Makamu mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA Tundu Lissu ambaye pia ni mgombea wa nafasi ya uenyekiti katika chama hicho amesema hawezi kutoboa kuanzisha chama kipya kwa sababu wahusika wa usajili wa vyama vya siasa nchini hawawezi kukubali kutokana na kile kinachodaiwa kuwa Lissu ni mgumu na mkweli kupitiliza.
Lissu ameyazungumza hayo katika kipindi cha Clouds 360 kinachorushwa na kituo cha televisheni cha Clouds TV ambapo mahojiano hayo yamefanyikia nyumbani kwake Tegeta jijini Dar es Salaam.
Mungu hawezi kukuokoa na kifo cha kikatili ukapona risasi 16, ili uwe mwanachama wa kawaida wa CHADEMA basi na uishi maisha simple tu na uendelee kukaa na mkeo na watoto wako nyumbani