Hawezi kwasababu gani wakati bado hajapata nafasi yakuongoza.Hakuna sababu yakukudanganya wakati ni kiasi cha wewe kutoka usingizini nakuamua kushughulisha kichwa chako kuona je anayoyasema lissu yanawezekana na kama yanawezekana How?.kudangwa wachwa anidanganywe lakini siwez kumpinga na kumkataa kabisa utaratibu huu tunaishi nao kwa sasa naona ni bora kuliko na hata mpinzani huyu lissu hawez fanya hata robo haya aliyo yafanya maguli,
Kumsikiliza Lissu inabidi uvute bangi kwanza; tena lile ambalo halijakauka sana. Aliweka pingamizi kwa Magufuli na Lipumba kuwa hawakujaza fomu vizuri hivyo hawaruhusiwi kugombea uraisi, baadaye akasema wagombea ubunge wa CHADEMA na ACT ambso wameeungliwa kwa kutojaza fomu vizuri walitakiwa wasaidie na tume kujaza fomu hizo wasienguliew.CHADEMA kupitia Mgombea Urais wao ametamka kujenga masoko yatakayofanya kazi nyakati za usiku.
Namnukuu Lissu “Tutajenga majengo makubwa kwa ajili ya Wamachinga ili wafanye biashara kwa uhuru na sio kuwapa vitambulisho halafu wafanyie biashara kwenye mitaro ambako mvua inakuwa yao na jua linakuwa lao” -Tundu Lissu akiwa Mbeya
“Kwenye stendi za Mabasi tutajenga majengo ambayo Mama Lishe watauza vyakula, tunataka kuwa na masoko ambayo yatakuwa yanafanya kazi usiku kucha ili Mtu yeyote ambaye atakuwa amechelewa kufika kwenye mji husika apate huduma”-Lissu
Hoja kuu hapa ni kujenga masoko, watu kufanya biashara nyakati za usiku na vitambulisho vya wajasiliamali.
Lissu huyu anayesema kila siku maendeleo ni Watu na sio vitu, leo hii huyo huyo Lissu anasema atajenga masoko. Iko wapi hoja yake aliyosema maendeleo ya Watu na sio vitu? Ama soko ni Watu na sio kitu tena?
Huyo huyo Lissu na wenzake wanaosema wakiingia ikulu watauza ndege zote za nchi zilizonunuliwa na Rais Magufuli ndio hao hao wanatumia usafiri wa ndege kuzunguka mikoani. Au wanazopanda sio ndege ni mitumbwi?
Lissu huyu huyu anayepinga ujenzi wa umeme wa Mto Rufiji utakaozalisha megawatts 2115 kuwa unalifilisi Taifa, leo hii anasema atahakikisha Wajasiliamali wanafanya biashara hadi usiku. Anapinga ujenzi wa umeme wa uhakika anataka hao Wajasiliamali wafanye biashara gizani?
Alivyokuwa mkurupukaji Lissu anazungumzia vitambulisho vya Wajasiliamali kuwa havina tija kwa Wamachinga na Wajasiliamali. Lahaula!
Inawezekana "dish" limeyumba hajui kuwa hajui vitambulisho hivyo ni mkombozi kwa Wamachinga na Wajasiliamali wote wadogo. Mmachinga, Mama Lishe hapo awali walikuwa kwenye misukosuko mikubwa na Mgambo kutokana na suala la ulipaji ushuru waliokuwa wakitozwa kila siku ambapo walikuwa wakilipia ushuru wa Tsh. 500/- ama Tsh. 1,000/- kwa siku.
Leo hii badala ya kulipa Tsh. 180,000/- ama Tsh. 365,000/- kwa mwaka leo hii wanalipa Tsh. Elfu ishirini tu (20,000/-). Wanaokoa Tsh. 160,000/- na wengine wanaokoa Tsh. 345,000/- pamoja na bidhaa zao. Lissu atasemaje vitambulisho havina tija?
Inawezekana Lissu anapajua zaidi Ubelgiji kuliko Tanzania, nimkumbushe Tanzania kuna masoko kwa ajili ya Wamachinga yapo mfano hai ni soko la Machinga Complex lililopo Karume wilaya ya Ilala mkoani Dar es Salaam.
Si hayo tu bali pia Rais Magufuli amejenga stendi mpya nyingi tu ikiwemo ya Mpanda Katavi, Morogoro, Dodoma nk na kote huko kuna majengo ya Wajasiliamali wote wakiwemo Mama Lishe.
Lissu aache kujikoroga, aelewe hizi sio zama za drama, siasa za uongo kwani Watanzania wa sasa ni waelewa sana wanajua mbivu na mbichi, hawalishwi matango pori!!
*Shilatu E.J*
ww mpka sasa umeshakamilsha mangapi amabayo umeyapanga /me naona unabishana na upepo mkuu kama ww leo huona magufli kafanya nn bas hutoweza kuona la mwingine yoyote yule atakae kuja kuongoza nchi hii
mkuu kwa sera gani za lissu kubinafsisha mali za uma yan turud kwa mkapa tukilo toka.Hawezi kwasababu gani wakati bado hajapata nafasi yakuongoza.Hakuna sababu yakukudanganya wakati ni kiasi cha wewe kutoka usingizini nakuamua kushughulisha kichwa chako kuona je anayoyasema lissu yanawezekana na kama yanawezekana How?.
Lissu ANAWEWESEKA anavyopenda mtandao Sasa Atakuwa Anaweweseka na NYOMI LA MWANZAA MAANA KUMETAPIKA HUKUCHADEMA kupitia Mgombea Urais wao ametamka kujenga masoko yatakayofanya kazi nyakati za usiku.
Namnukuu Lissu “Tutajenga majengo makubwa kwa ajili ya Wamachinga ili wafanye biashara kwa uhuru na sio kuwapa vitambulisho halafu wafanyie biashara kwenye mitaro ambako mvua inakuwa yao na jua linakuwa lao” -Tundu Lissu akiwa Mbeya
“Kwenye stendi za Mabasi tutajenga majengo ambayo Mama Lishe watauza vyakula, tunataka kuwa na masoko ambayo yatakuwa yanafanya kazi usiku kucha ili Mtu yeyote ambaye atakuwa amechelewa kufika kwenye mji husika apate huduma”-Lissu
Hoja kuu hapa ni kujenga masoko, watu kufanya biashara nyakati za usiku na vitambulisho vya wajasiliamali.
Lissu huyu anayesema kila siku maendeleo ni Watu na sio vitu, leo hii huyo huyo Lissu anasema atajenga masoko. Iko wapi hoja yake aliyosema maendeleo ya Watu na sio vitu? Ama soko ni Watu na sio kitu tena?
Huyo huyo Lissu na wenzake wanaosema wakiingia ikulu watauza ndege zote za nchi zilizonunuliwa na Rais Magufuli ndio hao hao wanatumia usafiri wa ndege kuzunguka mikoani. Au wanazopanda sio ndege ni mitumbwi?
Lissu huyu huyu anayepinga ujenzi wa umeme wa Mto Rufiji utakaozalisha megawatts 2115 kuwa unalifilisi Taifa, leo hii anasema atahakikisha Wajasiliamali wanafanya biashara hadi usiku. Anapinga ujenzi wa umeme wa uhakika anataka hao Wajasiliamali wafanye biashara gizani?
Alivyokuwa mkurupukaji Lissu anazungumzia vitambulisho vya Wajasiliamali kuwa havina tija kwa Wamachinga na Wajasiliamali. Lahaula!
Inawezekana "dish" limeyumba hajui kuwa hajui vitambulisho hivyo ni mkombozi kwa Wamachinga na Wajasiliamali wote wadogo. Mmachinga, Mama Lishe hapo awali walikuwa kwenye misukosuko mikubwa na Mgambo kutokana na suala la ulipaji ushuru waliokuwa wakitozwa kila siku ambapo walikuwa wakilipia ushuru wa Tsh. 500/- ama Tsh. 1,000/- kwa siku.
Leo hii badala ya kulipa Tsh. 180,000/- ama Tsh. 365,000/- kwa mwaka leo hii wanalipa Tsh. Elfu ishirini tu (20,000/-). Wanaokoa Tsh. 160,000/- na wengine wanaokoa Tsh. 345,000/- pamoja na bidhaa zao. Lissu atasemaje vitambulisho havina tija?
Inawezekana Lissu anapajua zaidi Ubelgiji kuliko Tanzania, nimkumbushe Tanzania kuna masoko kwa ajili ya Wamachinga yapo mfano hai ni soko la Machinga Complex lililopo Karume wilaya ya Ilala mkoani Dar es Salaam.
Si hayo tu bali pia Rais Magufuli amejenga stendi mpya nyingi tu ikiwemo ya Mpanda Katavi, Morogoro, Dodoma nk na kote huko kuna majengo ya Wajasiliamali wote wakiwemo Mama Lishe.
Lissu aache kujikoroga, aelewe hizi sio zama za drama, siasa za uongo kwani Watanzania wa sasa ni waelewa sana wanajua mbivu na mbichi, hawalishwi matango pori!!
*Shilatu E.J*
Hata miundombinu yenyewe iko wapi? Kila mradi aliouanzisha hajamaliza.Lissu anasema maendeleo ya vitu na watu viende pamoja. Awamu zote tulishuhudia miundombinu ikijengwa, mishahara ikipanda, ajira zikitoka, fao la kujitoa mifuko ya jamii liilikuwepo, biashara zinafanyika. Lakini kwa JPM kila kitu kime switch off isipokuwa miundombinu
Magufuli kafanya vitu vya kawaida ambavyo kila Rais alifanya kwa nafasi yake. Worse enough huyu Magufuli pamoja na yote amevuruga uchumi, wananchi wamekuwa maskini kuliko miaka 25 iliyopita. Usimuamulie Tundu Lissu kwa kuwa hajawahi kuwa Raiskudangwa wachwa anidanganywe lakini siwez kumpinga na kumkataa kabisa utaratibu huu tunaishi nao kwa sasa naona ni bora kuliko na hata mpinzani huyu lissu hawez fanya hata robo haya aliyo yafanya maguli,
imeiuliza vyema hiyo green guard.Ni asilimia ngapi ya watanzania wanaaccess na masoko kulinganisha na asilimia ya watanzania wenye access na usafiri wa ndege
Hawajuwi wachagaMkuu Lissu anatumiwa na chama chake kwa nia ya kuongeza majimbo ili ruzuku iwe nene miaka mitano ijayo.
Mwenye kumtumia siku akifanikiwa kukipata akitakacho kutazuka mtafaruku mkubwa. Ni siasa zile zile za malengo yaliyojificha.