Tundu Lissu, unakuwaje Rais wa nchi bila kukemea Rushwa, bila kuongelea suala la maji, miundombinu na Elimu?

Lissu hafanyi kampeni, anatangaza nia, nyie mnaotaka aongelee maswala yote yanayowakumba watanzania hivi matatizo yenu ni mangapi? mnadhani yatamchukua nusu saa tu kusummarize matatizo yote? Hakutakiwa hata kuongelea matatizo yoyote jana zaidi ya kutangaza nia tu na kuondoka.
 
Yani Lisu atoke kutangaza nia baada ya masaa machache Mbowe avamiwe?

Tena avamiwe saa saba usiku alikuwa anatoka wapi?
Kuna dalili ya Lisu kutengenezewa tukio la kufunikwa hapa .

pole sana Mh Mbowe.
 
Ngoja tuone Jiwe safari hii ataahidi kupunguza bei ya mfuko wa cement toka Tsh9000 aliyotuahidi watanzania mwaka 2015 kwenye kampeni
 
Hiki ndo kile kikundi cha kikabila cha gwajima na bashite.
HAKUNA KM LISSU. Watz wanamtaka LISSU sio mtu anayeunda jamhuri ya watuwa chato. Mnamsifia mtu ambaye hasifiki ila kwasababu ya kutafuta vyeo tu
 
Nimeshtushwa sana tena eneo analotoka yeye Singida ni eneo guswa sana na Tatizo la maji...
 
Kitengo cha kubwabwaja na kuropoka ndo kinamfaa,ila sio Urais wa nchi.
 
Huja muelewa labda.....Ameongea vitu vichache alikuwa anatangaza nia tu..... kwenye kampeni ndio ataongea kila kitu hadi kuhusu mama ntilie bodaboda na etc.....
JUST BE CALM AND STAY TUNED
 
Mleta mada una hoja hotuba ilitakiwa kuwa manifesto yake ya uchaguzi ajikite atakavyo shughulikia huduma za jamii,miundombinu nk na uchumi atatumia mfano mbinu ipi.kuongeza mapato ya nchi nk hotuba yake ilikuwa too shallow akiongea Kama mwanaharakati zaidi kuliko mwanasiasa anayetaka utawala

Hakutakiwa speech kujaa attacks kwa serikali ,bunge na mahakama Hivyo vyote Ni ruling tools bunge Ni watawala, mahakama watawala,serikali watawaka .Alijikita kwa watawala badala ya wananchi walio wengi ambao wanahitaji maji,miundombinu,vituo vya afya ,elimu Bora nk wanavyovihitaji hakugusa!! Mgombea uraisi wa ajabu! Asiyejua wananchi wanahitaji Nini anajua tu vile bavyo bunge,mahakama na serikali wanahitaji.Very fun

Ile hotuba ukiiitizama Ni hewa tupu haina kitu
 
Mambo ya Muhimu kama
Elimu, Uchumi, ukwepaji wa kodi na Rushwa
Usimamizi wa rasilimali n.k hajagusa
Hotuba ilikuwa dhaifu. Natamani kama akipange atoe labda nyingine.
Lisu kichwani hamna kitu Ni kama samaki ukimtoa kwenye maji ukamuweka nchi kavu anaishia.Na Lisu ukimtoa kwenye fani ya sheria huku Kwingine kichwani Ni mweupe kabisa.Hayo ndiyo alitakiwa kuongea lakini Wala akawa anaendea kubwabwaja anavyoviota kichwani mwenyewe
 
Hehehe,
Jibu lepesi tu ni kwamba, lisu alikuwa anatoa hotuba ya kutangaza nia yake na akataje machache anayoamini yamekosa tiba, hvyo yanamsukuma kuuomba uraisi ili ayarekebishe,.ila haikuwa hotuba ya kampeni wala ya kuomba kura ndo maana kaongea ki ujumla tu,

Swala LA kusema hataji maji, umeme, sijui barabara hayo ni mambo ya wakati wa kampeni na huongelewa maeneo husika,
.yaan akienda mkoa wenye shida ya maji basi atawaahidi maji, maana sio kila mkoa una shida ya maji, umeme na mengine kadhalika

Kwa hyo wana ccm msipate shida, ila ya Jana ilikuwa na briefing tu ya kutangaza nia


Ila kampeni zikianza ndo tutaanza mizania mnazoleta sasa.

Asante.
 
Wewe boya ile alikuwa anatangaza nia ya kugombea tu wala hata hajapitishwa na Chama chake kugombea au uliambiwa ile ilikuwa ilani ya uchaguzi?
 
Yani Lisu atoke kutangaza nia baada ya masaa machache Mbowe avamiwe?

Tena avamiwe saa saba usiku alikuwa anatoka wapi?
Kuna dalili ya Lisu kutengenezewa tukio la kufunikwa hapa .

pole sana Mh Mbowe.
Kazi ya uvccm hiyo
Your browser is not able to display this video.
 
Chadema mnatia huruma kwa hiyo ukifika mkoa unauliza mna shida gani wakwambie Halafu unasema nitatatua !!! Uko too shallow .Nini utafanya yanakuwa kwenye Ilani yako ya chama ya uchaguzi huendi tu kule unasubiria waseme

Hotuba yake ilitakiwa aisome Kama ilani yake ya Ugombea kuwa atashughuliaje kero kwa hiyo hazijui anasubiri apitishwr atajulia mbele kwa mbele huko huko mikoani akiwa kwenye kampeni? Huo Ni utapeli wa kisiasa

Heri hata angeongelea ilani ya chadema. Kuwa nitaisimamia ilani ya chama na kuainisha maeneo ya ilani

Yeye hata ilani tu ya chadema hakuitimia anatunga yake tu kichwani utadhani ni.mgombea binafsi asiye na chama angeitumia hata ilani tu ya chadema angegusia hayo mambo lakini Hana mpango wa kujua ilani ya chadema Wala kuitumia anaeleza tu anavyoota ambayo hata kwenye Ilani ya chadema havimo.
Kamata ilani ya chadema Halafu linganisha na hotuba ya mheshimiwa mtaka kuteuliwa vitu viwili tofauti !!! Anabwabwaja ya kigombea binafsi badala ya ya kwenye Ilani ya chama chake.Chadema waambieni Hawa wagombea uraisi hewa watumie ilani mnatia aibu ona Lisu alivyotia aibu
 

We unahisi muda wa kutamka ayo ilikuwa jana?? [emoji16][emoji16][emoji16][emoji16] ila MATAGA kweli kazi ipo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…