mkate ni mdogo kwanini wasingegawa kidogo kidogo?
Kama walijua kuwa badget ni ndogo kwanini walikubali kupokea maombi zaidi ya uwezo wao? Watu walitumia pesa kuomba mikopo wakanyimwa kwamba pesa hakuna, sasa watu waki appeal pesa itatoka wapi?
 
Chukulia mfano;wewe ndio upo pale last say wa heslb;

je ungempa nani mkopo na kumnyima nani,wakati haujui family background ya applicant hata mmoja....

Hapa ndipo utakuta kuna vigezo fulani vinajitokeza kubashiri kua mtu fulani ni muhitaji mkubwa..
*yatima
*aliyesoma shule za serikali nk nk
 
Hakuna sababu ya kubashiri kwani hali ya uchumi wa mtu anaijua mwenyewe. Mpaka anaomba mkopo anautaka. Kwanini wasingetoa 50% kwa wote?
 
Hii ni bodi ya mikopo na sio NGO, ndio maana watu wanakopeshwa na wanakuja lipa na riba.
 
Hakuna sababu ya kubashiri kwani hali ya uchumi wa mtu anaijua mwenyewe. Mpaka anaomba mkopo anautaka. Kwanini wasingetoa 50% kwa wote?


Hebi jiulize,je ni haki kumpa mtoto wa pedeshee 50% na mtoto wa mvuvi nae apewe kiasi hicho hicho....??

Lazima baadhi ya vigezo japo havina accuracy to 100% vitumike ili kuwatenganisha mapedeshee na wavuvi.....
 
Hii ni bodi ya mikopo na sio NGO, ndio maana watu wanakopeshwa na wanakuja lipa na riba.

Hata kama wangekuwa NGO haimaanishi kuwa wanaendeshwa kulingana na wateja wao...

Pia kumbuka kua kila asasi ina sheria,masharti na vigezo...

Kwanza ikumbukwe kuwa,heslb wana kifungu kinachoainosha kuwa kupata mkopo si lazima,maanake nini??
 
Hivi unajisikiliza? Unahakika gani kuwa wafaidika wa mkopo kwa 100% ya mkopo ni watoto masikini?
Hebi jiulize,je ni haki kumpa mtoto wa pedeshee 50% na mtoto wa mvuvi nae apewe kiasi hicho hicho....??

Lazima baadhi ya vigezo japo havina accuracy to 100% vitumike ili kuwatenganisha mapedeshee na wavuvi.....
 
Bodi ipo kwa ajili yetu ndo maana inatumia pesa za kodi zetu kufanya kazi zake. Kila mwaka wanaongezewa pesa ili watuhudumie na utambue uwepo wa bodi ni kuhakikisha watu wanasoma na sio kuwazua watu wasisome. Sasa kusema kuwa wanakipengele kuwa ukikosa ni sahihi hakina mantiki.
Hata kama wangekuwa NGO haimaanishi kuwa wanaendeshwa kulingana na wateja wao...

Pia kumbuka kua kila asasi ina sheria,masharti na vigezo...

Kwanza ikumbukwe kuwa,heslb wana kifungu kinachoainosha kuwa kupata mkopo si lazima,maanake nini??
 
Hivi unajisikiliza? Unahakika gani kuwa wafaidika wa mkopo kwa 100% ya mkopo ni watoto masikini?


Ndio maana nikakwambia ili kumesh out masikini na tajiri,ni busara kuweka vigezo fulani japi havitakuwa na ufasaha wa 100%
 
Bodi ipo kwa ajili yetu ndo maana inatumia pesa za kodi zetu kufanya kazi zake. Kila mwaka wanaongezewa pesa ili watuhudumie na utambue uwepo wa bodi ni kuhakikisha watu wanasoma na sio kuwazua watu wasisome. Sasa kusema kuwa wanakipengele kuwa ukikosa ni sahihi hakina mantiki.


Hukujibu swali langu....
"Kifungu kinachoainisha kuwa kupata mkopo kwa ajili ya elimu ya juu maana yake ni nini??"

Wala sikumaanisha kuwa kukosa mkopo ni haki yako....
 
Chukulia mfano;wewe ndio upo pale last say wa heslb;

je ungempa nani mkopo na kumnyima nani,wakati haujui family background ya applicant hata mmoja....

Hapa ndipo utakuta kuna vigezo fulani vinajitokeza kubashiri kua mtu fulani ni muhitaji mkubwa..
*yatima
*aliyesoma shule za serikali nk nk

Nakuona kama unatetea pasipokuwa na hoja! Wewe ndo mkurugenzi wa mikopo? Basi kama kweli wewe ni mfanyakazi wa hiyo Bodi nachelea kusema akili yenu ndogo! Unapotuuliza tungekuwa wasemaji wa mwisho pale HESLB tungefanyaje, nakuona kama mburula fulani hivi! Hivi unaona kabisa vigezo walivyoweka vinatoa taswira halisi ya wahitaji wakubwa? Basi mimi ningekuwa bodi ningeigawanya fedha iliyopo kidogo kidogo angalau kila mmoja apate japo 70%. Hapa kigezo kingekuwa kupata chuo tu!!
 
Nakuona kama unatetea pasipokuwa na hoja! Wewe ndo mkurugenzi wa mikopo? Basi kama kweli wewe ni mfanyakazi wa hiyo Bodi nachelea kusema akili yenu ndogo! Unapotuuliza tungekuwa wasemaji wa mwisho pale HESLB tungefanyaje, nakuona kama mburula fulani hivi! Hivi unaona kabisa vigezo walivyoweka vinatoa taswira halisi ya wahitaji wakubwa? Basi mimi ningekuwa bodi ningeigawanya fedha iliyopo kidogo kidogo angalau kila mmoja apate japo 70%. Hapa kigezo kingekuwa kupata chuo tu!!


Nahisi umekurupuka ndugu yangu.....

Fuatilia mjadala vizuri then uje na judicious thoughts sio unabwabwaja kama mtoto....

Wewe unadhani kila aliyepata nafasi ya chuo anahitaji huo mkopo....??
Unadhani kila aliyeomba nkopo hana uwezo...??
Fikiria mbali pimbi wa kifikra wewe..
 
Napingana na wewe katika baadhu ya maeneo;

1.kuhusu kupendelea wanawake (si busara kusema hivo),jamii zetu za kiafrika zilikua na desturi za kuundergrade wanawake,kitu ambacho ni tofauti na haki za binadamu.Kwahiyo affirmative actions kama kuwapa nafasi kwenye sekta za uongozi,elimu,kazini,siasa nk nk ili kupunguza gender discrimination...

2.kuhusu elimu ya juu si vyema kusema kuwa baadhi ya michepuo imeshushwa hadhi, ni kwamba baada ya kuona kuwa kuna uhitaji mkubwa wa wanasayansi,michepuo ya sayansi ilipewa vipaumbele ili kuwapa motisha wanafunzi wasome hayo masomo....

3.kuhusu nikopo,nahisi nchi yetu haina uwezo wa kuwapatia wanafunzi wote hiyi mkopo,so inabidi ichaguo baadhi ya wanafunzi watakaonufaika na hiyo mikopo,,hapa ni hekima zaidi kuwapa wale wenye uhitaji,swali la kujiuliza ni;
Ni vipi utawatambua hao wenye uhitaji mkubwa wa mkopo...??
Mi nakupinga vilevile na kaulli zako hasa 2,,,ya kusema si busara kusema kuwa wanawake wanapendelewa,,hilo lipo wazi,,,wengi wao hawana vigezo na ndio maana grade zao zinashuswa,,,,,,kama kweli wanaweza wafight na vidume na washindane ili watoke siyo kuwashushia alama za ufaulu,,,,,kingine unasema coz za sayansi zimepewa vipaumbele,,,vipaumbele vipi hivyo na wakati 2po wengi 2 na 2na vigezo vya kupata hiyo mikopo 2nasoma engineering,,ha2pati hata sh 0,,,,na wanaopata ni wa2 ambao wanapga mabiashara na social sciences coz,,,,,ni hayo 2
 
Mi nakupinga vilevile na kaulli zako hasa 2,,,ya kusema si busara kusema kuwa wanawake wanapendelewa,,hilo lipo wazi,,,wengi wao hawana vigezo na ndio maana grade zao zinashuswa,,,,,,kama kweli wanaweza wafight na vidume na washindane ili watoke siyo kuwashushia alama za ufaulu,,,,,kingine unasema coz za sayansi zimepewa vipaumbele,,,vipaumbele vipi hivyo na wakati 2po wengi 2 na 2na vigezo vya kupata hiyo mikopo 2nasoma engineering,,ha2pati hata sh 0,,,,na wanaopata ni wa2 ambao wanapga mabiashara na social sciences coz,,,,,ni hayo 2

Usiseme kuwa wengi wa wanawake hawana uwezo ndio maana wanashushiwa vigezo,hapo nyuma kidogo wanawake walikua wanasoma katika mazingira magumu sana ukilinganisha na wanaume,jamii nyingi haikupenda kuandaa mazingira mazuri kwa mtoto wakike kusoma na kufaulu,hivyo ufaulu wao ukawa mdogo,ili kuneutralize hii hali selikali ikashusha vigezo vya kuingia mashuleni na vyuoni kwa wanawake...

Pole sana ndugu yangu kwa kukosa mkopo wakati unachukua uhandisi... yawezekana info zako zinawaridhisha heslb kukunyima,laa sivyo jaribu kuappeal wakitoa hiyo chance,naamini kama una vigezo vya kupewa huo mkopo utapata...
 
Kuomba kuna mawili,kupata au kukosa,bodi haikusema kuwa wanafunzi wote walioomba watanufaika na mkopo,na kama mnakumbuka mwisho wa kujaza chaguzi za kozi na vyuo kuna sehemu ilitakiwa ukubali kuwa mkopo si guaranteed,na hata hizo priority course waliandika kiasi unachoweza kusaidiwa endapo utafanikiwa kupata mkopo,kwahyo kama hujapata mkopo ujue kuna mwingine kapata,c lazima wewe upate hata kama una vigezo kwa maana wapo wenye vigezo zaidi yako ndio maana wamepata na tatizo inginre msijiamini sana,inaonyesha mnajipaga mkopo kabla bodi hawajatoa majina,siku waki release majina mkiwa hampo ndio mnaanza kulalamika,hapo mlishapanga bajeti kbs,
Poleni sana
 
Dada yangu nimejifunza mambo kadhaa kutokana na coment yako.
1. Dharau na kiburi cha kike.
2. Kutoelewa dhamira ya kuanzishwa bodi ya mikopo. Tambua kuwa kuwepo kwa bodi ya mikopo ni umasikini wa watz. Tungekuwa tunaweza kujisomesha kusingekuwepo heslb.
3. Kutojua kuwa bodi haipo kwa ajili ya kuwanyima watu mikopo. Ndio maana vigezo vikawekwa.
4. Una ubinafsi kiasi cha kutoumizwa na yanayowakuta wenzako. Nachokiona ni kashfa kwa waliokosa.

N.B. Kama bodi imeishiwa pesa kwa watao appeal watazitoa wapi?
Kuomba kuna mawili,kupata au kukosa,bodi haikusema kuwa wanafunzi wote walioomba watanufaika na mkopo,na kama mnakumbuka mwisho wa kujaza chaguzi za kozi na vyuo kuna sehemu ilitakiwa ukubali kuwa mkopo si guaranteed,na hata hizo priority course waliandika kiasi unachoweza kusaidiwa endapo utafanikiwa kupata mkopo,kwahyo kama hujapata mkopo ujue kuna mwingine kapata,c lazima wewe upate hata kama una vigezo kwa maana wapo wenye vigezo zaidi yako ndio maana wamepata na tatizo inginre msijiamini sana,inaonyesha mnajipaga mkopo kabla bodi hawajatoa majina,siku waki release majina mkiwa hampo ndio mnaanza kulalamika,hapo mlishapanga bajeti kbs,
Poleni sana
 
Hili suala la mkopo inabidi kulifikiria mara kwa mara, ikiwa hivi sasa unaona kunaugumu wa kupata mkopo basi jiulize,
1: Mtoto wako umemuandalia mazingira gani kielimu?
2: Utaweza kumsomesha mtoto wako bila kutegemea mkopo hapo baadae?
3: Idadi hiyo ya watoto unaofikiria kuwazaa je utamudu kuwahudumia kielimu?

Jipange kijana mwenzangu kwaajili ya maisha ya watoto wako.
 
tatizo nchi yetu ina vitu vingi unwanted..kama mbio za mwenge, sherehe za uhuru wa bendera nk. kutokana na uhuru wa bendera tunashindwa kuwasomesha watu kiuhakika ili watuletee uhuru halisi... sidhani kama kuna mtoto wa tajiri anayesoma nchini. Tukiacha hizo kitu za kupoteza kodi ya mwananchi. Mi naona bado hatujaona umunimu sahihi wa elimu...wala tusingekubali wasomi wetu waende kusoma kwa stress, mtu anawaza jinsi ya kulipa ada na kula..matokeo yake kudisco au kusap..mnasema hana akili kumbe kulikuwa na sababu nyingi. Serikali iliangalie hili swala kwa macho hata ya jirani
 
Back
Top Bottom