Tuongee ukweli: Soko la pesa la Tanzania (UTT, Hisa N.k) haliwezi kukufanya ukawa tajiri kwa mtaji wako mdogo

Tuongee ukweli: Soko la pesa la Tanzania (UTT, Hisa N.k) haliwezi kukufanya ukawa tajiri kwa mtaji wako mdogo

Kwani mfano UTT ni mifuko miwili tu ndiyo inatoa gawio hiyo mengine minne, haitowi gawio.

Hivyo siyo kila anayeweka pesa uko ni kwa lengo la kupata gawio, binafsi nimeweka umoja ili nikuze mtaji wangu sasa utasemaje UTT ni mbaya ??
Hizo zote ni product za UTT
Aidha zitoe gawio ulichukue au uliache Ila ni gawio.

Endeleeni kunidanganya na returns za kina Mirambo Holdings tuu.
Umri unaenda.

Anzeni kupenda risk mkiwa bado vijana.

#YNWA
 
Umeanza tena maswala ya kujidanganya, kaingia rostam hapa.
Nimehudhuria semina nyingi sanaa za kina UTT na UMOJA FUND
Tatizo lao Hua wanapiga Mifano ya mamilioni
Utasikia "kwa miaka 7 ukiweka mil 100 utapata Mil 170"

Sasa hiyo mil 100 anamzungumzia bodaboda au Miramb holdings?

#YNWA
 
INTRODUCTION.
Mr. Liverpool kwa maisha ni mfanyakazi, mfanyabiashara na mmiliki wa vipande kwenye mutual fund..

Nasoma(ga) sanaa watu humu wanasifia FOREX, Mutual Funds (hasa UTT), Government bonds and bills na fixed deposits.

BODY:-
Soko la pesa Tanzania sio kubwa kiasi kwa maana kuna hisa, vipande vya mutual fund, government bonds and bills, na fixed deposit.

Ila nachojiuliza ""Hivi kuna mtanzania mwenye kipato kidogo anaweza ishi vizuri kwa kumiliki chochote hapo juu?""

Kuna ukweli mwingi sanaa huwa hausemwi na wataalamu wa finance and investment, ""Je soko letu ni sahihi kwa watu masikini na kipato cha kawaida??""

SCENARIO:-
Mimi binafsi ni muwekezaji wa mutual fund inayoitwa FAIDA FUND inayosimamiwa na Watumishi Housing kupitia Wizara OR - Tamisemi.
Nina vipande 25,768.9364 nilivyoanza ununuzi tokea June/2023.

Lakini pia nina biashara kubwa tu mjini yenye mtaji wa Mil 40 na assets za mil 15.

PROBLEM.
Changamoto ya soko letu la pesa ni faida yake ambayo ni ndogo sanaaa...
1. Nilishawahi miliki hisa za Vodacom na CRDB, nilikaa nazo mwaka na nusu, ilinichukua miezi mitatu kuziuza. Hiki ndicho kilichonikera balaa na kuachana na mambo ya hisa.
2. Nikaingia UTT Amis, wale jamaa walikaa na pesa yangu mwaka wakanipa 100k kama Faida..!!
3. Nikaingia kwenye forex nako nikapigwa 200 dollar yoteee (kupitia IQ Option).
4. Nikawaza Crypto currency ila sikushiriki.

Wakati nateseka na money market nilikuwa tayari nina hii biashara iliyoanza kwa mtaji wa mil 10 (bidhaa Mil 5 na Assets 3 na maandalizi mil 2).

Wakati huo wotee biashara ilikuwa inakuwa na wateja wanamiminika Ila money market ilikuwa tu inasumbua na kuiweka hela yangu idle.

Nilivutiwa na money market kwasababu ya
1. Elimu yangu ya chuo, nimesoma Economics, Finance and Investment kwa Diploma, Bachelor na Masters yangu.
2. Ujana, kutaka kuwa tajiri
3. Kuona kazini napoteza muda.

Kwasasa nipo na FAIDA FUND tu japo naona performance yake inazingua tuuuu (slowly growing).

CONCLUSION:-
Kifupi soko la fedha la kibongo bado ni nogo sanaa na si salama kwa kijana mtafutaji.

Yaani, si rafiki kwa kijana ambae anajitafuta akapata mil 2 yake eti akawekeza ili atoke kimaisha, na ni tofauti sanaa na wenzetu.

Wenzetu ukisikia mtu anamiliki 1% ya hisa za facebook huyu ni tajiri balaaa, ila hebu nitafutie mtanzania anayemiliki kampuni 1% ya share akawa tajiri...!!!

ANYWAY:-
Mimi nipo FAIDA FUND kwasababu BONUS Account ya NMB imeshindwa kunipa nachotaka. Bonus Account ili upate interest inatakiwa upambane hasaaaaaa.

Kwasasa nina mpango wa kununua fuso niwe napeleka mizigo kijijini, hivyo nawekeza FAIDA FUND ili ikifika hela ya bei ya fuso basi nitoe ninunue hiyo gari iingie mzigoni...!!!

Hivyo FAIDA FUND naifanya kama bank account ya malengo yangu..!! ila sio NJIA YA KUNITOA KIMAISHA.

Na kiukweli:-
1. Money market ya bongo ni kwa ajili ya watu waoga na wasio na muda wa kufanya biashara Ila nyie wenye mioyo migumu NJOONI KWENYE BIASHARA TUPAMBANE.
Biashara ina hela balaaaaa.

2. Money market ya bongo ni kwaajili ya matajiri tu, yaani jitafutee kwenye biashara halafu "diversify your portifolio" kwa money market, Ila sio eti umepiga deal la mil 5 halafu unaingia money market ili Uwe tajiri, aiseee HAIPO.

Watakaokwambia biashara ni high risk hebu....
1. Waulize kuhusu hisa za NICO, JATU, TOL
2. Waulize kuhusu Vodacom, waliingia DSE kwa 1000/share ghafla wakashuka mpaka 800/share..!!
3. Waambie hivi, watokee watu wawili wasio na ajira wote wapewe mil 5 each, mmoja aende UTT na mwengine aende Kariakoo kuwa winga halafu baada ya mwaka tuje na mrejesho.

Tuendelee kutafuta pesa.

#YNWA
Kuna ukweli soko la mitaji Tanzania ni dogo sana kumbukeni tupo third world country najua Watanzania wengi hawataki kukubali hili lakini hii Nchi ni maskini kwenye dunia Bakhressa na Mo ni maskini. Hata hivyo kwa maisha ya kitanzania naona T/bonds zina afadhali kidogo pia msiogope kwenda kuweka pesa kwenye masoko mengine kama ya Kenya, Botswana na SA. Mkiweza nendeni hata Asia, Ulaya na US. Pia ndugu yangu Mtaji wa mil 40 siyo biashara kubwa usitosheke mapema.
 
Nimehudhuria semina nyingi sanaa za kina UTT na UMOJA FUND
Tatizo lao Hua wanapiga Mifano ya mamilioni
Utasikia "kwa miaka 7 ukiweka mil 100 utapata Mil 170"

Sasa hiyo mil 100 anamzungumzia bodaboda au Miramb holdings?

#YNWA
Umehudhuria mikutano mingi ya UTT na Umoja fund.
Umeudhuria mikutano ya wapi? Ipi?
Na kwanini waelezale vitu hivyo. Ndugu mimi ni kijana mdogo sana, ila hapa unanidanganya. Matapeli ndio uongea hivo, yaani mkutanoni upewe kauli ya hivo. Acha bwana. UTT asset management na investor service hawafanyi vikao vya kihuni hivo.
Na kila mwaka wanatoa taarifa ya liquid fund yako mwaka jana wametoa november. Haiwi kihuni hivo boss. Embu tulia si kila kitu cha kuropoka hadharani
 
Umehudhuria mikutano mingi ya UTT na Umoja fund.
Umeudhuria mikutano ya wapi? Ipi?
Na kwanini waelezale vitu hivyo. Ndugu mimi ni kijana mdogo sana, ila hapa unanidanganya. Matapeli ndio uongea hivo, yaani mkutanoni upewe kauli ya hivo. Acha bwana. UTT asset management na investor service hawafanyi vikao vya kihuni hivo.
Na kila mwaka wanatoa taarifa ya liquid fund yako mwaka jana wametoa november. Haiwi kihuni hivo boss. Embu tulia si kila kitu cha kuropoka hadharani
Hutakiwi kujibizana na watu wapumbavu mkuu. Save your Energy please..huyo hayupo tayari kuelewa
 
Kwa mfano wangu huohuo
Kuna utofauti Kati ya Compound interest ya Mkurugenzi/boss wako na mdada wenu wa kazi.

Jikite kwenye mada, hebu tengeneza schedule ya house girl kuwa tajiri kwa hizo compound interest akiwa na miaka 25.

Usisahau LIFE SPAN yetu.

#YNWA
Tafuta watu wakujibu mkuu kuna watu hawana finance literacy just ignore, watakutoa kwenye mada yako, ni wacheche wa kuelewa tu, mke wangu alinunua hisa NmB za 2m miaka 15 nyuma lakini mpaka leo hajawahi kupokea hata 500,000 kwa mwaka mimi nilio wekeza kwenye biashara ndo nimemuajiri tena... Finance market haowezi kutoa mtu kwenye umasikini ila inaweza kuendeleza wenye nacho sio masikini
 
Nilishasema humu kitambo, hizo biashara za UTT na bonds ukitaka uone pesa walau uwe na 500M ama zaidi ya hapo. Otherwise wenye hizo million 5 mpaka 10 fanyeni uchuuzi tu. You will make more money that way kuliko kusubiria gawio la laki hadi laki 5 mwisho wa mwaka.
Ukishakuwa na cash 500 millions huwezi kubali kuweeka pesa yako kwenye faida ndogo kama hiyo ya Utt
Kiufupi labda uwe na pesa zilizopatikana kwa wizi na deals huko serikalini au uwe mstaafu uliyelipwa billions.
 
unauhakika kozi ulisomea uchumi mkuu? compounding interest unaielewa vyema inavyo piga kaz there is no wonder ulipigwa forex inaonekana unapenda utajir wa chap kitu ambacho kimewaponza kina meek mill
Boda boda anawekesa kiasi gani Utt ili naye aishi kibos akistaafu.?
Mada ni simple tu, unaicomplicate! Soko la pesa Sio kwa kila mtu in fact ni kama lipo kwa ajili ya matajiri tu. Haiingii akilini niweke 10 mil Utt halafu nisubiri faida ya 1 mil baada ya mwaka! Ila tajiri anaweza subiri gawio la 100mil kwa mwaka kama kaweka 1 billion utt.
 
Nimehudhuria semina nyingi sanaa za kina UTT na UMOJA FUND
Tatizo lao Hua wanapiga Mifano ya mamilioni
Utasikia "kwa miaka 7 ukiweka mil 100 utapata Mil 170"

Sasa hiyo mil 100 anamzungumzia bodaboda au Miramb holdings?

#YNWA
Wako sahihi kupigia hio mifano maana hao ndio targets wao! Wewe bukuonaire na lakionaire mkae pembeni😂
 
Ukishakuwa na cash 500 millions huwezi kubali kuweeka pesa yako kwenye faida ndogo kama hiyo ya Utt
Kiufupi labda uwe na pesa zilizopatikana kwa wizi na deals huko serikalini au uwe mstaafu uliyelipwa billions.
500m ni mtaji wa kuanzisha micro finance au credit facility nzuri tu katika semi urban area na kua na tellers wswili, kama loans za short period1moth to 6 months uki-charge kwa 22% intrest rate, ndani ya mwaka moja unaweza ukawa na annual turnover 1.5bn manaake kwa mwaka unaweza ukatengeneza faida ya 700m both in assets and cash.

Sasa kws watu wanao jua finance banking kwanini uweka pesa yoko kwenye marketing Finance, labda kama ya wizi au betting.
 
Umehudhuria mikutano mingi ya UTT na Umoja fund.
Umeudhuria mikutano ya wapi? Ipi?
Na kwanini waelezale vitu hivyo. Ndugu mimi ni kijana mdogo sana, ila hapa unanidanganya. Matapeli ndio uongea hivo, yaani mkutanoni upewe kauli ya hivo. Acha bwana. UTT asset management na investor service hawafanyi vikao vya kihuni hivo.
Na kila mwaka wanatoa taarifa ya liquid fund yako mwaka jana wametoa november. Haiwi kihuni hivo boss. Embu tulia si kila kitu cha kuropoka hadharani
Wizara ya fedha ikiwa na semina Dodoma kwa watumishi, huwa wanaalikwa hao UTT na FAIDA FUND Kuja kutoa elimu.

Ila tuishie hapo.

Okey ma - investor, investment is the marathon not a race.
🤣🤣🤣🤣
Angalieni isije ikawa ni race mnakimbizana na wakenya..!!

Anyway:-
Karibuni kwenye biashara
Risk Lovers, YESS WE ARE.

#YNWA
 
Matumizi ya wakati huo ni pamoja na magonjwa ya uzeeni yenye gharama, kurepair etc. Bora kupata 160K ukiwa kijana kuliko hiyo na matumizi kuwa makubwa ya uzeeni. Usisahau wakati huo hata watoto wazuri unakula kwa macho na michepuko haikubali kuja kwa Bus bali ndege.
Utaipataje ukiwa kijana wakati babaako hana influence yeyote chamani😂
 
500m ni mtaji wa kuanzisha micro finance au credit facility nzuri tu katika semi urban area na kua na tellers wswili, kama loans za short period1moth to 6 months uki-charge kwa 22% intrest rate, ndani ya mwaka moja unaweza ukawa na annual turnover 1.5bn manaake kwa mwaka unaweza ukatengeneza faida ya 700m both in assets and cash.

Sasa kws watu wanao jua finance banking kwanini uweka pesa yoko kwenye marketing Finance, labda kama ya wizi au betting.
Hio 22% unayopigia hesabu ni kwa hawa hawa wabongo naowajua mimi au utaifanyia maeneo ya Norway?😂
 
Pia ndugu yangu Mtaji wa mil 40 siyo biashara kubwa usitosheke mapema.
Sijaridhika ndio maana ya kununua FUSO.
Nanunua Fuso kwasababu kuna "Market share" Nimeiona sehemu hivyo naona ili kuipata linatakiwa FUSO.

Kwahiyo hii plan tu ya kununua FUSO ni kwamba Ninataka kukuza biashara.

#YNWA
 
Mada ni nzuri ila nimesoma kama comments 20 za mwanzo naona wengi wanashindwa kutofautisha biashara na uwekezaji. Kwenye biashara always tunategemea faida ya haraka lakini uwekezaji faida ni ndogo inayoweza chukua muda mrefu. Hizi UTT na Gov Bonds wanauchumi wakubwa wanaziita ni securities.

Kwahiyo unapoweka hela UTT means unafanya kwa ajili ya ulinzi wa pesa yako lakini ukitegemea kwa matumizi ya baadae. Mfano wewe mleta mada unasema unatunza pesa UTT ili uje ununue tipper tofauti na kwamba hii pesa ungekua umeiweka bank tu. Lakini neno security linakuja ku apply zaidi pale utakapo chukulia mkopo manunuzi ya tipper badala ya kununua cash. Hivyo UTT inabaki kukulinda hata pale majanga yatakapo tokea.

Ni kweli kwa nchi kama yetu hizi faida yake ni ndogo lakini bado zinasimama kama the best securities kwa waTZ wengi kulinda pesa zao. Kwa nchi nyingine wanafaidika sana kutokana na nchi hizo kuwa stable kiuchumi.
 

Attachments

  • Screenshot_20220922-124152.png
    Screenshot_20220922-124152.png
    120.6 KB · Views: 37
Wizara ya fedha ikiwa na semina Dodoma kwa watumishi, huwa wanaalikwa hao UTT na FAIDA FUND Kuja kutoa elimu.

Ila tuishie hapo.

Okey ma - investor, investment is the marathon not a race.
🤣🤣🤣🤣
Angalieni isije ikawa ni race mnakimbizana na wakenya..!!

Anyway:-
Karibuni kwenye biashara
Risk Lovers, YESS WE ARE.

#YNWA
Boss investing is not getting rich, getting rich is a result
 
Back
Top Bottom