Pre GE2025 Tundu Lissu: Mambo ya umma hayazungumziwi chumbani, wapambe wa bwana mkubwa hawapendi nizungumze nje

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Usichanganyikiwe siasa ni mchezo wa kubadilika badilika
 
Kwani mtoto wako ni mali ya umma
 
ACHA INYESHE TUJUE PANAPOVUJA🤣
Maana tumesema sana kwamba Chadema ni wezi kama wezi wengine hamkutuskia. Wachumia juani pro max
 
Shetani ndiye hufanya mambo yake kwa siri, Mungu na watu wake wasio na mawaa au uchafu, mambo yao ni hadharani nuruni...

NURU na GIZA havipatani kabisa.....

Mbowe na watu wake anawakilisha GIZA na Tundu Lissu ni kielelezo cha NURU....

Unatolea mfano wa mtoto kuiba kwamba hiyo ni siri ya familia. Mjinga wewe, hujui....!!

Tabia ya mtu (nzuri au mbaya) haiwagi siri kwa sbb hujionesha wazi na kila mtu huiona. Hata "solution" yake, lazima iwe ya wazi na kila mtu aone...

By the way, huyo mtoto unapokuwa unamchapa mboko, kilio chake kitasikika tu na baadae watu kujua kuwa, anaadhibiwa kwa sababu ameiba pesa ya babaye....

Kama kuna wizi ndani ya CHADEMA, hiyo haiwezi kuwa siri kwa sababu watajenga tabia ya wizi ndani ya chama na wakija kupewa Serikali, wataiba na kuifusadi nchi pengine kuliko hata CCM wanavyoiba na kufanya ufisadi wao sasa...!!!

Au baadhi ya viongozi kuhongwa au kununuliwa kwa mapesa ya CCM kupitia wakala wao Abdul (mtoto wa Rais Samia) na tayari mmoja Hezekiah Wenje ametajwa, yaweza vipi kuwa siri kiasi cha isrmewe chumbani...?

All in all, tangu tuanze kumsikiliza Tundu Lissu, hakuna chochote ambacho kinahusu chama au kiongozi mwenzake yeyote ndani ya chama alichokwisha kukisema ambacho mtu anaweza kusema hakikupaswa kusema hadharani...

Kama jambo au kitu hicho kipo, hebu kiseme hapa tukijadili...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…