Tundu Lissu: Sijawahi kupishana maneno na Mbowe tangu nijiunge CHADEMA 2004, hakuna wa kutufitinisha!

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716


Makamu mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu amesema yeye na Mwenyekiti wake Mbowe wako vizuri kuliko wakati mwingine wowote.

Lissu amesema hata alipokutana na Rais Samia kule Ubelgiji alimweleza wazi kuwa atarudije nyumbani ilhali Mwenyekiti wake yuko magereza, ndipo Rais akalifanyia kazi.

Lissu amesisitiza kuwa wanatarajia yeye na Mbowe wakosane basi watasubiri sana.

Source: ITV

Sabato njema!
 
Hahaha kumbe Rais Samia kamtoa Mbowe ili Lissu arudi Tanzania? Na Samia alipoapishwa tu kuwa Rais baada ya kifo cha Magufuli pia alimpigia simu Samia kumpongeza.

Hakika Lissu si mtu wa mchezomchezo.
 

Umewakumbusha wenzako kuwa mna jambo lenu Magomeni Leo?



Au ndiyo kusema si Jilala Country Mtambuka wote mmemtelekeza kipenzi chenu ila Lissu au Chadema tu anayewakosesha usingizi?
 
Kila mwenye akili timamu analijua hilo !!
 
Mbowe aliagiza kupigwa Risasi kwa Tundu lisu mjini Dodoma
 
Maa
Maana yake nini,unajua Jo,vichwa viwili vinavyo charge sawa vimejikuta pamoja na ndio siri ya chama pendwa kwa wananchi wa Tanzania,hata vigagula wote wanaungana kuona ni jinsi gani walishusha chama hiki,ila walisha nyoosha mikono kubwa hawawezi😂
 
Tunachotakiwa tujifunze ni kuwa Rais Samia Suluhu ni Rais wa watanzania wote na sio Rais wa chama kwaiyo Lissu ni mtanzania ndio maana Rais Samia Suluhu alimuhakikishia usalama watanzania tuna bahatiu sana kuwa na kiongozi anaejali usalama wa wananchi wake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…