Tunduru: Mauaji ya madereva bodaboda yaongezeka, hofu yatanda

Tunduru: Mauaji ya madereva bodaboda yaongezeka, hofu yatanda

kumusoma

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2014
Posts
567
Reaction score
893
Hofu imetanda katika wilaya ya Tunduru , kutokana na Mauaji na kutekwa kwa vijana waendesha boda boda.

Taarifa kutoka mjini Tunduru zinasema , vijana wa bodaboda wamekuwa wakipotea baada ya kukodiwa na watu, wanaojifanya wanakwenda vijiji vya mbali na Tunduru.

Katika tukio la hivi karibuni kijana mmoja alikodiwa na watu wasiojulikana tarehe 12/8/2022.Na baadae mwili wake ulikuja kuonekana maeneo yanayoitwa Nandembo ,akiwa amefariki.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, vijana kadhaa wameshapotea katikati ya mwezi wa saba na nane mwaka huu na bado hawajaonekana. Vitendo hivyo vya kikatili kwa vijana hao wadogo waendesha bodaboda vinahusishwa na wizi wa bodaboda hizo ,ambazo inasemekana zimekuwa na soko kubwa katika nchi ya jirani ya Msumbiji. Wauaji hao, Mara baada ya Mauaji hayo uondoka na boda hizo na kuzipeleka huko Msumbiji ambako Kuna soko kubwa. Pia kumekuwa na taarifa kwamba boda hizo hutumiwa kutengeneza injini ya boti katika nchi hiyo.

Wakazi wa wilaya hiyo wamemuomba mkuu wa wilaya na jeshi la polisi kuchukua hatua kali za kuzuia Mauaji hayo au waagize jeshi la polisi kutoka makao makuu ili waje kufanya uchunguzi .
 
Usishangae kusikia traffic wakimlaumu Kinana.
 
Hofu imetanda katika wilaya ya Tunduru , kutokana na Mauaji na kutekwa kwa vijana waendesha boda boda.

Taarifa kutoka mjini Tunduru zinasema , vijana wa boda boda wamekuwa wakipotea baada ya kukodiwa na watu, wanaojifanya wanakwenda vijiji vya mbali na Tunduru.

Katika tukio la hivi karibuni kijana mmoja alikodiwa na watu wasiojulikana tarehe 12/8/2022.Na baadae mwili wake ulikuja kuonekana maeneo yanayoitwa Nandembo ,akiwa amefariki.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, vijana kadhaa wameshapotea katikati ya mwezi wa saba na nane na bado hawajaonekana.

Wakaazi wa wilaya hiyo wamemuomba mkuu wa wilaya na jeshi la polisi kuchukua hatua kali za kuzuia Mauaji hayo au waagize jeshi la polisi kutoka makao makuu ili waje kufanya uchunguzi .
Labda wa Msumbiji wamerudi tena. Vyombo vya Ulinzi lazima waifanyiyekazi taarifa hii kwa haraka sana.
 
Ni jambo baya sana kuuana.Pamoja na ujahili huo,vijana wetu wapendwa waendesha boda wajifunze kuwa wasafi,wakimya,wasiri,wenye ubongo uliochangamka na wasomi wa mazingira.Ni jamaa,ndugu na watoto wetu.Wasipende kumuamini kila mteja.Na upande wa wateja wauaji ni kwamba walaaniwe na kufa kibudu.Sensi sao!
 
Swali!wanauwawa na kuacha bodaboda,au bodaboda pia zinapotea

Ova
Ila umasikini wa akili ni kitu mbaya sana.Unaweza kukuta ni kweli muuaji anafanya yake ili achukue boda ya milioni moja.Umasikini kummmnna?
 
Kubwa ni injini za boti...tena sio pikipiki zote....wakikamatwa wabinywe pumbu waseme wanakouza
 
BIASHARA YA BODABODA INA PESA NDOGO NDOGO NYINGI.
NA HII INAWAFANYA VIJANA KUWA NA JEURI YA KUHUDUMIA WAKE ZA WATU.
UNAKUTA KIJANA NA ANAUWEZO WA KUNUNUA NUSU KILO YA NYAMA KILA SIKU KWA MKE WA MTU KULIKO MWENYE MKE.
WENGI WANAPOTEA KWA SBB YA VISASI, HII YA KUIBA PIKIPIKI NI NAMNA YA KUPOTEZA USHAHIDI.
 
BIASHARA YA BODABODA INA PESA NDOGO NDOGO NYINGI.
NA HII INAWAFANYA VIJANA KUWA NA JEURI YA KUHUDUMIA WAKE ZA WATU.
UNAKUTA KIJANA NA ANAUWEZO WA KUNUNUA NUSU KILO YA NYAMA KILA SIKU KWA MKE WA MTU KULIKO MWENYE MKE.
WENGI WANAPOTEA KWA SBB YA VISASI, HII YA KUIBA PIKIPIKI NI NAMNA YA KUPOTEZA USHAHIDI.

Sijawahi kuwaza hili ila linawezekana pia kwa wivu wa mapenzi
 
Back
Top Bottom