Uchaguzi 2020 Tundu Lissu atashindwa uchaguzi kwasababu anahubiri utengano badala ya Umoja

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu atashindwa uchaguzi kwasababu anahubiri utengano badala ya Umoja

Benson Mramba

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2013
Posts
648
Reaction score
1,485
Lissu na Mbowe mara kadhaa nimewasikia wanamshambulia Mbatia na NCCR hadharani. Pia jana nimemsikia Mbowe akiwaita wabunge waliohamia NCCR kutoka CHADEMA kuwa ni wasaliti.

Pia Lissu anawaita wanaCCM wote MaCCM sasa kauli hizi za kiubaguzi zinawaunganisha wanaobaguliwa kuliko kuwagawa. Nyerere alisema bila Muungano hakuna Watanganyika wala Wazanzibar.

Wazanzibar ni wamoja sasa hivi kwasababu kuna watanganyika ndani ya Muungano. Muungano ukivunjika hakuna watanganyika bali kuna makabila mbalimbali pia hakuna wazanzibari bali kuna waunguja na wapemba.

Sasa kama Lissu anataka Urais agenda yake namba moja ilipaswa kuwa kuwaunganisha watanzania na kutokuwabagua ili aweze kupata kura za wanaCCM, WanaNCCR n.k wenye msimamo wa wastani lakini kwa ubaguzi wake huu na chama chake ni ngumu kupata kura za wanachama wa vyama vingine. Ila kama wanatafuta kura nyingi kwa ajili ya ruzuku au kupata wabunge wengi kwa ajili ya kambi ya upinzani basi waendelee na ubaguzi huo. Lissu usirithi maadui wa Mbowe hawakuhusu.

Lowassa pamoja nguvu zake alisimamia agenda ya kuunganisha watu wa vyama vyote na makundi mbalimbali hapa nchini ndio maana kila mtu alijiona sehemu ya Lowassa.

Sasa ili kushinda Urais unapaswa kuunganisha makundi mbalimbali. Lissu anahitaji kura za Vunjo za watu wanaoiunga mkono NCCR Mageuzi na Mbatia. Halikadhalika Moshi vijijini, Rombo na maeneo mengine.

Lissu abadili kauli na mindset yake. Kitabu cha Dr. Slaa kinanukuu kauli ya Lissu wakati wa kumpokea Lowassa CHADEMA wakati ule 2015 kuwa " Hata kama watalazimika kushirikiana na shetani ili kuitoa CCM madarakani watafanya hivyo" Je NCCR, CHAUMMA, CCM, NGO,CSO ni mbaya kuliko shetani? Je Lissu hawahitaji hawa kwa ajili yake?

Sasa endeleeni kulewa na nyomi la watu elfu 10 uwanjani kwenye jimbo lenye wapiga kura laki 2 na ushee halafu mje kulia mmeibiwa.

Lema mwenyewe haamini kama Lissu atashinda Urais kadhalika kikundi chake ambacho ni Mbowe, Regy, Mrema n.k sasa Lissu acha usifungue macho wakati wenzio walimtaka Nyalandu
 
Wewe mwenyewe msaliti, kwa hiyo lazima utete wasaliti wenzio.......pambaneni na hali yenu huko mliko?
 
chadema itaidhinisha maendeleo kwa majimbo yote, yule anayesema hatapeleka maendereo kwa majimbo ya wapinzani ndio mbaguzi
 
We ulisikia wapi hizo habari kuwa Lissu anatengeneza utengano au Lema kaona Lissu hawezi shinda we ulisikia wapi
IMG_20200930_091356.jpg
 
Kweli nyani haoni kundule!Huyo anayewatisha wananchi wakichagua upinzani hapeleki maendeleo naye anatuunganisha wananchi?shame
 
Kupeleka uwanja wa ndege chato ni umoja?
Kuwapa nafac za juu familia ni umoja?
Kutopeleka maendeleo maeneo ya wapinzani ni umoja?
Kuzuia nyumba zisivunjwe coz wao walikupa kura ni umoja??
 
Mi nikajua yule Magufili Dikteta ichwara anayesema msipo wachagua wangombea wa CCM sileti maendeleo ndio anahubiri utengano?.

Ama yule anayetaka aonyeshwe kila kituo cha habari na kuandikwa kwenye media zote ndio analeta utengano.

Ushindwe na ulegee.
 
MAGUFULI atashinda uchaguzi kwakuwa Tume ya Uchaguzi kaiteua yeye.
Mkuu wa Polisi kamteua yeye
Mkuu wa majeshi kamteua yeye
Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa kamteua yeye na wote wanna report kwake.
Tundu Lissu atashindwa uchaguzi huu kwasababu hauko huru, wazi na haki
 
Kamasy wewe magufuli anayetulazimisha tuwachague ccm tusipowachagua tutajuta yeye hapo kuhubiri umoja au ujinga wako ndio unakusumbua??
 
Anayegawa wananchi ni yule anayesema ukichagua mpinzani utaishi miaka 5 ya maumivu.
 
Wewe pamoja na kujikomba kwa madhalimu wa CCM wamekukataa, ile tuhuma ya kukwapua hela Chadema ukichanganya na kabila lako halikubaliki huko CCM hupati kitu.Jikite tu kwenye biashara yako ya mama lishe na bar bubu achana na Chadema kabisa.
 
Back
Top Bottom