Tundu Lissu: Ninahofu kuhusu uchaguzi mkuu wa CHADEMA lakini dawa ni moja tu

Tundu Lissu: Ninahofu kuhusu uchaguzi mkuu wa CHADEMA lakini dawa ni moja tu

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,307
Reaction score
25,932
Mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu A.M. Lissu amesema kuwa ana hofu kubwa juu ya mustakabali wa CHADEMA baada ya uchaguzi mkuu utakaofanyika juma lijalo.

Lissu ameyasema hayo katika kipindi cha runinga cha Crown Media kijulikanacho kama Kasri la Kikeke kilichoongozwa na Salim Kikeke. Lissu amesema kuwa kulingana na yanayoendelea kuelekea uchaguzini, mtu yeyote timamu lazima awe na hofu.

Lissu ameongeza kusema kuwa kwasasa CHADEMA imegawanyika katika pande mbili-ya Mbowe na Lissu...mgawanyo unaotishia mustakabali wa chama hicho kikuu cha upinzani nchini.

Alipoulizwa iwapo atashindwa uchaguzini atafanya nini na kama atahama au la, Lissu amesema akishindwa atakuwa hajawahi kuwa Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA na HATAHAMA chama hicho na atabaki kuwa mwanachama wa kawaida wa CHADEMA.

Kuhusu dawa ya kuzuia suitafahamu inayoweza kujitokeza baada ya uchaguzi, Lissu amesema kuwa dawa pekee ni kuwa na uchaguzi mkuu wa CHADEMA huru, wa haki na wa wazi.

Yetu macho na masikio!
 
20250114_185518.jpg
 
Alipoulizwa iwapo atashindwa uchaguzini atafanya nini na kama atahama au la, Lissu amesema akishindwa atakuwa hajawahi kuwa Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA na HATAHAMA chama hicho na atabaki kuwa mwanachama wa kawaida wa CHADEMA.
Muongo huyo, hapo anazuga tu kwa kuwa kuna uchaguzi unakuja.
Mtu ameshatangaza wazi kuwa chadema siyo mama yake au baba yake, atabaki chamani namna gani?
Amekuwa akiwapaka kila mtu asiyemuunga mkono yeye, atabaki chamani namna gani akishindwa?
Lisu yuko chadema ili kuridhisha tamaa yake ya uroho wa madaraka tu, asipoyapata atatimuka mara moja!
 
Muongo huyo, hapo anazuga tu kwa kuwa kuna uchaguzi unakuja.
Mtu ameshatangaza wazi kuwa chadema siyo mama yake au baba yake, atabaki chamani namna gani?
Amekuwa akiwapaka kila mtu asiyemuunga mkono yeye, atabaki chamani namna gani akishindwa?
Lisu yuko chadema ili kuridhisha tamaa yake ya uroho wa madaraka tu, asipoyapata atatimuka mara moja!
Kunywa maji mkuu. Hiyo temper uliyonayo hata Mbowe hajawahi kuwa nayo
 
Huyo Lisu kawaida yake kulia lia, kabla ya kugombea urais TLS alipiga kelele sana, akashinda hakuna lililofanyika, yeye ni Makamu mwenyekiti hata haelewi nafasi yake anapaswa kufanya nini, maana hata ukimuuliza yeye kafanya nini tangu ashike hiyo nafasi haelewi, waulize wafuasi wake sasa, utaambulia matusi asubuhi mpaka jioni lakini nao hawana jibu.

Halafu wanakwambia Lisu ni kichwa anapaswa awe mwenyekiti, afanye nini, alichoshindwa kukifanya sasa?

Leo anagombea uwenyekiti chadema anajiona ni malaika aliyeshuka, lakini yeye ndiye huwa anahujumiwa tu kila siku, kila mahala, na keshaanza kulilia anatilia mashaka matokeo hata uchaguzi haujafanyika.

Labda atashinda, sasa ukiwauliza wafuasi wake atafanya nini, eti atakomesha Rushwa za Mbowe, Wakati hata sasa hawana ushahidi wowote wa Mbowe kupokea rushwa, wanasema Abdul na Mama yake, ushahidi hawana.

Lisu anawaburuza lakini watajuata ikitokea bahati mbaya akashinda.

Mini nashauri afukuzwe akishindwa, ili abebe wafuasi wake waende waendako, na wakiweza waanzishe chama chao.
 
Hili genge wanaojiita Team Lisu, wanatafuta madaraka, wakiyakosa watageukana huko chadema. Hao hao watakao mshambulia Lisu, kwasababu muda huo Mbowe hatokuwepo.
 
Muongo huyo, hapo anazuga tu kwa kuwa kuna uchaguzi unakuja.
Mtu ameshatangaza wazi kuwa chadema siyo mama yake au baba yake, atabaki chamani namna gani?
Amekuwa akiwapaka kila mtu asiyemuunga mkono yeye, atabaki chamani namna gani akishindwa?
Lisu yuko chadema ili kuridhisha tamaa yake ya uroho wa madaraka tu, asipoyapata atatimuka mara moja!
Sasa ataenda wapi maana hakuna wa kumpokea ccm hawawezi kamwe kumkubali
 
Kunywa maji mkuu. Hiyo temper uliyonayo hata Mbowe hajawahi kuwa nayo
Hakuna cha kunywa maji wala soda, huo ni ukweli mtupu tunasubiri utimilifu wake tu. Aliposema chadema siyo mama yake wewe unadhani alimaanisha nini, kama siyo kuwa mguu mmoja ndani na mguu mwingine nje?
 
Muongo huyo, hapo anazuga tu kwa kuwa kuna uchaguzi unakuja.
Mtu ameshatangaza wazi kuwa chadema siyo mama yake au baba yake, atabaki chamani namna gani?
Amekuwa akiwapaka kila mtu asiyemuunga mkono yeye, atabaki chamani namna gani akishindwa?
Lisu yuko chadema ili kuridhisha tamaa yake ya uroho wa madaraka tu, asipoyapata atatimuka mara moja!
Uwe unaongea kama mtu mwenye akili timamu mahaba yako kwa Ayatolah yasikufanye uropoke namna hiyo dada angu!!kama huna idea na siasa jadili na wadada wenzio mambo yenu sio unajivunjia heshima kwa kuropoka mambo ya hovyo
 
Muongo huyo, hapo anazuga tu kwa kuwa kuna uchaguzi unakuja.
Mtu ameshatangaza wazi kuwa chadema siyo mama yake au baba yake, atabaki chamani namna gani?
Amekuwa akiwapaka kila mtu asiyemuunga mkono yeye, atabaki chamani namna gani akishindwa?
Lisu yuko chadema ili kuridhisha tamaa yake ya uroho wa madaraka tu, asipoyapata atatimuka mara moja!
Kwani wewe chadema ni mama yako? Kama Mwl Nyerere ndiye muasisi wa ccm lakini alidiriki kusema ccm sio mama yake sembuse Lisu?
Unazijua sababu za Mwalimu kusema ccm sio mama yake au unajiropokea tu?
 
Mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu A.M. Lissu amesema kuwa ana hofu kubwa juu ya mustakabali wa CHADEMA baada ya uchaguzi mkuu utakaofanyika juma lijalo.

Lissu ameyasema hayo katika kipindi cha runinga cha Crown Media kijulikanacho kama Kasri la Kikeke kilichoongozwa na Salim Kikeke. Lissu amesema kuwa kulingana na yanayoendelea kuelekea uchaguzini, mtu yeyote timamu lazima awe na hofu.

Lissu ameongeza kusema kuwa kwasasa CHADEMA imegawanyika katika pande mbili-ya Mbowe na Lissu...mgawanyo unaotishia mustakabali wa chama hicho kikuu cha upinzani nchini.

Alipoulizwa iwapo atashindwa uchaguzini atafanya nini na kama atahama au la, Lissu amesema akishindwa atakuwa hajawahi kuwa Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA na HATAHAMA chama hicho na atabaki kuwa mwanachama wa kawaida wa CHADEMA.

Kuhusu dawa ya kuzuia suitafahamu inayoweza kujitokeza baada ya uchaguzi, Lissu amesema kuwa dawa pekee ni kuwa na uchaguzi mkuu wa CHADEMA huru, wa haki na wa wazi.

Yetu macho na masikio!

Alipoulizwa iwapo atashindwa uchaguzini atafanya nini na kama atahama au la, Lissu amesema akishindwa atakuwa hajawahi kuwa Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA na HATAHAMA chama hicho na atabaki kuwa mwanachama wa kawaida wa CHADEMA.
 
Muongo huyo, hapo anazuga tu kwa kuwa kuna uchaguzi unakuja.
Mtu ameshatangaza wazi kuwa chadema siyo mama yake au baba yake, atabaki chamani namna gani?
Amekuwa akiwapaka kila mtu asiyemuunga mkono yeye, atabaki chamani namna gani akishindwa?
Lisu yuko chadema ili kuridhisha tamaa yake ya uroho wa madaraka tu, asipoyapata atatimuka mara moja!
Mkuu kweli unajua maana na tafsiri ya hili neno 'uroho'???
 
Back
Top Bottom