Tundaman, Chegge na Ferouz sio wasanii kabisa

Tozi na wewe kumbe hujui muziki
Juvenile mimi sijui mziki lakini Chegge anajua. Angalia ame featuring na waimbaji kama Diamonds, Malaika, Chikuze,Runtown, Uhuru Sweet, Norah, Temba, Dully Sykes na wengine wengi tu nitajie huyo unae muona muimbaji wako mzuri na featuring yake ziweke hapa.
 
Achana na huyu bwege hajui mziki ye anafikiri ladha ya mziki anaoutaka yeye ndo iko sahihi, anasahau kuwa kila mtu ana ladha yake, ye kama anajiskia raha kusikiliza nyimbo za makashikashi na kufokafoka asitutaabishe sisi tunaopenda za kukubembeleza.

Angejua hakuna msanii ananikonga nyoyo kama Chegge asingeongea hayo madudu yake.
Huyu dogo bado hajakua hajua mziki ni nini anakurupuka.
 
Samahani sana wanajamvi wale nitakao wakwaza.....

Sijawahi kupenda uimbaji wa chege hata kwa bahati mbaya na wala huwa sijui anaimbaga kitu gani. huwa najitahidi kumsikiliza lkn sijawahi kuelewa kabisa anaimba nini na kwa lugha gani. Sema huwa anabebwa sana na kolabo za muheshimiwa temba.

Pia kuna wengine wanaopenda kuimba lkn muziki unawakimbia sana tu - junia, sechu (hasira=hasara uko poa) yule mngine wa banji, wale wawili wa mapacha wa3...orodha ni ndefu sana
 
Wewe ndio kipimo cha mtu anajua au hajui kuimba?kwanza muziki huujui unaropoka ropoka tu au unafikiri kila mtu akili yake kama yako ya kushikiwa
 
We sijui umeanza kumsikiliza Chegge miaka ya hiv karibuni maana ana ngoma za miaSio lazima umpende mkuu, we tambua kila mtu ana test yake, kwa mfano mi huwezi kunisikilizisha regge ingawaje najua unaujumbe matata sana.
All in all Muzic is about ones feelings na hakuna formula..
 
Chege ndo sijawahi vutiwa na nyimbo ambazo ameimba bila kolabo.
Namuonaga chenga tu
 
Temba ndio hamna kitu.Anaongeaga Tu.Hussein machozi nae kulialia Tu.
 
Ferooz? unahangaikiwa ww cio bure
 
hivi we jamaa uliyefungua huu uzi unajua mziki au unatumia uhuru wako ipasavyo.unajua maana ya /uniqueness of the artist/au umekurupuka.unamjua ferooz ama ndo kizazi cha diamond. Chegge.ahah kweli unafurahisha..fuatilia kwanza kabla ya kuongea.ukija na hoja ntakuwekea hoja vile vile.
 
Nitajie wimbo wa ferooz au chege au tundaman ambao hawajalialia?
 
Oanisha hii hoja yako na nyimbo ulizotajiwa kisha jitafakari unless kama hizo nyimbo huzifahamu!
  • Starehe
  • Boss
  • Barua
  • Kamanda
NOTE: Usihadaike na majina ya hizo nyimbo bali content yake!
Mkuu hiki kizazi cha Lik Kiba na Diamond hakielewi nyimbo hizi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…