Tunayo ya kujifunza kwa Raila, baba wa demokrasia Kenya

Tunayo ya kujifunza kwa Raila, baba wa demokrasia Kenya

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Kenya ni taifa katika mazingira halisi tuliyomo sisi. Hata hivyo taifa hili limepiga hatua kubwa sana kidemokrasia zenye kustahili kupigiwa mfano.

Hizi tantarira za eti kuwa IEBC ni sawa tu na NEC yetu, kwamba ya Kenya tuwaachie wakenya wenyewe, nk nk, zote ni kelele za vyura tu. Nia na madhumuni kutupoteza maboya tuache kuzichambua mbivu za wenzetu dhidi ya mbichi zao.

Haipo shaka kuwa ukaribu usiokuwa na afya baina ya Raila na shujaa wetu, ulimweka Raila kwenye upande dhoofu wa historia ya wapigania haki. Hata hivyo weka mahusiano hayo binafsi na jiwe pembeni, huyu bwana ni jembe haswa na demokrasia ya Kenya inayo mengi ya kumkumbuka nayo.

Kwa hakika wandugu kama ni kwa dhati tunataka haki, demokrasia au katiba mpya? Baba anayo majibu na anayo njia inayoweza kutufaa:

IMG_20220916_133341_267.jpg

Raila anaongelea watu milioni moja kuifanyaia mageuzi mahakama kwa anachoamini moyoni kuwa hakipo sawa.

Kwani kwetu, kuna hata aliyewahi kutamka anahitaji watu wangapi Ili kufanya nini? Kwani agenda yetu ni nini basi?

Au kwetu sisi ni uwoga (playing it safe) na kutegeana (opportunism)?

"Woga kuchelea kulipa gharama zozote au kutegeana yaani kuwa mkao wa kifursa zaidi Ili kujilia matunda yakipatikana kwa gharama za wengine, kiulaini?"

Tunataka katiba mpya. Iko wapi roadmap ya kufanikisha tunayafikia malengo yetu?

Tupende au tusipende, Baba anaweza kuwa wa msaada kwetu pia.

Source: Raila, Rigathi in surprise meeting
 
Mahela umfuate Jiwe
Mahela haondoki kumfuata jiwe kwa kumwambia hivi mtandaoni.

Raila anasema anahitaji watu milioni 1 kumfanya Mahela na wapambe wake kufanya kinachotakiwa.

Tunayo ya kujifunza kumpeleka Mahela kwenda alikopeleka mboga.
 
Huwa naona tumeshapata masomo mengi sana, sijui lini tutaanza kujifunza, au kama tumejifunza basi hatuelewi.

Tumekuwa kama wanafunzi wanaohudhuria masomo kila siku, lakini kila wakipewa mitihani wanafeli, naona tuendelee tu kuishi kwa matumaini.
 
Huwa naona tumeshapata masomo mengi sana, sijui lini tutaanza kujifunza, au kama tumejifunza basi hatuelewi.

Tumekuwa kama wanafunzi wanaohudhuria masomo kila siku, lakini kila wakipewa mitihani wanafeli, naona tuendelee tu kuishi kwa matumaini.

Nini tunataka - kinafahamika.
Namna gani kinapatikana - inafahamika.

"Hakuna haja ya kumung'unya maneno. Tatizo letu zaidi ni uongozi."

Wengi wa viongozi wetu ñi dhaifu. Wengi wao na baadhi yetu wafuasi (kama walivyo member wengine wengi hapa JF) ni waoga na opportunists wakutupwa wenye kuweza kujaribu kuvikimbia hadi vivuli vyao. Hata kutoa mawazo tu wanaogopa.

Pana haja ya kuwapa makavu watu hawa.

Kwa hakika wao ni mzigo kuliko hata malumumba.
 
Kenya ni taifa katika mazingira halisi tuliyomo sisi. Hata hivyo taifa hili limepiga hatua kubwa sana kidemokrasia zenye kustahili kupigiwa mfano.

Hizi tantarira za eti kuwa IEBC ni sawa tu na NEC yetu, kwamba ya Kenya tuwaachie wakenya wenyewe, nk nk, zote ni kelele za vyura tu. Nia na madhumuni kutupoteza maboya tuache kuzichambua mbivu za wenzetu dhidi ya mbichi zao.

Haipo shaka kuwa ukaribu usiokuwa na afya baina ya Raila na shujaa wetu, ulimweka Raila kwenye upande dhoofu wa historia ya wapigania haki. Hata hivyo weka mahusiano hayo binafsi na jiwe pembeni, huyu bwana ni jembe haswa na demokrasia ya Kenya inayo mengi ya kumkumbuka nayo.

Kwa hakika wandugu kama ni kwa dhati tunataka haki, demokrasia au katiba mpya? Baba anayo majibu na anayo njia inayoweza kutufaa:

View attachment 2358674
Raila anaongelea watu milioni moja kuifanyaia mageuzi mahakama kwa anachoamini moyoni kuwa hakipo sawa.

Kwani kwetu, kuna hata aliyewahi kutamka anahitaji watu wangapi Ili kufanya nini? Kwani agenda yetu ni nini basi?

Au kwetu sisi ni uwoga (playing it safe) na kutegeana (opportunism)?

"Woga kuchelea kulipa gharama zozote au kutegeana yaani kuwa mkao wa kifursa zaidi Ili kujilia matunda yakipatikana kwa gharama za wengine, kiulaini?"

Tunataka katiba mpya. Iko wapi roadmap ya kufanikisha tunayafikia malengo yetu?

Tupende au tusipende, Baba anaweza kuwa wa msaada kwetu pia.

Source: Raila, Rigathi in surprise meeting
Railq hana ubavu ww kuondoa majaji wa mahakama. Raila yeye ni nani mpaka awe muamuzi wa wakenya milioni 40? Wakenya wamemkataa kupitia sanduku la kura hata afanyeje hawezi kupata urais wa mezani kwenye sahani, njia pekee ya kupata urais Kenya ni kuwakabili wapiga kura na kuwaridhisha kwa sera ndio wakuchague. Na safari hii Rais Ruto ameishasema wazi hakuna handshake.

Mfumo wa kuteua na kuondoa majaji Kenya uko vizuri na independent na umewekwa na katiba ya. Kemyo yeye Raila alishiriki kuitengeneza. Hivyo hakuna jaji atakayejiuzuru kwa vigezo vya Raila. Hao watu milioni moja sio ndio wakenya wote.

Tatizo kubwa la Raila anafikiri heye ndiye nwenye haki siku zote ya kuwaamulia wakenya. Jinsi siku zinavyoenda ndivyo wakenya wanavyozidi kumfahamu vizuri jinsi ambavyo hafai.

Kana alidhani kuwa, kabla hajafa kazima aweke rekodi ya kuwa rais wa Kenya basi afahamu kuwa kamwe urais haupati ng'o.
 
Back
Top Bottom