Hadi pale mtakapofikia kugundua mabaya ya viongozi wenu waliopita ndipo inakuwa borderline ya historia na sasa. Kumbuka Germany na Hiltler, USSR na Gorbachev n.k. Hakuna Mjerumani anayekumbatia mambo ya Hitler na ndipo sasa unaona hata Germany haipigani tena vita za kijinga.
Kama kuna mabaya ya Nyerere yawekwe hadharani na iwe mwisho wa siasa za mzimu wake. Hii ni era nyingine na of course ukisema ku-practice ujamaa kwa sasa kwa mpangilio wa Nyerere na Sokoine dunia itakucheka, utawekewa sanctions na utaitwa dikteta, watakungoa kwa risasi za moto. Ni nyakati tu kama inavyosemekana "time will tell". Kama siasa za Nyerere zinakuwa questionable kabla hata hajaoza vyema basi ni wazi hakuwa intelligent na wala hakuwa nabii wa kisiasa na hivyo basi alikuwa na makosa mengi na wala mambo yake hayastahili kutumika kwa reference ya kutatua matatizo yetu tuliyonayo kwa sasa. He was short sighted. Tusidanganyike. My take is hakuwa Mungu na hivyo alikuwa prone to human errors na gross mistakes kama wanadamu wengine. Hakuwa genius kwa kuwa hamna jipya zaidi ya undugu ambao hautusaidii chochote katika nyanja za financial freedom. Kifupi alitupa utumwa wa milele katika uchumi kama sio Mwinyi.
To me Mwinyi is an intellectual and intelligent than Nyerere. How? He ruled 10 years only and the effect is what we will keep for the rest of our lives. Enormous positive impact to development na wachumi watakubali Mwinyi aliweza na kufanikiwa kwenye turn around ya uchumi wa nchi katika sectors zote. English medium, better housing, transport, afya, trade, taxation, kipato cha kila mmoja wetu, nk. na akadumisha undugu vile vile kwa ruksah! Hakuwa mwongo mwongo. Alikuwa m-sure wa ukweli. Hakuwa mtu wa ndio mzee. Hakuna kitu kikubwa kama rais wa nchi kuwapatia wananchi wake financial freedom. Haya ndiyo maendeleo. Kuficha dollars, kuogopa kufanya biashara na kumiliki mali haya ndio baadhi ya makosa na udanganyifu wa Nyerere.
Kwa kifupi tunaweza mwita mwana mapinduzi katika uchumi na maisha ya watanzania.
Juzi kati miaka ya mwanzo 80's kariakoo ilijaa vijumba ya wazee wake Nyerere vya tope je tujiulize nani alifanikiwa kuviezeka kwa bati na tofali kutani? Mwinyi ndiyo anakuja kwenye picha kwa wale wabishi.
Kama Mwinyi aliweza hayo yote kwa muda mfupi Nyerere alishindwa nini? Hapo ndio sasa nani ana akili na kujua miongozo ya nchi inakuja into play.
Then sasa hawa wadogo zake Mkapa na Kikwete wakaendeleza alipoishia kaka yao Mwinyi.
Mwinyi yeye hakupata alipoishia Nyerere zaidi ya kubomoa kabisa alichokijenga na hii minaonyesha wazi kuwa ilikuwa uchumi wa vijumba vya udongo na makuti juu na akaanzisha kitu kipya, Tanzania mpya katika uchumi, elimu, afya, biashara nk. Itakumbukwa pia kuwa aliweza hata kuweka mipango ya ukusanyaji kodi ambao sasa wengine wameusimamia kwa dhati na kufika hapa tulipo. Alipoishia Nyerere palikuwa hapana mashiko kabisa. Kumbukeni sukari, unga, mafuta, kwa balozi. Viatu ilikuwa luxury na majority ya watanzania walitembea peku kama enzi za primitive age. Nguo ilikuwa tabu, na tuliishi kama wafungwa tu waishivyo sasa. Sabuni tabu, sukari tabu, pesa kwa raia tabu ili mradi lindi la umaskini.
Sasa ukiona doctrine za mwanasiasa zimekuwa questionable hiyo ni dhahiri - udanganyifu uko ndani yake na wananchi wapipumbazwa sasa wanaamka mfano Hitler, Gorbachev, nk. Kwa wanaobisha mtayaona makubwa zaidi ya haya yanayoulizwa sasa.
Nawasilisha