Tundu Lissu: International pressure na internal mobilisation majibu ya Katiba Mpya Tanzania

Tundu Lissu: International pressure na internal mobilisation majibu ya Katiba Mpya Tanzania

Unko T

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
200
Reaction score
266
Katika madahalo wa Twitter Spaces wa Maria Sarungi, Tundu Lissu ameongea mambo mengi juu ya duru za siasa ya Tanzania na mistakabali wa chaguzi ya 2020 na nini kifanyike kabla ya 2025.

Likaja swali, je ni kwa namna gani tutaweza kupata tume huru ya uchaguzi na kuwa na chaguzi huru kwa maneno mengine demokrasia ya kweli. Lisu akatoa mtazamo wake kuwa mtu pekee atakayefanikisha au kukwamisha demokrasia ya kweli Tanzania ni rais SSH. Kama rais ataafiki katiba mpya, automatically tume ya uchaguzi na msajili wa vyama vya siasa hawata teuliwa na rais, vile vile wafanyakazi wa serikali hawatakua wasimamizi wa uchaguzi tena. Tume huru ya uchaguzi itaweka mazingira sawa ya kisiasa na kidemokrasia na hii tume itapatikana kwa katiba mpya tu.

Lissu akaendelea kusema kuwa Bunge la Ndugai sio kikwazo Kwani tangu enzi na enzi bunge hufuata maelekezo ya Ikulu. Bunge likiambiwa na rais kutekeleza jambo fulani, lenyewe hutii amri. Hivyo mtu wa kupambana nae ni rais na njia za kupambana nae ni mashinikizo ya kimataifa na pressure ya raia wa ndani ya Tanzania kudai katiba kwa nguvu zote.

Historia inamuangalia rais Samia kama atakua mbadilisha mchezo au na yeye atakua kama waliopita, walioogopa mabadiliko.
 
Mungu akubariki na wewe maana huwa unapost mambo mazuri na unatoa comments zako kwa ustaarabu sana na niseme always mimi ni mwumini wako mzuri sana/barikiwa sana wewe kiongozi wangu
Kanisa lake lipo wapi?
 
Kumtoa mtu kwenye jungu kuu hilo lililojaa biriani si ukoko:

IMG_20211119_091739_123.jpg


Yataka waliodhamiria kweli kweli ndani na nje ya nchi.

Mh. Tundu Lissu, Lema, Lembrus Mchome, Mbowe, Mdude, na wote mtesekao kwa ajili ya haki ya nchi hii hamko peke yenu.

Shime waungwana mwanzo mpya hauko mbali.
 
Kwanza ni msaliti kakimbia mapambano pili anajua hawazi kushinda mpaka tume na wafanyakazi wa serikali waache kuteuliwa na raisi mbona anaingia kwenye kinyang'anyiro aje huku atoe hilo shinikizo!
 
Hii Katiba ya sasa ndio inawalinda CCM na serikali yake, hata Samia analijua hilo ndio maana alishatuambia hata tusipowachagua, ni wao ndio watakaotangazwa washindi, hivyo sioni sababu ya kuwa na matumaini hewa ya kusubiri Katiba Mpya kuletwa na mnufaika wa hii Katiba mbovu iliyopo.
 
Nin kifanyike? Au ndio tumeshakubali matokeo?
Hii Katiba ya sasa ndio inawalinda CCM na serikali yake, hata Samia analijua hilo ndio maana alishatuambia hata tusipowachagua, ni wao ndio watakaotangazwa washindi, hivyo sioni sababu ya kuwa na matumaini hewa ya kusubiri Katiba Mpya kuletwa na mnufaika wa hii Katiba mbovu iliyopo.
 
Ni, Vigumu sana kwa ccm kufanya mabadiliko ya katiba mpya. Bila kuwa na shinikizo kubwa la wananchi.

Anyway tuendelee kusubiria
 
Nin kifanyike???au ndio tumeshakubali matokeo?
Watanzania wenyewe ndio tuamue hatma yetu, tusimsubiri fulani tena tunazidi kupoteza muda na tuwe tayari kwa yote yatakayojitokeza wakati wa kuidai ukifika.
 
Kwa watz hawa,inahtajika miaka 50 ijayo
Watanzania wenyewe ndio tuamue hatma yetu, tusimsubiri fulani tena tunazidi kupoteza muda na tuwe tayari kwa yote yatakayojitokeza wakati wa kuidai ukifika.
 
Hongera Lissu na wapambanaji wote. Elimu kubwa bado inahitajika wa Watanzania kujitambua.

Bado wapo wengi wanadhani hata huduma muhimu maji, umeme, barabara ni hisani ya viongozi. Mh JPM, Mh. SHS katoa.
 
Kwanza ni msaliti kakimbia mapambano pili anajua hawazi kushinda mpaka tume na wafanyakazi wa serikali waache kuteuliwa na raisi mbona anaingia kwenye kinyang'anyiro aje huku atoe hilo shinikizo!
Amekusaliti nini weye? Endelea kulima maboga!😝😝😝😝
 
Back
Top Bottom