Tundu Lissu: Mwl. Nyerere alizoea kuishi kwa uongo na udanganyifu

Tundu Lissu: Mwl. Nyerere alizoea kuishi kwa uongo na udanganyifu

Shemeji,

Inauma sana nikisoma na kukumbuka matukio hayo kisha ninashangaa kuna vijana wa tz hii eti wanatetea maovu haya.
 
Wakuu.

Hivi majuzi rais Kikwete ameingia kwenye mtego wa propaganda na kujikuta naye anaingia kwenye kundi la kumsulubu Mheshimiwa Tundu Lissu kwa madai kuwa amewatukana waasisi wa Taifa letu, Jana tena kwenye hotuba yake amerudia yaleyale! cha kushangaza na kustaajabisha ni kwamba wote wanao imba na kughani (akiwemo JK) kuwa Tundu Lissu amemtukana Baba wa Taifa hawasemi kuwa ni tusi gani baya ambalo Mheshimiwa Tundu Lissu amelitukana hata na wakiulizwa kuwa tusi hilo ni lipi hawawezi kulitaja.

Naomba kuwakumbusha pia kuwa hata Mheshimiwa Joseph Mbilinyi (SUGU) Mbunge wa Mbeya mjini kwa tiketi ya CHADEMA naye alisha wahi kuingizwa matatani baada ya kusema kuwa Mhe waziri mkuu Bw Mizengo Pinda ametoa kauli ya "KIPUMBAVU", Sugu alitoa kauli hiyo baada ya waziri mkuu kutoa ile kauli ambayo mahakama ili dhibitisha kuwa ilikuwa kauli ya kipumbavu. kauli ile pia imemuingiza Pinda matatani maana ana kesi ya kujibu. Kauli yenyewe ambayo imeitwa ya kipumbavu ni ile ya "....Wapigwe tu..." Sugu alishatakiwa kwa kuiita kuwa ilikuwa kauli ya "Kipumbavu" na baadae mahakama ikamuona hana kesi ya kujibu.

Mtakumbuka kuwa mheshimiwa Tundu Lissu alipata wasaa wa kujibu alicho kiita kihoja cha kuambiwa kuwa amemtukana Mwl Myerere alipo kuwa anachangia kwenye BM la katiba kule Dodoma. Alisema...

"Mh, Mwenyekiti naomba nijibu vioja , kuna kioja Mh,mwenyekiti kinasema TUNDU LISSU amemtukana baba wa taifa, naomba mh,nijibu kama ifuatavyo mwaka 1995 baba wa taifa alihudhuria mkutano wa Meimosi Mbeya na badae akaandika kijitabu kinaitwa " TUJISAHIHISHE" katika kijitabu chake baba wa taifa alisema asiye kubali kukosolewa hawezi kuwa kiongozi bora na baba wa taifa aliye kuwa mwenyekiti mwanzilishi wa ccm alisema CCM sio mama yangu,Mh mwenyekiti baba wa taifa alikuwa binadamu, hakuwa mungu, hakuwa malaika na hajawa mtakatifu bado, tunaposema makosa yake tunathibitisha ubinadamu wake, na baba wa taifa mwenyewe angekuwa wa kwanza kukubali alikuwa binadamu na sio mungu na kama binadamu alikuwa anakosea, na kwa wasio fahamu mwenyekiti; baba wa taifa aliwahi kuunga mkono jamuhuri ya biafra iliyokuwa inapigana vita kujitenga na Nigeria, alikosea hakuwa mungu, alikosea na tunaposema alikosea hatumdhalilishi tunathibitisha ubinadamu wake, kuna watu ambao wapo humu bungeni ambao akiwa hai walikikimbia chama chake wakaenda NCCR -MAGEUZI wakasubiri mwl amekufa wakarudi CCM, leo wanajidai wao ndo watetezi wa baba wa taifa , Mh,Mwenyekiti nimemaliza na baba wa taifa sitarudia!.."

Jana tarehe 25 April 2014 kwenye hotuba yake, JK ameendelea kupotosha tana kuwa Tundu Lissu amemtukana baba wa Taifa, Hii ilipelekea kujiuliza maswali kadhaa, Je ni kweli kwenye hoja zote na ufafanuzi alio toa Tundu Lissu kuna neno lenye ncha kali (TUSI) ambalo amemtukana baba wa Taifa?! Je kwenye hotuba nzima JK ameshikilia tu tusi ambalo halionekani na hakuna hoja nyingine za msingi ambazo zinahitaji majibu ya kina?! Na kama tusi hilo amelishikilia na kulighani kila mara, Je tusi hilo ni lipi?! Je wakati huu rais JK anapo msingizia Tundu Lissu kuwa amemtukana Mwl Nyerere (muasisi wa taifa) yeye anajijua kuwa ametukana Mwl Nyerere kuliko anavyo msingizia Tundu Lissu?!


Kama raisi wetu (JK) ana msingizia Tundu Lissu kuwa amemtukana Mwl Nyerere, je orodha hii fupi ya matendo ya serikali ya JK sio matusi ya dhahiri kwa Mwl Nyerere (muasisi) wa Taifa letu?!

1. Mabadiliko ya 10 ya katiba ya Zanzibar ambayo yamempora JK mabadaraka tena akiwa bado yungali madarakani na aka kaa kimya na sasa hivi analalamika kuwa kuna vyama vinataka kuvunja muungano huku akijua kuwa ukimya wake ndio umechangia kuvunja nchi moja (Ya muungaon) tuliyo kuwa nayo na sasa tuna nchi mbili, Je haya sio matusi kwa Mwl JK aliyesema "...Rais tunaye mchagua lazima ajue kuitetea na kuilinda katiba na kama hawezi aende akalime shamba lake..." na amedhihirisha kwa kuacha madaliko ya 10 ya katiba kule ZNZ kuanzisha dola huru?

2. Rais Jk anajua kuwa ulitokea wizi wa pesa za wavuja jasho kupitia akaunti ya malipo ya nje (EPA) na imesemwa maraka kadhaa kuwa pesa hizo ndio zilisaidia kampeni za kumuingiza madarakani 2005 (Haijawahi kukanushwa) na baadae walio iba pesa hizo (baadhi) ambao ni makada wa CCM yeye mwenyewe akihutubia bunge Dodoma akawaombwa kuzirejesha fedha hizo huku akijua kuwa waliofanya wizi huo ilikuwa kinyume na sheria, Je hayo hayakuwa matusi kwa baba wa Taifa kukiuka katiba na sheria za nchi?!

3. Je wale watanzania wenzetu walio uwawa kule Arusha Jan 5, 2011 na baadae ripoti ya tume ya jaji Ramadhani Manento kukiri kuwa Polisi walihusika na mauwaji yale kwa sababu za kisiasa na baadae JK huyo huyo akiwa Dodoma akiwahutubia wajumbe wa kamati kuu akawaagiza CCM kuacha kulitumia jeshi la Polisi kudhibiti vyama pinzani na baadae akauwawa Daud Mwangosi na aliyesimamia mauwaji ya Mwangosi, JK huyohuyo akampandishwa badala ya kumuwajibisha! Je hayo hayakuwa matusi kwa Mwl Nyerere aliyepinga ukandamizaji na ukiukaji wa haki za binadamu?!

4. Je aibu hii ya dawa za kulevya ambayo viongozi wa CCM na serikali yake wameamua kulibebesha taifa hili ili wao wapate fedha huku wakiwageuza vijana wenzetu kuwa punda wao wa kubebea bidhaa hizo haramu, na wengine kugeuka kuwa mazezete kwa matumizi ya madawa hayo sio Matusi kwa Mwl Nyerere (Muasisi wa Taifa hili)?!

5. Je; sio matusi kwa viongozi waandamizi wa CCM kuhusishwa na uporaji na uwindaji haramu wa raslimali za Taifa (Kama kujilimilikisha madini na uuwaji wa wanyama pori) ambapo Mwl Nyerere enzi za utawala wake alizilinda na kuzihifadhi kwa matumizi na faida ya wananchi wote wa Tanzania?! (mwalimu alilinda mpaka mabenki, leo NBC iko wapi URAFIKI iko wapi, SUKITA iko wapi, Viwanda alivyojenga na kuviacha viko wapi?)

6. Je kurithishana madaraka kwenye chama ambako Mwl Nyerere hakuthubutu kufanya hivyo kwa mwanaye yoyote sio matusi kwake?! (rejea chaguzi ndogo za hivi karibu). Ni ipi kamusi ya matusi ambayo JK ameamua kuitumia na wapambe wengine kusema kuwa Tundu Lissu ametukana?!

7. Je Mwl Nyerere alipo kuwa mwenyekiti wa CCM aliasisi na kusimamia kikosi cha kijeshi ndani ya chama ambacho kimekuwa na kawaida ya kuteka, kuuwa na kutesa wanachama wa vyama vingine na polisi wakaogopa kuchukua hatua dhidi ya kikosi hicho?! (rejea mauwaji ya Mbwana Masudi kule Igunga, Mauwaji ya Samson Mbwambo kule Arumeru nk), Je haya sio matusi kwa Mwl Nyerere aliyekuwa ana sisitiza kuheshimu utu wa mwanadamu?!

8. Je hayakuwa matusi kwa Mwl Nyerere kukiri mbele ya vyombo vya habari vya kimataifa kuwa ".... Sijui kwa nini wananchi wangu ni maskini..." Huku akijua kuwa nchi ina raslimali nyingi na yeye amekuwa busy kwenda nje kuomba misaada kuliko Mwl aliyekuwa busy kusisitiza kujitegemea na kuondoa utegemezi kupitia program kadha wa kadha?
(Mfano vijiji vya ujamaa, kilimo cha kufa na kupona nk)

9. Je si matusi kwa Mwl Nyerere kutokuheshimu maoni ya wananchi na matokeo yake kutumia ubabe kuhakikisha kuwa msimamo wa chama ndio unaleta katiba huku akijua kuwa katiba inayoundwa si katiba ya chama bali katiba ya nchi ambayo ni kuu kuliko katiba yenye itikadi au msimamo wa chama chochote?!

10. Je kumfanya Mwl kuwa aliyo yafanya hayafai kukosolewa sio kumfananisha na Mungu au Malaika?! Je hayo sio matusi ya kujipendekeza wakati Mwl Mwenyewe amesha kiri makosa yake mara kadhaa na hata kufikia hatua ya kutoa machapisho kukiri makosa yake?! (Mfano; Ukisoma "Tujisahihishe" "Uongozi wetu na hatma ya Tanzania") na, je sio kinyume na mafundisho ya Mungu kumfanya binadamu mwenzako kuwa ni mtimilifu kuliko Mungu?!

Nabaki tu kujiuliza; Kati ya Mheshimiwa Kikwete na Tundu Lissu nani kamtukana Mwl Nyerere matusi yanayo onekana dhahiri kuliko yale ya kubumba na kusingizia bila ushahidi wenye mashiko?! Nani anaweza kunieleza TUSI lililo tukanwa na Tundu Lissu?




Yale matendo uliorodhesha ni mabaya Sana. Lkn hata Kama JK kamtukana Nyerere kwa kiwango kipi HAKUFUTI MATUSI NA KASHFA ZA MAKUSUDI ZA TUNDU LISU DHIDI YA TUNU YA NCHI YETU MUASISI WA TAlFA HILI MWALIMU NYERERE.
Huwezi kusema NYERERE ameghushi saini halafu tusi hilo lifunikwe kwa makosa mengine yaliyofanywa na wengine. Matusi ya lisu dhidi ya Baba wa Taifa yatasimama na ya wengine hivyo hiyo. Tusichanganye wala kulinganisha mambo hayo kwa minajili OVU NA KUPUNGUZA UZITO WA MAKOSA YA TUNDU LISU YA KUTUTUKANIA KIPENZI CHETU BABA WA TAIFA MWALIMU NYERERE.
 
Hawa wakat mwl. akiwepo walifyata mikia, pumbavuuu angewashona midomo. Waoga wakubwa nyie shenz type, wakat wa ukolon baba zenu walijifanya mabubu mbele ya Wazungu...leo mna vi-tv mnaropoka2, Majinuni mkubwa wee.
 
Wewe umefanya nn? Umejaa nadharia2 za kjinga, hebu tafakar kwa upana we mzee. Hv huu wiz wa fedha za Umma unaofanywa na baadh ya viongoz, Udini, rushwa kibao, Elimu yenyewe ndiyo kama yenu "theoletical chain" munamuhoj nan? Mnajifanya mnafalsafa kumbe fate tupu...hamjadili ujinga unaotokea bungeni, mnajadili marehemu...andiken vitabu bas waoga wa hoja nyie. Aliye juu mngoje chini pambafuu mtangoja saana. Kama ni mwongo, alitumia uongo mt. kilimanjaro ikawa Tz, Ni uongo huo huo uliitoa Kagera Uganda, na ziwa nyasa kuwa partly Tz. Siku zote ktk nchi watu machizi huwa hawakosikani so Nyerere angewafanyeje kama sio kuwapa kipondo. Kaz kwel kwel!
 
Mungu hamtupi mja wake, kwa jinsi ambavyo vichaa wamemdhalilisha baba wa taifa, Marehemu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere(R.I.P) kwa kumtukana tena tukiwa hatunaye duniani, hakika SERIKALI tatu hata kama ikitokea miujiza zikawepo lazima Marehemu atapigana kufa na kupona waasisi wake walaaniwe.

Vita hiyo ya baba wa taifa dhidi ya wanaodhani kubaki kwao hapa duniani na yeye kutangulia mbele za haki ni ticketi tosha ya kumdhihaki, kudhihaki muundo wa serikali aliouacha lazima mshindi atakuwa Marehemu tu.

Watu kutoka kona mbalimbali za Tanzania wakiwemo viongozi wa dini, wasomi na makundi mbalimbali waliojitokeza hadharani kulaani dhihaka dhidi ya baba wa Taifa ni majemadari wa vita hiyo wakiongozwa na Marehemu mwenyewe Baba wa taifa.

Tusubiri tu tuone mwisho wa kulalama kwa hawa wanaojiita jeshi la waasi lililosubiri Kamanda Nyerere atoweke duniani ndo wajitokeze kama nyoka alivyojitokeza kule kwenye bustani ya hedeni na kuwadanganya ADAM na HAWA, nyoka huyo akifikiri Mungu hayupo.

Hawa watatambaa na tumbo kama nyoka, ni suala la muda tu.
 
Ndugu Cybercrime marehemu hawaongei wala kujua neno lolote linaloendelea huku kwenye dunia ya walio hai. Wewe jenga hoja yako tu utaeleweka huna haja ya kutafuta uhalali wa hoja zako kwa kumtumia marehemu ambaye hana jinsi ya kuchangia hoja ili kuweka wazi msimamo wake.
 
This is crazy. We don't believe in the living dead. Kama mnadhani marehemu huwa wana msaada mbona msiutafute siku zote hizo?
 
Acheni upuuzi, mwalimu alifanya yake na amemaliza, acheni kumtumia marehemu kujustify ujinga wenu, sisi ndo tuko hai na tunajua muundo gani wa serikali tunaoutaka!
wadanganyeni vichaa wenu, lazima watalaaniwa, dhambi kubwa sana kudhihaki marehemu.
 
Tayari wameshalaaniwa hawa ndo maana waliomtusi Mungu kawaumbua hasa kwa michezo yao ya hit from the back. Kamuulize Mbatia, Mnyika, Lipumba na Jussa
 
Acheni upuuzi, mwalimu alifanya yake na amemaliza, acheni kumtumia marehemu kujustify ujinga wenu, sisi ndo tuko hai na tunajua muundo gani wa serikali tunaoutaka!

waache upuuzi wale wanaotukana marehemu.
 
Mungu hamtupi mja wake, kwa jinsi ambavyo vichaa wamemdhalilisha baba wa taifa, Marehemu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere(R.I.P) kwa kumtukana tena tukiwa hatunaye duniani, hakika SERIKALI tatu hata kama ikitokea miujiza zikawepo lazima Marehemu atapigana kufa na kupona waasisi wake walaaniwe.

Vita hiyo ya baba wa taifa dhidi ya wanaodhani kubaki kwao hapa duniani na yeye kutangulia mbele za haki ni ticketi tosha ya kumdhihaki, kudhihaki muundo wa serikali aliouacha lazima mshindi atakuwa Marehemu tu.

Watu kutoka kona mbalimbali za Tanzania wakiwemo viongozi wa dini, wasomi na makundi mbalimbali waliojitokeza hadharani kulaani dhihaka dhidi ya baba wa Taifa ni majemadari wa vita hiyo wakiongozwa na Marehemu mwenyewe Baba wa taifa.

Tusubiri tu tuone mwisho wa kulalama kwa hawa wanaojiita jeshi la waasi lililosubiri Kamanda Nyerere atoweke duniani ndo wajitokeze kama nyoka alivyojitokeza kule kwenye bustani ya hedeni na kuwadanganya ADAM na HAWA, nyoka huyo akifikiri Mungu hayupo.

Hawa watatambaa na tumbo kama nyoka, ni suala la muda tu.

Mkuu naomba nikukumbushe maneno aliyosema Nyerere mwenyewe, akiwashauri wakuu ndani ya ccm juu ya namna bora ya kuchagua mgombea wao wa Urais kwa mazingira ya sasa alisema hivi ".... kuchagua mgombea kwa njia ya mizengwe kama tulivyokuwa tukifanya kumepitwa na wakati.....", hapa inamaanisha anakiri kuna makosa aliwahi kuyafanya huko nyuma, hata hili la serikali 3 akiibuka leo atawashangaa sana CCM kung'ang'ania 2 maana ni mizengwe tu iliyopitwa na wakati.
 
Tayari wameshalaaniwa hawa ndo maana waliomtusi Mungu kawaumbua hasa kwa michezo yao ya hit from the back. Kamuulize Mbatia, Mnyika, Lipumba na Jussa

teh teh, malipo ni hapa hapa duniani mkuu, lissu lazima ataokota makopo tu.
 
Ndugu Cybercrime marehemu hawaongei wala kujua neno lolote linaloendelea huku kwenye dunia ya walio hai. Wewe jenga hoja yako tu utaeleweka huna haja ya kutafuta uhalali wa hoja zako kwa kumtumia marehemu ambaye hana jinsi ya kuchangia hoja ili kuweka wazi msimamo wake.
Hayo ni mawazo ya kitaahira kabisa
 
teh teh, malipo ni hapa hapa duniani mkuu, lissu lazima ataokota makopo tu.
Si unamuona anavyochanganyikiwa sasa? Wenzake hawajahitimisha mazungumzo, yeye anageuka kuwa msemaji wa Msajili wa vyama vya siasa. Huo ndo mwanzo wa kuokota makopo
 
Mkuu naomba nikukumbushe maneno aliyosema Nyerere mwenyewe, akiwashauri wakuu ndani ya ccm juu ya namna bora ya kuchagua mgombea wao wa Urais kwa mazingira ya sasa alisema hivi ".... kuchagua mgombea kwa njia ya mizengwe kama tulivyokuwa tukifanya kumepitwa na wakati.....", hapa inamaanisha anakiri kuna makosa aliwahi kuyafanya huko nyuma, hata hili la serikali 3 akiibuka leo atawashangaa sana CCM kung'ang'ania 2 maana ni mizengwe tu iliyopitwa na wakati.
Hayo maneno umeyatoa wapi na mbona hayana uhusiano wowote na serikali tatu? Kwa nini akina lissu hawakuibuka na ulaghai wa serikali tatu kabla hajafa?
 
Mungu hamtupi mja wake, kwa jinsi ambavyo vichaa wamemdhalilisha baba wa taifa, Marehemu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere(R.I.P) kwa kumtukana tena tukiwa hatunaye duniani, hakika SERIKALI tatu hata kama ikitokea miujiza zikawepo lazima Marehemu atapigana kufa na kupona waasisi wake walaaniwe.

Vita hiyo ya baba wa taifa dhidi ya wanaodhani kubaki kwao hapa duniani na yeye kutangulia mbele za haki ni ticketi tosha ya kumdhihaki, kudhihaki muundo wa serikali aliouacha lazima mshindi atakuwa Marehemu tu.

Watu kutoka kona mbalimbali za Tanzania wakiwemo viongozi wa dini, wasomi na makundi mbalimbali waliojitokeza hadharani kulaani dhihaka dhidi ya baba wa Taifa ni majemadari wa vita hiyo wakiongozwa na Marehemu mwenyewe Baba wa taifa.

Tusubiri tu tuone mwisho wa kulalama kwa hawa wanaojiita jeshi la waasi lililosubiri Kamanda Nyerere atoweke duniani ndo wajitokeze kama nyoka alivyojitokeza kule kwenye bustani ya hedeni na kuwadanganya ADAM na HAWA, nyoka huyo akifikiri Mungu hayupo.

Hawa watatambaa na tumbo kama nyoka, ni suala la muda tu.

wewe Alikuwambia kua Ataleta Shida? Nyie ndio wale wale tu
 
Back
Top Bottom