Malimi Jr
JF-Expert Member
- May 28, 2017
- 1,287
- 2,743
Takribani miaka 60 sasa Watanzania hususani tabaka tawaliwa, tumeishi kwenye ufukara uliotopea. Wakati huo tabaka tawala wakijineemesha kupitia msamiati uzalendo.
Miaka 60 ya uhuru bado tunapewa ahadi ya jiji la Arusha kuwa kama CALIFORNIA, wakati watoto wetu wanasomea chini ya miti, maajabu haya!!!
Miaka 60 ya uhuru wameshindwa hata kutengeneza mazingira wezeshi ya vijana kuajiriwa na kujiajiri. Halafu mtu mmoja anataka kuibadilisha Tz iwe kama ulaya kwa miaka 5 ijayo. Kama tu sera ya viwanda imemshinda hilo la kuwa kama ataliweza? Lakini nisimlaumu sana make Ulaya yake ipo chattle.
Watanzania sio wajinga tuna jambo letu masaa machache yajayo. Tunaenda kumchagua Tundu Lissu, nusu mtu nusu chuma. Tunahitaji Rais mwenye uthubutu hata tukimtuma kwenda kudai haki kwenye tanuru la moto ataingia na kurudi akiwa hai.
Tundu Lissu atakuwa Rais ambaye ni mfariji, mtenda haki, mpenda maendeleo ya watu na sio vitu, mtoa misaada kwa wahanga wa majanga mbalimbali, hata tukimtuma UN ataenda bila uoga.
Watanzania tumeshaamua kuliondoa jinamizi hili la ufukara (CCM) ambalo kwa miaka 60 limetung'ang'ania. Limefeli sekta zote, UTALII, KILIMO, UVUVI, MISITU, MADINI, NISHATI, MIUNDOMBINU, AFYA, MAJI, kote ni kilio tu.
Masaa machache yajayo Watanzania twendeni, twendeni, twendeni, twendeni tukampigie kura mtu ambaye hata akipigwa risasi 38 anatoka hai. Watanzania tunaenda kuitetea nchi yetu iliyovurugwa kwa miaka 60. Si kazi rahisi ila kwa umoja wetu tutashinda.
@NIYEYE2020. Tarehe 28.10.2020 hatufanyi makosa tunaenda kuchagua nusu chuma, nusu mtu. Ameonesha uthubutu hata kupitia kwenye kampeni zake, ni mtu asiyechoka kutupigania hakika huyu ndiye mbeba maono.
Tukutane Jumatano. Usihangaike kutafuta jina lake ukipewa tu ile karatasi ya kura nenda chini mwishoni utamuona niyeye 2020. weka alama ya vema([emoji818]) kwenye kisanduku kilicho wazi kulia kwake. Usiongeze alama nyingine, kunja karatasi yako kisha kaweke kwenye sanduku lenye mfuniko wa rangi ya bluu.
HAKI, UHURU NA MAENDELEO.
Miaka 60 ya uhuru bado tunapewa ahadi ya jiji la Arusha kuwa kama CALIFORNIA, wakati watoto wetu wanasomea chini ya miti, maajabu haya!!!
Miaka 60 ya uhuru wameshindwa hata kutengeneza mazingira wezeshi ya vijana kuajiriwa na kujiajiri. Halafu mtu mmoja anataka kuibadilisha Tz iwe kama ulaya kwa miaka 5 ijayo. Kama tu sera ya viwanda imemshinda hilo la kuwa kama ataliweza? Lakini nisimlaumu sana make Ulaya yake ipo chattle.
Watanzania sio wajinga tuna jambo letu masaa machache yajayo. Tunaenda kumchagua Tundu Lissu, nusu mtu nusu chuma. Tunahitaji Rais mwenye uthubutu hata tukimtuma kwenda kudai haki kwenye tanuru la moto ataingia na kurudi akiwa hai.
Tundu Lissu atakuwa Rais ambaye ni mfariji, mtenda haki, mpenda maendeleo ya watu na sio vitu, mtoa misaada kwa wahanga wa majanga mbalimbali, hata tukimtuma UN ataenda bila uoga.
Watanzania tumeshaamua kuliondoa jinamizi hili la ufukara (CCM) ambalo kwa miaka 60 limetung'ang'ania. Limefeli sekta zote, UTALII, KILIMO, UVUVI, MISITU, MADINI, NISHATI, MIUNDOMBINU, AFYA, MAJI, kote ni kilio tu.
Masaa machache yajayo Watanzania twendeni, twendeni, twendeni, twendeni tukampigie kura mtu ambaye hata akipigwa risasi 38 anatoka hai. Watanzania tunaenda kuitetea nchi yetu iliyovurugwa kwa miaka 60. Si kazi rahisi ila kwa umoja wetu tutashinda.
@NIYEYE2020. Tarehe 28.10.2020 hatufanyi makosa tunaenda kuchagua nusu chuma, nusu mtu. Ameonesha uthubutu hata kupitia kwenye kampeni zake, ni mtu asiyechoka kutupigania hakika huyu ndiye mbeba maono.
Tukutane Jumatano. Usihangaike kutafuta jina lake ukipewa tu ile karatasi ya kura nenda chini mwishoni utamuona niyeye 2020. weka alama ya vema([emoji818]) kwenye kisanduku kilicho wazi kulia kwake. Usiongeze alama nyingine, kunja karatasi yako kisha kaweke kwenye sanduku lenye mfuniko wa rangi ya bluu.
HAKI, UHURU NA MAENDELEO.