Pre GE2025 Sophia Simba: Wanawake waliokaa muda mrefu kwenye Viti Maalum waachie nafasi kwa vijana

Pre GE2025 Sophia Simba: Wanawake waliokaa muda mrefu kwenye Viti Maalum waachie nafasi kwa vijana

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Mwanasiasa na Waziri Mstaafu, Sophia Simba, amesema ni wakati muafaka kwa wanawake waliokaa muda mrefu kupitia Viti Maalum Bungeni kuwaachia nafasi vijana ili kuendeleza harakati za uwezeshaji wa wanawake katika siasa.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Ijumaa Februari 28, 2025, kwenye kongamano la kuadhimisha miaka 15 ya Taasisi ya ULINGO na miaka 30 ya Azimio la Beijing, Sophia Simba ameeleza kuwa Taasisi ya ULINGO, ambayo imefikisha miaka 15 tangu kuanzishwa kwake, imekuwa chachu kubwa ya kuwainua wanawake katika siasa bila kujali vyama vyao.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Soma Pia: Kipindi hiki cha Uchaguzi wanawake wanapata nafasi ya kutosha kushiriki kwenye masuala ya uchaguzi?


“ULINGO imekuwa na mafanikio makubwa. Tumeona wanawake wengi wakiwa wabunge, madiwani na hata vijijini akina mama wanajitokeza kugombea nafasi mbalimbali,” alisema Sophia Simba.

 
Mwanasiasa na Waziri Mstaafu, Sophia Simba, amesema ni wakati muafaka kwa wanawake waliokaa muda mrefu kupitia Viti Maalum Bungeni kuwaachia nafasi vijana ili kuendeleza harakati za uwezeshaji wa wanawake katika siasa.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Ijumaa Februari 28, 2025, kwenye kongamano la kuadhimisha miaka 15 ya Taasisi ya ULINGO na miaka 30 ya Azimio la Beijing, Sophia Simba ameeleza kuwa Taasisi ya ULINGO, ambayo imefikisha miaka 15 tangu kuanzishwa kwake, imekuwa chachu kubwa ya kuwainua wanawake katika siasa bila kujali vyama vyao.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

“ULINGO imekuwa na mafanikio makubwa. Tumeona wanawake wengi wakiwa wabunge, madiwani na hata vijijini akina mama wanajitokeza kugombea nafasi mbalimbali,” alisema Sophia Simba.
Wangefanya muhula 1 kwa vitu maalumu
 
Niwakati familia zawatu waliokuwa viongozi wakaepembeni wanaposhika madaraka hawana uwezo wakutatua machangamoto zaidi yakupata mali nakuwaza madaraka zaidi
 
Mwanasiasa na Waziri Mstaafu, Sophia Simba, amesema ni wakati muafaka kwa wanawake waliokaa muda mrefu kupitia Viti Maalum Bungeni kuwaachia nafasi vijana ili kuendeleza harakati za uwezeshaji wa wanawake katika siasa.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Ijumaa Februari 28, 2025, kwenye kongamano la kuadhimisha miaka 15 ya Taasisi ya ULINGO na miaka 30 ya Azimio la Beijing, Sophia Simba ameeleza kuwa Taasisi ya ULINGO, ambayo imefikisha miaka 15 tangu kuanzishwa kwake, imekuwa chachu kubwa ya kuwainua wanawake katika siasa bila kujali vyama vyao.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

“ULINGO imekuwa na mafanikio makubwa. Tumeona wanawake wengi wakiwa wabunge, madiwani na hata vijijini akina mama wanajitokeza kugombea nafasi mbalimbali,” alisema Sophia Simba.
Mama la shoka amerudi trending, alikuwa kasahaulika +hasikiki since 2017.
Baada ya Nchimbi kushika usukani nae kaanza kusikika
 
wanatembelea hoja za Tundu Lissu Halafu wanaona aibu kumpa credit au maua yake- taabu tupu- plagiarism huwa haikubariki popote pale duniani- Semeni tu kwamba hoja za Tundu Lissu munaziunga mkono na hamtapungukiwa na kitu
 
Hoja nyingine ya Lissu ni NO REFORMS NO ELECTION na yenyewe ichukueni basi ndugu Mbogamboga?!
 
DAR ES SALAAM: JUMUIYA ya Wanawake Viongozi wa Vyama vya Siasa Tanzania (T-WCP/ULINGO) imetaka kuwepo na ukomo wa miaka 10 kwa wabunge wa viti maalumu na baada ya hapo waende kugombea kwenye majimbo na si kuhodhi nafasi hizo.

Akizungumza Dar es Salaam kwenye maadhimisho ya miaka 15 ya ULINGO na miaka 30 ya Beijing, mwanasiasa mkongwe nchini, Sophia Simba alisema jambo hilo lipo kwenye dondoo za vikao Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) vilivyoketi mara kadhaa miaka ya nyuma.

“Vitu maalumu tulishasema viwe na ukomo, angalau miaka 10 badala ya mtu mmoja kung’ang’ania zaidi ya miaka 30, ananyima wengine fursa ya kujifunza kupitia nafasi hizo,” alisema Simba.

Alisema pamoja na jambo hilo kuzungumzwa mara kwa mara, utekelezaji wake umekuwa mgumu kwa vyama vya siasa nchini na kusema ifike wakati sasa wabunge hao waone haja ya kuachia ngazi wenyewe na kwenda kugombea ngazi ya jimbo.

Alisema vyama vya siasa vinapaswa kuteua wanawake kugombea nafasi mbalimbali na kuwa nafasi za viti maalumu ni kwa ajili ya kuwawezesha kupata uzoefu tu.

“Viti maalumu ni vya uwezeshwaji, wanawake wapate ujuzi na hata fedha za kuingia kwenda kugombea majimboni, lakini si vitu vya kudumu navyo miaka 20 au 30, vina ukomo,” alisema Simba.

Alisema matarajio yao mwaka huu ni kuwa vyama vya siasa vitateua wabunge wa viti maalumu kwa kuzingatia uanzishwaji wake ili kuwapa uzoefu wanawake badala ya wabunge kuhodhi nafasi hizo kwa muda mrefu.

“Tuachie sasa vijana, ni nafasi za kuwawezesha wapate uzoefu, kama umeshakaa bungeni miaka 20, bado unashindwa kuingia kwenye jimbo, basi huwezesheki, umeshindwa kujiwezesha, vinginevyo kukataa kuachia nafasi hizo ni choyo,” alisisitiza Simba.

Alisema wanawake wa awali, akiwemo Zakhia Menghji, Anna Abdallah wangeng’ang’ania wangekuwepo bungeni hadi leo kwa sababu wako hai, ila walikaa miaka mitano wakaingia majimboni, kama ni kushindwa wameshindiwa majimboni.

Akitoa mifano mingine alisema Zanzibar kulikuwa na Tereza Alban Ali na Asha Simba, walipigania sana hakuna watoto wao walioko bungeni, siasa haitaki choyo inataka kupeana nafasi.

Alisema kuna mkwamo, kwani yeye alikuwa mbunge wa viti maalumu kwa miaka 10 akaingia kwenye jimbo akashindwa lakini kwa bahati akateuliwa baadaye akawa mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake wa CCM.

“Naelewa si kwamba wanawake hawawezi, wanao bunge mwenzio? Nenda kagombee jimboni, ukikaa miaka 10 ya viti maalumu inatosha, lakini tunaangaliana usoni tunasema hivi yule ataweza kweli kwenye jimbo? alisema Simba.

Kuhusu uchawa, mbunge huyo wa zamani alisema enzi zao hakukuwepo na watu wanaoitwa ‘chawa’ na kuwa nafasi za uongozi zilipatikana kwa uzoefu.

“Ukiwa chawa lazima utasema uongo, fitna na majungu, ndio yanawafikisha hapo, utasema lako la uongo hata likiwa na kaukweli fulani ila uongo unaweza kuzidi na kupendeza kumbe unaumiza wenzako, tunawapa viongozi wetu wakati mgumu,” alisema Simba.

Awali, Mratibu wa Ulingo, Dk Ave Maria Semakafu alisema taasisi hiyo imetimiza miaka 15 ya kuanzishwa kwake ikiwa na malengo ya kuunganisha wanawake katika vyama vya siasa vyenye usajili na kuwawezesha ili dhana ya 50 kwa 50 itimie.

Imeandaliwa na Ikunda Erick
 
DAR ES SALAAM: JUMUIYA ya Wanawake Viongozi wa Vyama vya Siasa Tanzania (T-WCP/ULINGO) imetaka kuwepo na ukomo wa miaka 10 kwa wabunge wa viti maalumu na baada ya hapo waende kugombea kwenye majimbo na si kuhodhi nafasi hizo.

Akizungumza Dar es Salaam kwenye maadhimisho ya miaka 15 ya ULINGO na miaka 30 ya Beijing, mwanasiasa mkongwe nchini, Sophia Simba alisema jambo hilo lipo kwenye dondoo za vikao Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) vilivyoketi mara kadhaa miaka ya nyuma.

“Vitu maalumu tulishasema viwe na ukomo, angalau miaka 10 badala ya mtu mmoja kung’ang’ania zaidi ya miaka 30, ananyima wengine fursa ya kujifunza kupitia nafasi hizo,” alisema Simba.

Alisema pamoja na jambo hilo kuzungumzwa mara kwa mara, utekelezaji wake umekuwa mgumu kwa vyama vya siasa nchini na kusema ifike wakati sasa wabunge hao waone haja ya kuachia ngazi wenyewe na kwenda kugombea ngazi ya jimbo.

Alisema vyama vya siasa vinapaswa kuteua wanawake kugombea nafasi mbalimbali na kuwa nafasi za viti maalumu ni kwa ajili ya kuwawezesha kupata uzoefu tu.

“Viti maalumu ni vya uwezeshwaji, wanawake wapate ujuzi na hata fedha za kuingia kwenda kugombea majimboni, lakini si vitu vya kudumu navyo miaka 20 au 30, vina ukomo,” alisema Simba.

Alisema matarajio yao mwaka huu ni kuwa vyama vya siasa vitateua wabunge wa viti maalumu kwa kuzingatia uanzishwaji wake ili kuwapa uzoefu wanawake badala ya wabunge kuhodhi nafasi hizo kwa muda mrefu.

“Tuachie sasa vijana, ni nafasi za kuwawezesha wapate uzoefu, kama umeshakaa bungeni miaka 20, bado unashindwa kuingia kwenye jimbo, basi huwezesheki, umeshindwa kujiwezesha, vinginevyo kukataa kuachia nafasi hizo ni choyo,” alisisitiza Simba.

Alisema wanawake wa awali, akiwemo Zakhia Menghji, Anna Abdallah wangeng’ang’ania wangekuwepo bungeni hadi leo kwa sababu wako hai, ila walikaa miaka mitano wakaingia majimboni, kama ni kushindwa wameshindiwa majimboni.

Akitoa mifano mingine alisema Zanzibar kulikuwa na Tereza Alban Ali na Asha Simba, walipigania sana hakuna watoto wao walioko bungeni, siasa haitaki choyo inataka kupeana nafasi.

Alisema kuna mkwamo, kwani yeye alikuwa mbunge wa viti maalumu kwa miaka 10 akaingia kwenye jimbo akashindwa lakini kwa bahati akateuliwa baadaye akawa mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake wa CCM.

“Naelewa si kwamba wanawake hawawezi, wanao bunge mwenzio? Nenda kagombee jimboni, ukikaa miaka 10 ya viti maalumu inatosha, lakini tunaangaliana usoni tunasema hivi yule ataweza kweli kwenye jimbo? alisema Simba.

Kuhusu uchawa, mbunge huyo wa zamani alisema enzi zao hakukuwepo na watu wanaoitwa ‘chawa’ na kuwa nafasi za uongozi zilipatikana kwa uzoefu.

“Ukiwa chawa lazima utasema uongo, fitna na majungu, ndio yanawafikisha hapo, utasema lako la uongo hata likiwa na kaukweli fulani ila uongo unaweza kuzidi na kupendeza kumbe unaumiza wenzako, tunawapa viongozi wetu wakati mgumu,” alisema Simba.

Awali, Mratibu wa Ulingo, Dk Ave Maria Semakafu alisema taasisi hiyo imetimiza miaka 15 ya kuanzishwa kwake ikiwa na malengo ya kuunganisha wanawake katika vyama vya siasa vyenye usajili na kuwawezesha ili dhana ya 50 kwa 50 itimie.

Imeandaliwa na Ikunda Erick

Tubadilishe Katiba ya nchi ili Wabunge watokane na mikoa, kila Mkoa utoe Wabunge wa kuchaguliwa wapatao wawili au wanne, yaani Wabunge Wanaume Wawili na Wabunge Wanawake pia wawe wawili. Kusiwepo na Wabunge wa Viti Maalumu wa kuteuliwa Kutokea Majimboni au wa kuteuliwa kutoka kwenye Uwakilishi wa Majimbo au Mikoa.

Rais wa nchi apewe nafasi zake Kumi tu (10) za kuteua Wabunge wa Kuteuliwa, pasiwepo na idadi nyingine zaidi ya Wabunge wa kuteuliwa zaidi ya hao Kumi wa kuteuliwa na Rais wa nchi.
 
Back
Top Bottom