Tungekomaa na Ujamaa bila kuikumbatia SAP labda sasa hivi tungekuwa mbali

Fafanua sap ndio nini wengine atuijui
SAP ni ufupisho wa maneno matatu ya kiingreza. S:-stands for Structural, A:-stands for Adjustment and P:- for Program.So, in its full form SAP ni Structural Adjustment Program.Kiufupi ni kwamba IMF na WB walifanya mabadiliko katika namna ya kutoa mikopo kwa mataifa ambayo uchumi wake ulikuwa ukipitia kipindi kigumu baada ya kutokea oil crisis,drought nadhani na fall of the USSR.

Nchi ilibidi ziwe zimekidhi vigezo vilivyowekwa ili kupatiwa mkopo.Moja ya vigezo nadhani ni kuruhusu ushindani katika nyanja za kiuchumi,kijamii and etc(I mean to end state monopoly). Kwa ufupi ni hivyo sema ukitaka kupata ufahamu zaidi, I guess you need to consult google.
 
Ujamaa ndiyo umetufikisha hapa. Sikiliza hapa

 
Halafu ukiacha ujamaa tukakimbilia kujiunga na Non Aligned Movement (NAM) ambayo hatukujua maana yake ni nini tumebaki watembeza bakuli kama Malaya tu kisa hatufungamani na upande wowote wakati wenzetu waliingia NAM wakatumia siasa ya kujitegemea wakakuza uchumi wao vizuri kwa kutumia rasilimali zao na wataalamu wao sisi tunabaki na NAM kama mazuzu tu.
 
Soko huria
 
Ujamaa ulishindwa na Nyerere mwenyewe alikiri.

Ujamaa wa Nyerere aliutengeneza mwenyewe na hakuambilika juu ya namna ya kuuendesha. Ulikuwa ni Ujamaa wa kutafuta wahanga na watu wa kuwaangushia jumba bovu. Kuanzia Utaifishaji wa Mashirika na viwanda, Uanzishaji wa Vijiji vya Ujamaa, Operesheni maduka nk.

Ujamaa haukuwashirikisha Wadau Bali mtu mmoja au,kikundi cha watu ndiyo waliamua nini kifanyike. Hata pale wananchi walipoungana kuunda ushirika wao wa kijamaa walivurugwa kama ilivyotokea Ruvuma Development Association.

Sera za SAP hazikuwa mbaya na si kwamba ndiyo zimetukwamisha, zile zilikuwa sera za waliozitunga na ambao walitoa fedha. Tungekuwa na Uongozi wenye maono hiyo ingekuwa chachu ya kujikwamua zaidi.
 
Jaribu kukutana na raia wa nchi zilizokumbatia ujamaa hadi leo uone mateso wanayopitia. Nimeishi na kufanya kazi na waCuba yaani ni majuto. Wanalipwa mishahara lakini hawezi hata kutuma hela nyumbani, hela yake anabaki kuitumia huku huku. Au apitishie kwa dalali, dalali ndo aka withdraw hiyo kwa malipo fulani ndo aifikishie familia. Imagine watu wanananua mpaka tomato sauce huku tz na kutuma Cuba kupitia njia za panya.

Huo ujamaa bora ulijifia tu, sisi tulioonja hayo maisha ilikuwa ni zaidi ya mateso, nakumbuka watu wakipanga foleni kwenye maduka ya ushirika ili kununua tu sukari, mtu analazimika kuweka jiwe kwenye foleni anaenda shamba akirudi sasa sita anakuta bado zamu ya kununua sukari haijafika.

Mtu anahitaji kununua bati lakini anaambiwa alipie bati tano tu, nyingine asubiri mpaka zitakapokuja tena kwa awamu nyingine.
 
Nchi hii ilianguka kiuchumi kisa ghiriba, usaliti, umamluki, vita ya kagera pia imo, external forces zililaghai viongozi wa ndani kwenye taasis na mashirika, nchi kama Kenya ilitumika na magharibi kuua uchumi wa nchi hii, na sisi tukawa na viongozi mapopoma tu, wanaiba cha ajabu wakishakufa familia zao hazina uwezo wa kustain umaridadi.

Micro and Macro forces, baada ya vita ya kagera tukawa viwete, omba omba, wakiwa ule ufrontier ukakosa maana, Magufuli alilijua hili na alikuwa analisema kwa uchungu kuwa nchi hii tulifanya upuuzi wa kuwatumikia wengine ambao hawana msaada wote.

E.g The kind of financial help we got from Mugabe was significant but not satisfying equivalent to our earlier sacrifice we devoted to Zimbabwe and many others.

Sasa hivi tunaishi ujamaa wa kiutopolo wa kuhalalisha aina flani ya ukoloni baina wenyewe kwa wenyewe, local/internal colonialism, makusudically or rather purposefully manipulated hegemonial powers.
 
Saidia kudadavua kwa mifano ya components za SAP namna gani uongozi bora ungeweza kutumia SAP kama catalyst ya kukua kiuchumi.
 
Ujamaa haujawahi kuleta maendeleo popote pale.

Tuomae tupate katiba nzuri, itakayowafanya wanasiasa (wabunge) kuwatumikia wananchi badala ya kutumikia serikali na matumbo yao. Ccm ndio adui mkubwa wa maendeleo nchi hii. Hawataki katiba mpya maana hi iliyopo inalinda maslahi yao na sio maslahi ya taifa. Na sio ccm yote Ila Ile 'top layer' inayokula keki ya taifa kwa uchoyo.

Kuna mtu aliwahi kusema ccm inaungwa mkono na watu mbumbumbu, kauli ile ikaonekana Kama yanye nia ya kudhalilisha. Jiulize kwanini ni vigumu ccm kushinda uchaguzi halali (ulio huru na wa haki) katika maeneo ya majiji na miji mikubwa, au mikoa Kama Dar, Mbeya, Iringa, Kilimanjaro, Kagera etc. Maeneo haya na megine kama haya wakazi wake wengi wamefunguka macho, tofauti na maeneo ambayo ni ngome za ccm
 
Kabla ya vita ya Kagera uchumi ulikuwa chini, tulikuwa masikini. Ukiona nchi inafilisika baada ya kupigana vita ya miezi 8 tuu basi hiyo nchi ni masikini. Na usilaumu external forces wakati Nyerere na wanamapinduzi wenzake walitumika na nchi za mashariki kama China kufanya mapinduzi Rhodesia na kuharibu uchumi wake.

Nyerere na wanamapinduzi wenzake wa Zanu na Frelimo waliibaka nchi yenye uchumi wa juu Rhodesia na kuanzisha yao inaitwa Zimbabwe. Kama kawaida, wana mapinduzi na wajamaa hawajui kuongoza nchi na kuinua uchumi. Matokeo yake mwanamapinduzi mwenzake Nyerere, Mugabe alikufa akawaacha wananchi wake masikini wa kufa na njaa. Hiyo ndiyo sumu ya Ujamaa.
 
Ukweli wa mambo ni kwamba ujamaa ndio ulitudumaza, tungekuwa mbali sana kama tusingepitia kwenye ujamaa.
 
Mwinyi yeye alifanya jambo gani la maana?
Alirudisha uchumi kwa wananchi,akafuta foleni za unga na ukosefu wa mahitaji muhimu,Uhuru wa habari,akaanzisha TRA ili avune mapato baadae ya kuwafundisha kufanys biashara
 
TRA alianzisha mwinyi 31/7/1995

Tanzania Revenue Authority (Mamlaka ya Mapato Tanzania)​

Government agency


Description​

Description​

The Tanzania Revenue Authority is a semi-autonomous Government Agency of the United Republic of Tanzania. It was established by the Tanzania Revenue Act, CAP. 339 in 1995 and started its operations on the 1st of July 1996. Wikipedia
Headquarters: Sokoine Drive, Dar es Salaam
Key document: Tanzania Revenue Authority Act, 1995
Jurisdiction: Tanzania
Founder: National Assembly
Founded: July 31, 1995
Kweli mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…