Hehehe kaka tungekua tuna haja ya kuleta habari mbaya kuhusu Tanzania huku tungejaza server kwenye Kenyan news. Matukio yenu huko huwa nayaona na kupita kimya maana hayatuhusu, ukiona taarifa yoyote imeletwa huku kuhusu Tanzania, ujue ina umuhimu fulani kwa Wakenya na inatuhabarisha kitu fulani.
kama hili lenu la mabomu kwenye ofisi za mawakili lina umuhimu mkubwa kwa Wakenya, inatuhabarisha umuhimu wa kulinda demokrasia yetu na uhuru wa kukosoa na maoni, tunafaa kulinda kwa nguvu zote maana mabomu kwetu ni shughuli ya mashababi bin shetwan, lakini hiyo yenu kwa jinsi anaeleza huyo Tundu Lissu inatia wasiwasi mkubwa aisei. Sio kabisa, tena mlifaa kuilani nyote bila kuzingatia uchama kama mnavyofanya kwenye mitandao.
Nyie ndio mna hulka ya kupenda kutuletea vitaarifa kuhusu Tanzania, mara sijui satellite city Kawe, vitu ambavyo Kenya tunavyo hadi vimetuboa, mara eti Tanzania SGR taking shape wakati mnachotuletea ni hotuba za press conference kuhusu huo mradi baada ya kuchimba chimba hatua 500m, wakati sisi treni za SGR zinachana mbuga hata tushazisahau. Halafu kawaida wewe huwa upo wa kwanza kusifia na kwa taarifa yako wapo Watanzania wengi hulalamika kwanini mnazileta kwenye Kenyan news, ni vile huwa umefumba macho hutaki kuwajibu.