Tuongee ukweli: Soko la pesa la Tanzania (UTT, Hisa N.k) haliwezi kukufanya ukawa tajiri kwa mtaji wako mdogo

Tuongee ukweli: Soko la pesa la Tanzania (UTT, Hisa N.k) haliwezi kukufanya ukawa tajiri kwa mtaji wako mdogo

s
hilo ndio kosa tunalolifanya wengi hii ni kwaajili ya kizaz chako na unatakiwa uwafundishe watoto wako wajue kabisa na wao waendeleze hio knowledge kwa watoto hii ni njia ya kupambana na umasikin kwenye kizaz chako wenzetu wazungu wanakitu wanarithishanaga kinaitwa trust fund ambapo babu la mababu ndio lili invest kitambo inabak inaendelea kwenye generations sis huku tunarithishana magari na manyumba
Naam mkuu. Tunatakiwa ku break generational poverty. Tudundulize kidogo kidogo,wanufaika wawe watoto wetu na wajukuu.
 
Umeelewa nilichoandika?
Anyway:-
Nimekwambia Niko na masters, Bach ma dip unadhani kuna neno la kwenye makaratasi SILIJUI?

Hata hivyo, umesema kuhusu ""Making money while sleeping"" Ila chakukushauri, hakikisha kwanza Una active income nyingi then ndio uingie hizo passive income.

Kuna tajiri huko anamiliki hisa za FB, Apple na nyengine kwa asilimia 3 tu, Ila kwa bongo MONEY MARKET BADOOO SANAAAAA.

#YNWA
🤔🤔🤔🤔🤔
 
mkuu UTT wana calculator yao ukiweka 150,000 kila mwez kwa bila kuwithdraw kwa miaka 30 unsish na zaid ya milion mia nne hii knowledge watu wanalipiaga hela tuko hapa tunabishana kipimbi after all ku save 150,000 kila mwez kwa 30yrs is not for beginners inahitaji constancy na discipline so sio utajir mrahis pia
Miaka 30 ijayo value ya million mia nne si itakuwa sawa na 4/40 millioni tu ?
 
Mleta mada umezungumza mengi hapo kuhusu soko la pesa la Tanzania ukidadavua vyema kuhusu HISA,vipande na bond za serikali.. ..

Nimejaribu kufikiri kitu kimoja kwa sasa umeamuwa kuwekeza kwa kununua vipande vya FAIDA FUND baada ya kutapatapa huku kwingine..Kuna mifuko ya UTT AMIS inatoa gawio sawa au zaidi ya FAIDA FUND sasa nashindwa kukuelewa UTT unawapondea nn akati ndoo vile vile Jielimishe zaidi elimu ni bahari


Jambo la msingi zaidi katika elimu yako nikukumbushe ni kuwa Ili upate pesa zaidi unatakiwa uiwekeze zaidi katika sehemu mbalimbali Ili upate zaidi.Watu wanapowekeza wanakuwa na malengo ya muda mrefu na hata kabla ya kuwekeza katika hizi sehemu wanasisitizaga Sana "ELIMU ELIMU ELIMU" Kwamba kama ni mpambanaji sio kwamba hela yako yoote ndo utaiweka huku lazima uwe na shughuli kadha wa kadha za kukuingizia kipato .Pia ni bora kuweka huku hela usiyoitumia iongezeke thamani kuliko ikae nyumbani au benki tu inapopungua thamani (Makato, inflation)

MWisho unapokua na maono juu ya jambo fulani lenye manufaa kwako usiyumbishwe na mafanikio ya wengine badala yake jifunze na Ishi kulingana na mazingira yako .Kuwafikia kina Warren Buffett n.k Ni ngumu hivyo tufanye kulingana na uwezo, kipato na mazingira yetu hata kama ni kidogo ila chenye manufaa ni kizuri.
 
Deni la Taifa ni takribani Tsh 87 trillion...
Mikopo ya Ndani ni takribani 40 trillion...
Wakopeshaji wakubwa wa serikali ni Mabenki na Waarabu na Wahindi wa Bongo...
NMB na CRDB zinapiga faida ndefu kwa kuikopesha serikali kuliko mikopo ya biashara.
Kwa kukosa elimu ya uwekezaji,tumeweka rehani uchumi wetu mikononi mwa wahindi na waarabu...ambao wao ndiyo wafaidika wakubwa...
 
Watu wengi sana hatuna elimu ya haya mambo na ndio maana zinazalishwa zana nyingi sana za ajabu ajabu kama hizi

Shemeji yangu alifariki akaacha kama milioni 600 bank
Alikua na mke na watoto mapacha wawili.
Ukoo ulivutana sana nini kifanyike kuhusu na hizo hela

Mimi nikawashauri hela iwekwe Fixed acc bank iwe inatoa hela ya kujikumu hadi baadae tukitulia tutajua cha kufanya
makaka wakapinga sana kuwa huwezi kulaza hela nyingi hivyo bank ni UZEMBE

Mwisho wa siku ikaamuliwa
Mama mzazi apewe 50M.
Makaka 2 wapewe 100M wazungushe hela hadi watoto watakapo kuwa watu wazima
Mke wa marehemu akapewa 100M aanzishe biashara ya kujikimu
Halafu 300M ndio iwekwe fixed acc, rate yake ilikua 9.5%
Hapo kwa mwaka faida ni 28,500,000 na ikawa inagawanywa kwa miezi 12 ili ichukuliwe kila mwezi 2.3M

Baada ya mwaka tu mke wa marehemu biashara zake zote chalii 100M ikapotea.
Makaka wa marehemu ndio kabisa sijui walikwenda kununua mazao ikakatika 100M yote.

Sasa hivi familia ya marehemu wanaishi kwa kupokea 2.3M kila mwezi ya ile 300M kwenye fixed Acc, ndio pona pona yao vinginevyo wangeanza kuuza mali za marehemu
Watoto ndio kwanza wana miaka 10
Limepita AZIMIO hiyo hela asiguse mtu yeyote ibaki huko huko fixed Acc hadi watoto watakapo kwa watu wazima
Nyinyi ni Kabila gani? Kaka anaingiaje kwenye urithi wakati urithi ni wa mke na mtoto?

Huyo mke hajitambui kabisa, Kaka anaweza kuwa msimamizi wa mirathi tu na siyo mnufaika otherwise kuwe na wosia wa marehemu Kwa mwanasheria.
 
Naungana na wewe.
Kijana tumshuri na atumie mifuko kama Sehemu ya kuhifadhia hela.kuliko kuweka benk ambapo haimletei faida hata kidogo. Akitunza hela kwa mwaka huu anunue shamba mwakani anunue kiwanja. Na vile vyake vingine aweke utt Ili hata ikitokea dharula anaweza akauza Sehemu ya vipande vikawa hela baada ya siku 3.
1.Je,kuna tangazo lolote limeshawahi kuwepo kuhimiza watu watatajirika kwa low risks financial markets...

2.Kuna umuhimu wa watu kuwa na uelewa wa financial markets ili kusambaza vipato vyao...
 
Kuna ukweli soko la mitaji Tanzania ni dogo sana kumbukeni tupo third world country najua Watanzania wengi hawataki kukubali hili lakini hii Nchi ni maskini kwenye dunia Bakhressa na Mo ni maskini. Hata hivyo kwa maisha ya kitanzania naona T/bonds zina afadhali kidogo pia msiogope kwenda kuweka pesa kwenye masoko mengine kama ya Kenya, Botswana na SA. Mkiweza nendeni hata Asia, Ulaya na US. Pia ndugu yangu Mtaji wa mil 40 siyo biashara kubwa usitosheke mapema.
Hayo masoko ya nje mnawekezaje ??
 
Nyinyi ni Kabila gani? Kaka anaingiaje kwenye urithi wakati urithi ni wa mke na mtoto?

Huyo mke hajitambui kabisa, Kaka anaweza kuwa msimamizi wa mirathi tu na siyo mnufaika otherwise kuwe na wosia wa marehemu Kwa mwanasheria.
Mkuu ni story ndefu
Kuifupisha ni kwamba mama wa nyumbani si unawajua tena
Jamaa wakaja na wazo kwamba wafungue kampuni kuendelea kuzungusha hela ya marehemu hadi watoto watakapo kuwa watu wazima wakute mradi umeongezeka na mahela kibao waje kurithu kuliko kuilaza tu hela bank
Wenye akili tulijua ila hatuna sauti tukapiga kimya
 
Mkuu ni story ndefu
Kuifupisha ni kwamba mama wa nyumbani si unawajua tena
Jamaa wakaja na wazo kwamba wafungue kampuni kuendelea kuzungusha hela ya marehemu hadi watoto watakapo kuwa watu wazima wakute mradi umeongezeka na mahela kibao waje kurithu kuliko kuilaza tu hela bank
Wenye akili tulijua ila hatuna sauti tukapiga kimya
Yani ufunguwe kampuni Kwa pesa za Marehemu?

Wabongo tuna matatizo Sana, au ni Wajita nyinyi?
 
Mr Liverpool kitendo cha kusema tu June 2023, uzi ulitakiwa uishie hapo.
Kitendo cha kusema IQ option ukafanya forex tena kwa dollar 200.
Hapo tu uzi wako ulitakiwa uishie. Nakushauri, endelea na biashara yako ya milioni 40
Doller 200 kidogo sana kwenye Forex ,.mwaka 2015 wakati naanza baada ya kupata mchongo huo kwa Mcanada niliteketeza dollar 2500 ya Urithi[emoji23][emoji23]
 
Kwa value ya pesa yetu kwa sasa millioni 100 ya 2000 enzi hizo ingefanya mambo makubwa kuliko ya 2024.

Si mtalaamu wa uchumi lakini.
huwa na wana include inflation kwenye calculations zao sana sana thaman inazid kuongezeka with time ngoja niingie class kabisa niwe certified guru nianze kutoa hii elimu bure kabisa
 
Back
Top Bottom