Tuongee ukweli: Soko la pesa la Tanzania (UTT, Hisa N.k) haliwezi kukufanya ukawa tajiri kwa mtaji wako mdogo

Tuongee ukweli: Soko la pesa la Tanzania (UTT, Hisa N.k) haliwezi kukufanya ukawa tajiri kwa mtaji wako mdogo

Ebu ni kujibu mwaka 2000, million 100 ungeweza kununua Fuso tipper engine 16 zenye carbin kubwa 5 na unabakiza balance kule Japan CIF ilikua $10,000 kodi TRA 2.5m exchange rate ilikua 1$ ni 1,100TZ shilling......sasa hivi 100m ya sasa unanunua fuso tipper mayaye au 16 moja tu mpaka Dar port 90 000,000 na unabakiza 10m ambazo zitaisha pia kwenye vibali na matayiri,.......kwahiyo hapa sio sehemu ya kuwekeza longtime investment inflation and unstable economic policies zina ua biashara, sasa hivi exchange rate ni 2300 kwa dollar moja mpaka december dollar itafika sh 3000 au zaidi pesa ya Tanzania inashuka kwa kasi na hamna vya shiria vya kiuchumu ku-recover huvi karibuni
Sijui Kama atakuelewa mkuu

Labda muulize hizo million mia angeweka utt Leo angekuwa na faida ya sh ngapi

Pia hiyo 2000 Dola moja ilikuwa 500tsh million 100
Sawa na Dola ngapi

Je Leo hiyo million 100 sawa na Dola ngapi ?
 
nahis BOT wanaelewa zaid yetu na ule mfuko upo chini yao tuache ujanjaujanja kwenye mambo ya kitaalamu ni kukaa na wataalamu na sio kutumia common sense kwenye mambo ya taaluma wao wanasemaga fact vs common sense
Bot wamejaa wstoto wa vigogo hamna think tank wa uchumi mle. Wangekua wsnajua Uchumi wasinge mruhusu JPm kufunga maduka ya kubadilishia pesa ambazo zilikua zina chochea flow of foreign exchange......
 
Kuna principle moja ya uchumi ya "the time value of money "
Yaani,Laki moja yako uliyonayo sasa ina nguvu kuliko laki moja utakayokuwa nayo mwakani....

Vitu hupanda bei kila mara,
Heri uweke laki UTT utakauta ongezeko la 10,000 ambayo itafidia upandaji wa bei ,,kuliko ukaificha ndani ya kabati ukaja kuikuta ipo vilevile.
Uko sahihi purchasing power ya pesa inaenda ikipungua kwa sababu ya inflation.

Ila kwa mfano kama mtu anapokea 100k kwa mwaka haina maana yoyote ina maana ni kama analipwa 8k per month

Kwa cost of living za sasa haifidii chochote
 
Kwahiyo tunakubaliana kwamba kwa kijana anayejitafuta Leo "Financial market ya bongo sio sehemu yake sahihi ya kuanzia maisha ya kujitafuta?"

Kumwambia mtu aweke 2mil FAIDA FUND au Anunue hisa za Vodacom basi ni Bora akawe mchuuzi k.koo na hizo mil 2?

#YNWA
Mkuu, kwa kifupi sio bongo tu. Dunia nzima financial market kwa mtu masikini haimfai. Hata Ulaya na Marekani, hakuna faida utakayopata. Lengo la financial markets sio kumtajirisha mtu (hizi UTTs na Faida) lengo lake ni kukutunzia pesa zako. Yaani hata ukizihitaji miaka 30 mbele utazipata kama zilivyo na kafaida kidogo. Mutual funds ni securities tu.

Ukitaka zi grow kafanye biashara mkuu.
Kwa kijana anaye hustle biashara inamlipa haraka, lakini kumbuka ikitokea mfano janga labda kaibiwa duka zima au duka limeungua moto anafilisika on the spot wakati yule wa mil 5 UTT hela yake ipo tu.

Kuwekeza hela UTT ni sehemu za kukuzia mitaji for future use sio kutajirika na huwezi kutajirika.
 
Utaua na kuridhika vyatosha Sana kukupa usingizi !!

Lakini kupata mapesa kibao Ili ule anasa kunachosha sana hasta usingizi hamna!!

Nahisi kati ya watu wanaoishi Kwa shida duniani ni matajiri!! Sidhani kama wanalala hao watu!!
Nahitaji sanaa pesa nyingi, huo usingizi wa shida poa tu acha uje.

#YNWA
 
Yani mimi nakazia kwenye elimu yako mkuu,,,
Diploma, Degree na Masters ya uwekezaji halafu ukaenda nunua hisa za VODACOM ukaacha TBL ,TCC,TWIGA....dah.

Unapewa maswali unashindwa jibu, umebaki maneno...

Mfumo wetu wa elimu unahitaji maboresho makubwa sana.
Thanks.

#YNWA
 
Mleta mada umezungumza mengi hapo kuhusu soko la pesa la Tanzania ukidadavua vyema kuhusu HISA,vipande na bond za serikali.. ..

Nimejaribu kufikiri kitu kimoja kwa sasa umeamuwa kuwekeza kwa kununua vipande vya FAIDA FUND baada ya kutapatapa huku kwingine..Kuna mifuko ya UTT AMIS inatoa gawio sawa au zaidi ya FAIDA FUND sasa nashindwa kukuelewa UTT unawapondea nn akati ndoo vile vile Jielimishe zaidi elimu ni bahari


Jambo la msingi zaidi katika elimu yako nikukumbushe ni kuwa Ili upate pesa zaidi unatakiwa uiwekeze zaidi katika sehemu mbalimbali Ili upate zaidi.Watu wanapowekeza wanakuwa na malengo ya muda mrefu na hata kabla ya kuwekeza katika hizi sehemu wanasisitizaga Sana "ELIMU ELIMU ELIMU" Kwamba kama ni mpambanaji sio kwamba hela yako yoote ndo utaiweka huku lazima uwe na shughuli kadha wa kadha za kukuingizia kipato .Pia ni bora kuweka huku hela usiyoitumia iongezeke thamani kuliko ikae nyumbani au benki tu inapopungua thamani (Makato, inflation)

MWisho unapokua na maono juu ya jambo fulani lenye manufaa kwako usiyumbishwe na mafanikio ya wengine badala yake jifunze na Ishi kulingana na mazingira yako .Kuwafikia kina Warren Buffett n.k Ni ngumu hivyo tufanye kulingana na uwezo, kipato na mazingira yetu hata kama ni kidogo ila chenye manufaa ni kizuri.
Nikushauri "Diversify your portfolio through business"
Hakikisha una biashara ambayo hata kama haupo basi yenyewe inajiendesha.

Kuwa risk lover, hayo ya kukimbia risk achia wastaafu.

Fungua hardware, kuwa na depo, USA vifaa via electronics N.k Ila eti Mambo ya kumpa mtu mil 100 aje akupe mil 10 mwisho wa mwaka ni upuuuzi mtupu.

#YNWA
 
Mleta mada yuko sahihi, huwezi kuona multiplier effect ya bonds kwa uwekezaji wa hela za kuchungulia, bond price variation ina vary kwa less than 20+ or 15+ average kwa mwaka mzima.

The safest inv huwa naona bora ununue viwanja vinavyouzwa na halmashauri, vyenye vimepimwa na unakuwa na hati ya wizara kisha vipe hivo viwanja 5years to 10 yrs.
Ikipita lamitu huko umeula,, mfano kibada year 2007 sq 1300 ilikua worth 3m ila by 2020 you get yourself a clear 55m na simu za mdalali kila siku dc36d1e5-5cc3-4807-9157-326430b6606f.jpeg
 
Government bond ni biashara ya Wahindi, anaweza kuweka B 1 BOT kila mwezi akavuta mshahara wa million kadhaa na pesa inazaa.

Kapuku na biashara ya pesa hakuna kitu kama hicho.

Mambo ya Forex na bit coin sijui ndio cryptocurrency achana nayo kabisa.

Nimemsikia Bongo zozo mara nyingi akidanganya watu kwamba Siri ya yeye kuwa na pesa ya kusafiri duniani ni bit coin, si kweli msiingizwe mkenge huo, wazungu ni fallen Angels huwezi kuujuwa undani wao.

Kwenye ujasiriamali ukiwa na roho ngumu na ukakomaa pesa unaweza kuiona, na kingine Bongo visource vya income unatakiwa uwe navyo vingivingi tu bila kusahau kujenga lodge, hii ndio biashara ya uhakika, starehe ya mafukara NI ngono.
Hapo mwisho umeuaaa…
 
Back
Top Bottom