SI KWELI Tundu Lissu ametangaza nia ya kugombea Urais 2025

SI KWELI Tundu Lissu ametangaza nia ya kugombea Urais 2025

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Source #1
View Source #1
Source #2
View Source #2
Wakuu kuna hii inasambaa Twitter je, ni ya kweli?
SIKWELI_LISSU_URAIS_25_16FEB25.jpg
 
Tunachokijua
Tundu Lissu ni mwenyekiti wa Chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) na amekuwa mwenyekiti wa chama hicho kuanzia mwaka huu 2025, hivi karibuni amekuwa na ziara nyumbani kwao Ikungi Singida. Safari hiyo imekuwa ni ya kwanza kuanzia alipopata nafasi ya kuwa mwenyekiti wa chama hiko.

Madai

Kumekuwepo na grafiki inayoonekana kufanana na ya Millard Ayo inayosambaa ikionesha kuwa Tundu Lissu rasmi ametangaza nia ya kugombea Urais mwaka 2025, alipokuwa Ikungi Singida, Tazama hapa na hapa

Uhalisia wa taarifa hiyo

JamiiCheck imefuatilia madai hayo na kubaini kuwa Taarifa hiyo si ya kweli. Lissu alipokuwa Ikungi Singida. Ufuatiliaji wa kimtandao kwa kuangalia hotuba alizozitoa Lissu alipokuwa mkoani Singida umebaini kuwa hakuna mahali ambapo Lissu alisema atagombea urasi mwaka huu.

Lissu alipokuwa Ikungi, Singida alipokelewa na wananchi ambapo alizungumza nao, licha ya mambo mengine Lissu alizungumzia kuhusu changamoto za uchaguzi zilizojitokeza mwaka 2019, 2020 na 2024. Katika hotuba yake hiyo aliyoitoa Febuari 15, 2025 alisema kuwa uchaguzi umekuwa na madhaifu mengi ikiwemo wizi wa kura na mambo mengine mengi ambapo alisema watajtahidi wazuie uchaguzi unaotarajiwa kufanyika baadaye mwaka huu 2025, tazama hapa.

Aidha hotuba ya pili aliitoa alipopokelewa kijijni kwao kwa ajili ya maombi ambapo pia alitumia nafasi hiyo kuwakaribisha wanachama katika eneo hilo ambalo ndipo nyubani kwao alipozaliwa na kukulia na hakuzungumzia pia kuhusu nia ya kugombea nafasi ya Urais, tazama hapa.

Ufuatiliaji wa kimtandao pia umebaini grafiki hiyo pamoja na taarifa hiyo haikuchapishwa katika kurasa rasmi za mitandao ya kijamii ya Millard Ayo.
Si kweli. Huyo Sally Brown ni chawa kama alivyo Lucas. Hao wote ni watu wa propaganda
 
Mbona alishatangaza nia hata kabla ya kuchaguliwa kuwa mwenyekiti!
 
Wakuu kuna hii inasambaa Twitter je, ni ya kweli?
View attachment 3239266
Iwe Lissu ametangaza nia ya kugombea Urais katika Uchaguzi wa 2025, au hapana, hoja ya kujadili ni kuhusu lengo anataka madaraka ya Urais kwa maslahi yake binafsi, au kwa maslahi ya Wananchi? Kama anataka kuwania nafasi hiyo ya Rais wa Jamhuri ya Tanzania, atakuwa anahitaji ukubwa kwa maslahi yake binafsi. Ili aonekana kuwa anahitaji madaraka kwa nia njema ya kusimamia maslahi ya wananchi, sharti kwanza asimamie upatikanaji wa Katiba Mpya. Sasa hivi, kwa Katiba Iliyopo, anayeitwa Rais wa Muungano, ana madaraka ya utendaji katika mipaka ya Tanganyika. Hii ina maana kwamba Serikali chini ya Katiba iliyopo si Serikali ya Muungano kwa sababu Zanzibar ina Serikali yake ambayo inasimamia na kuongoza raslimali zote za Zanzibar. Lakini Tanganyika haina Serikali yake hivyo raslimal zake zinahesabika kuwa na raslimali za umiliki wa pamoja kati ya Tanganyika na Zanzibar. Hii siyo haki kwa Wananchi wa Tanganyika, na inaondoa dhana ya utawala wa haki na demokrasia. Kwa hiyo yeyote anayedai kugombea Urais kwa maslahi ya Wananchi, na hasa Wananchi wa Tanganyika, sharti kwanza azuie uchaguzi wa 2025 usimamishwe, adai Rasmu ya Katiba Mpya, ambayo inaipa Tanganyika haki sawa na Zanzibar ya kuwa na Serikali yake, kama ilivyo kwa Zanzibar.
 
Back
Top Bottom