Tuongee ukweli: Soko la pesa la Tanzania (UTT, Hisa N.k) haliwezi kukufanya ukawa tajiri kwa mtaji wako mdogo

Tuongee ukweli: Soko la pesa la Tanzania (UTT, Hisa N.k) haliwezi kukufanya ukawa tajiri kwa mtaji wako mdogo

Mleta mada yuko sahihi, huwezi kuona multiplier effect ya bonds kwa uwekezaji wa hela za kuchungulia, bond price variation ina vary kwa less than 20+ or 15+ average kwa mwaka mzima.

The safest inv huwa naona bora ununue viwanja vinavyouzwa na halmashauri, vyenye vimepimwa na unakuwa na hati ya wizara kisha vipe hivo viwanja 5years to 10 yrs.
Ikipita lamitu huko umeula,, mfano kibada year 2007 sq 1300 ilikua worth 3m ila by 2020 you get yourself a clear 55m na simu za mdalali kila sikuView attachment 2962859
Mkuu hivo pia impossible sio rahisi kuna watu walinunua viwanja miaka 10 uliopita ila mpaka leo kule bado porini .......pesa zimelala na thamani ya pesa hushuka kila ukicha hiyo biashara sio utauziwa hewa utajokuta muko watu 3 kwenye plot moja wizi wa almashauri ni mwingi.
 
Wewe ndio huna elimu ya uchumi unashindwa kutofautisha biashara na uuwekezaji.

Nani kakwambia Mutual funds ni biashara ? Mutual funds kama UTT Amis ni investment (uuwekezaji)


Sasa Nenda mwenyewe Google kasome uuwekezaji ni nini na business ni nini !
 
Government bond ni biashara ya Wahindi, anaweza kuweka B 1 BOT kila mwezi akavuta mshahara wa million kadhaa na pesa inazaa.

Kapuku na biashara ya pesa hakuna kitu kama hicho.

Mambo ya Forex na bit coin sijui ndio cryptocurrency achana nayo kabisa.

Nimemsikia Bongo zozo mara nyingi akidanganya watu kwamba Siri ya yeye kuwa na pesa ya kusafiri duniani ni bit coin, si kweli msiingizwe mkenge huo, wazungu ni fallen Angels huwezi kuujuwa undani wao.

Kwenye ujasiriamali ukiwa na roho ngumu na ukakomaa pesa unaweza kuiona, na kingine Bongo visource vya income unatakiwa uwe navyo vingivingi tu bila kusahau kujenga lodge, hii ndio biashara ya uhakika, starehe ya mafukara NI ngono.
Kabisa wee uza vifuniko vya asali na lodge basi sie bodaboda utatupata tuu kwenye lodge
 
Government bond ni biashara ya Wahindi, anaweza kuweka B 1 BOT kila mwezi akavuta mshahara wa million kadhaa na pesa inazaa.

Kapuku na biashara ya pesa hakuna kitu kama hicho.

Mambo ya Forex na bit coin sijui ndio cryptocurrency achana nayo kabisa.

Nimemsikia Bongo zozo mara nyingi akidanganya watu kwamba Siri ya yeye kuwa na pesa ya kusafiri duniani ni bit coin, si kweli msiingizwe mkenge huo, wazungu ni fallen Angels huwezi kuujuwa undani wao.

Kwenye ujasiriamali ukiwa na roho ngumu na ukakomaa pesa unaweza kuiona, na kingine Bongo visource vya income unatakiwa uwe navyo vingivingi tu bila kusahau kujenga lodge, hii ndio biashara ya uhakika, starehe ya mafukara NI ngono.
Kabisa wee uza vifuniko vya asali na lodge basi sie bodaboda utatupata tuu kwenye lodge
 
INTRODUCTION.
Mr. Liverpool kwa maisha ni mfanyakazi, mfanyabiashara na mmiliki wa vipande kwenye mutual fund..

Nasoma(ga) sanaa watu humu wanasifia FOREX, Mutual Funds (hasa UTT), Government bonds and bills na fixed deposits.

BODY:-
Soko la pesa Tanzania sio kubwa kiasi kwa maana kuna hisa, vipande vya mutual fund, government bonds and bills, na fixed deposit.

Ila nachojiuliza ""Hivi kuna mtanzania mwenye kipato kidogo anaweza ishi vizuri kwa kumiliki chochote hapo juu?""

Kuna ukweli mwingi sanaa huwa hausemwi na wataalamu wa finance and investment, ""Je soko letu ni sahihi kwa watu masikini na kipato cha kawaida??""

SCENARIO:-
Mimi binafsi ni muwekezaji wa mutual fund inayoitwa FAIDA FUND inayosimamiwa na Watumishi Housing kupitia Wizara OR - Tamisemi.
Nina vipande 25,768.9364 nilivyoanza ununuzi tokea June/2023.

Lakini pia nina biashara kubwa tu mjini yenye mtaji wa Mil 40 na assets za mil 15.

PROBLEM.
Changamoto ya soko letu la pesa ni faida yake ambayo ni ndogo sanaaa...
1. Nilishawahi miliki hisa za Vodacom na CRDB, nilikaa nazo mwaka na nusu, ilinichukua miezi mitatu kuziuza. Hiki ndicho kilichonikera balaa na kuachana na mambo ya hisa.
2. Nikaingia UTT Amis, wale jamaa walikaa na pesa yangu mwaka wakanipa 100k kama Faida..!!
3. Nikaingia kwenye forex nako nikapigwa 200 dollar yoteee (kupitia IQ Option).
4. Nikawaza Crypto currency ila sikushiriki.

Wakati nateseka na money market nilikuwa tayari nina hii biashara iliyoanza kwa mtaji wa mil 10 (bidhaa Mil 5 na Assets 3 na maandalizi mil 2).

Wakati huo wotee biashara ilikuwa inakuwa na wateja wanamiminika Ila money market ilikuwa tu inasumbua na kuiweka hela yangu idle.

Nilivutiwa na money market kwasababu ya
1. Elimu yangu ya chuo, nimesoma Economics, Finance and Investment kwa Diploma, Bachelor na Masters yangu.
2. Ujana, kutaka kuwa tajiri
3. Kuona kazini napoteza muda.

Kwasasa nipo na FAIDA FUND tu japo naona performance yake inazingua tuuuu (slowly growing).

CONCLUSION:-
Kifupi soko la fedha la kibongo bado ni nogo sanaa na si salama kwa kijana mtafutaji.

Yaani, si rafiki kwa kijana ambae anajitafuta akapata mil 2 yake eti akawekeza ili atoke kimaisha, na ni tofauti sanaa na wenzetu.

Wenzetu ukisikia mtu anamiliki 1% ya hisa za facebook huyu ni tajiri balaaa, ila hebu nitafutie mtanzania anayemiliki kampuni 1% ya share akawa tajiri...!!!

ANYWAY:-
Mimi nipo FAIDA FUND kwasababu BONUS Account ya NMB imeshindwa kunipa nachotaka. Bonus Account ili upate interest inatakiwa upambane hasaaaaaa.

Kwasasa nina mpango wa kununua fuso niwe napeleka mizigo kijijini, hivyo nawekeza FAIDA FUND ili ikifika hela ya bei ya fuso basi nitoe ninunue hiyo gari iingie mzigoni...!!!

Hivyo FAIDA FUND naifanya kama bank account ya malengo yangu..!! ila sio NJIA YA KUNITOA KIMAISHA.

Na kiukweli:-
1. Money market ya bongo ni kwa ajili ya watu waoga na wasio na muda wa kufanya biashara Ila nyie wenye mioyo migumu NJOONI KWENYE BIASHARA TUPAMBANE.
Biashara ina hela balaaaaa.

2. Money market ya bongo ni kwaajili ya matajiri tu, yaani jitafutee kwenye biashara halafu "diversify your portifolio" kwa money market, Ila sio eti umepiga deal la mil 5 halafu unaingia money market ili Uwe tajiri, aiseee HAIPO.

Watakaokwambia biashara ni high risk hebu....
1. Waulize kuhusu hisa za NICO, JATU, TOL
2. Waulize kuhusu Vodacom, waliingia DSE kwa 1000/share ghafla wakashuka mpaka 800/share..!!
3. Waambie hivi, watokee watu wawili wasio na ajira wote wapewe mil 5 each, mmoja aende UTT na mwengine aende Kariakoo kuwa winga halafu baada ya mwaka tuje na mrejesho.

Tuendelee kutafuta pesa.

#YNWA
Ukitaka uone faida YA money makert wekeza Kwa muda mrefu Na ACHA pesa ijizalishe usichukue Yani Ni utajiri ambao watarithi vizazi Na vizazi
 
Liverpool VPN huwa ninakufuatilia sana ila kwenye huu mjadala umeniangusha sana. Bahati mbaya sana umetaja kiwango chako chako cha elimu na field yako. Aisee umejidhalilisha sana. Mbaya zaidi unaelekezwa hautaki kutulia na kufuatilia unachokosolewa bali unabisha tu bila hoja.
Kama uko tayari kujifunza badala ya kubishana njoo tuulizane maswali na kuelekezana.
 
Investment sio swala la kuambiwa na mtu au kufuata mkumbo. Unatakiwa uelewe how each investment works (bonds, savings, shares, crowdfunding, trading).

Shabaha yako ni nini kutokana na mtaji wako ndio uchague pa kuwekeza. Mtu mmoja anaweza kwenda sehemu na expectations zake za returns, asipofikia goals zake akaona kule miyeyusho; sasa aina maana ni miyeyusho kwa wote.

Watu wawili wenye millioni kumi wanaweza wasifanane. Mmoja anaweza kuwa hana shida ya kuizungusha haraka kwa ivyo kwake kuiweka kwenye bank savings with compound interest ya 5% mwisho wa mwaka akapata łąki tano. Akaicha hiyo hela bank ipate compound interest kwa miaka kadhaa kwake inafaida.

Mwingine anaona bora afanyie biashara ambayo kwa mwaka inaweza rudisha faida ya million 5 (risk biashara ikienda mrama hela inapotea).

Unachotakiwa ni kujua wewe unataka nini, and whats your risk appetite na kujipeleka unakodhani kuna kufaa.

Sio tu kwenda kununua hisa kwa kuambiwa wakati kampuni yenyewe hujui policy yao ya kugawa gawio ipoje, mfano wanatenga asilimia ngapi ya Net Profit kila mwaka kutoa gawio, wanahisa ngapi na kila hisa Ina thamani gani kwenye vitabu vyao (sio market price), unahitaji hisa ngapi ili upate income unayotaka, unayo iyo hela ya kununua hizo idadi za hisa, historical performance ya shirika ikoje wanapata hiyo faida ya kutoa gawio, comparison na similar businesses sokoni ikoje, vipi wanatoa financial statement zao periodically ili ujiridhishe na ratio muhimu kabla ya kuweka hela yako.

Trading ya forex, shares, cryptocurrencies na yenyewe inataka kujua share price drivers (wholly) na sio sehemu ya amateurs ambao wavivu wa kusoma business news na kujifunza how the market works. Vinginevyo hiyo hiyo hela badała ya kwenda kupoteza huko kama uwezi kujifunza ni bora upeleke sadaka nyumba ya ibada.

Biashara nayo inataka market research kabla ya kuji-commit, kama lengo ni kukua basi na basic management knowledge.

Crowdfunding na yenyewe lazima uelewe hiyo biashara sio kusikiliza hadithi za Mr Kuku bila ya kuona vitabu vyake; utatapeliwa.

Mutual funds kama (UTT Amis) ni taasisi ya wataalamu ambao wanawekeza kwa niaba yako katika maeneo hayo ya juu mainly kwenye bonds (both corporate and government), bank savings, buying shares on plc, investing on startup business, buying preference shares, redeemable bonds, irredeemable bonds.

Mutual funds mara nyingi wanawekeza hela yako kwenye safe investment but it’s not unheard of na wao kupoteza hela, faida yao inatokana na fees ndogo wanayokuchaji kwenye investment return ya hela uliyowapa. Walau ni wataalamu wanaotumia mud ku-asses hizo investment kwa niaba yako kabla ya kuwekeza.

Sasa badala ya kuambiwa wapi kizuri au wapi kubaya elewa kwanza malengo yako, uwezo wako wa kifedha na kuamua; we are not the same. Ukiwa na billion mbili kuweka billion 1 kwenye Savings account au popote unaweza kushinda Bahamas mwaka mzima una habari unakula interest, lakini huna luxury hiyo kwa savings ya 10 milllion.

Haya mambo yanataka ujielewe wewe sio uambiwe wapi kuzuri au wapi kubaya na mwingine wakati motive zenu sio sawa, risk appetite sio sawa, mitaji sio sawa na uelewa wa kina sio sawa; ukishajijua then commit.
 
Liverpool VPN Hizi mutual fund ni za watu wote kuanzia matajiri mpaka masikini mf Bodaboda kama ulivyowatolea mfano mara kadhaa

Twende taratibu
Unategemea dereva bodaboda anapaswa kuendesha bodaboda kwa miaka mangapi ili awe tajiri?
Tobo sahihi la watu wa mpunga mchache ni biashara.
Mil 5 kwa asilimia 10 kama Rate of Return ni ndogo.
Acheni kukimbia risk, fanyeni biashara.

#YNWA
 
Wewe ndio huna elimu ya uchumi unashindwa kutofautisha biashara na uuwekezaji.

Nani kakwambia Mutual funds ni biashara ? Mutual funds kama UTT Amis ni investment (uuwekezaji)


Sasa Nenda mwenyewe Google kasome uuwekezaji ni nini na business ni nini !
Hebu njoo hapa wewe unayejua,
Nani kasema investment ni biashara?
Wapi, nimesema lini, na nani?

Kwamba miaka 12 kwenye investment, economics na finance mpaka Leo bado google ndio anisaidie??

Umemaliza kupuyanga tu.
Nijibie hoja yangu ""Je money market ya bongo inamfaa mtu anayejitafuta?""

Uongee kwa mfano:- unipe financial plan na schedule ya mtu anayeweka buku 5 kila siku, uniambia huyu bila kuinvest kwenye biashara atatoboa lini??

#YNWA
 
Kuna mabadiliko ya tabia nchi, baada ya miaka hiyo hilo shamba laweza kuwa sio kama sasa.

Alafu hiyo mifano yako unayopiga siyo sawa kabisa

Usipoteze muda kuelimisha hao watu mkuu.
Ngoja nikupe mfano:-

Kama unavyosema watu wasome documents za hizo bonds, kampuni na chochote wanachotaka kuwekeza kwenye money market ndio wawekeze wakiwa full informed basi hata kwenye biashara nako wafanye hivyohivyo.

Ila NGOJA nikupe mfano;

1. 2012 ndio niliajiriwa, nilivyoajiriwa nilikua bahili balaa na nilikuwa natunza sanaa pesa zako.

Kufika 2013 June nilienda mkoa Fulani nikanunua beach plot mil 3 (Eka 1)

Mwaka juzi (2022) nilipata simu kutoka kwa dalali ya kwamba kuna mzungu anaitaka anataka kunipa mil 40 ili nimuachie (anajenga hotel ya kitalii).
Jirani yangu (eka 5) aliuza Ila Mimi nimegoma, Ila nimegoma kwasababu ya bei.
Nilichofanya nimetafutia hati kuongeza thamani halafu nimevunga.

Kuna hela naitaka Ila mzungu bado kawa mbishi.

Hivyo namsubiri tu mzungu, najua hotel yake inazidi kuwa kubwa na eneo lake lina kuwa dogo hivyo ATAINGIA KINGI TUUUU....

NAOMBA NIAMBIE FINANCIAL MARKET GANI INGENIPA HIZI HELA KWA MIAKA HII 9?

2. Mshikaji wangu bwana 2015 alipiga mshindo akapata mil 15, fasta akaenda kununua nyumba Mwananyamala Dar.

Sasa bwana sasa hivi Mwananyamala ipo kwenye ule mradi wa CBD (Kama sijakosea jina) hivyo nyumba yake imezungukwa na rami pande mbili (lami za mtaani) na ipo kwenye kona.

Kuna mwarabu alimtafuta mwaka huu anataka kumpa mil 45 mwamba kakaza kasema ataiuza mwaka 2030 akiwa anastaafu (lengo lake ni kuacha kazi akiwa na miaka 40 (2030)) ili akaanze Mambo yake mapema. Malengo yake ni kufanya uwekezaji mkubwa kwenye biashara.

Sasa unadhani mwaka 2030 hii nyumba itakuwa na thamani gani ikiwa Leo watu wanaitaka kwa mil 45?

Mutual fund, share, and so forth WANAWEZA KUTOA KIASI KAMA HICHI kwa kipindi hicho?

Ushauri:-
Vijana wakiume wenye nguvu na akili, karibuni kwenye biashara acheni mambo ya kukimbia risk.

Njoo mjitose muone utamu wa biashara.

Hapa nilipo nataka kuuza hicho kuwanja/beach plot ili nifanye biashara ya kuwa wakala mkubwa sanaa wa gas za kupikia huu mkoa.

Let's think about risk vijana, mbona tuna wazee wetu waswahili wametufungulia njia, wakina R.I.P Mengi, Ruge, na Vunja Bei wangekuwa na akili hizi za kukimbia risk LEO WANGEKUWA WAPI, UNGEWAJUA WEWE KWA HAYA MAFANIKIO WALIYOYAPATA?

HEBU KIMBIENI NJOO KWENYE BIASHARA tukusanye pesa.

Akili hiyohiyo ya kusoma soma kwenye mabond huko na mashare ili upate high RR basi hiyohiyo akili na mbinu njoo uiapply kwenye biashara vijana.

#YNWA
 
Ngoja nikupe mfano:-

Kama unavyosema watu wasome documents za hizo bonds, kampuni na chochote wanachotaka kuwekeza kwenye money market ndio wawekeze wakiwa full informed basi hata kwenye biashara nako wafanye hivyohivyo.

Ila NGOJA nikupe mfano;

1. 2012 ndio niliajiriwa, nilivyoajiriwa nilikua bahili balaa na nilikuwa natunza sanaa pesa zako.

Kufika 2013 June nilienda mkoa Fulani nikanunua beach plot mil 3 (Eka 1)

Mwaka juzi (2022) nilipata simu kutoka kwa dalali ya kwamba kuna mzungu anaitaka anataka kunipa mil 40 ili nimuachie (anajenga hotel ya kitalii).
Jirani yangu (eka 5) aliuza Ila Mimi nimegoma, Ila nimegoma kwasababu ya bei.
Nilichofanya nimetafutia hati kuongeza thamani halafu nimevunga.

Kuna hela naitaka Ila mzungu bado kawa mbishi.

Hivyo namsubiri tu mzungu, najua hotel yake inazidi kuwa kubwa na eneo lake lina kuwa dogo hivyo ATAINGIA KINGI TUUUU....

NAOMBA NIAMBIE FINANCIAL MARKET GANI INGENIPA HIZI HELA KWA MIAKA HII 9?

2. Mshikaji wangu bwana 2015 alipiga mshindo akapata mil 15, fasta akaenda kununua nyumba Mwananyamala Dar.

Sasa bwana sasa hivi Mwananyamala ipo kwenye ule mradi wa CBD (Kama sijakosea jina) hivyo nyumba yake imezungukwa na rami pande mbili (lami za mtaani) na ipo kwenye kona.

Kuna mwarabu alimtafuta mwaka huu anataka kumpa mil 45 mwamba kakaza kasema ataiuza mwaka 2030 akiwa anastaafu (lengo lake ni kuacha kazi akiwa na miaka 40 (2030)) ili akaanze Mambo yake mapema. Malengo yake ni kufanya uwekezaji mkubwa kwenye biashara.

Sasa unadhani mwaka 2030 hii nyumba itakuwa na thamani gani ikiwa Leo watu wanaitaka kwa mil 45?

Mutual fund, share, and so forth WANAWEZA KUTOA KIASI KAMA HICHI kwa kipindi hicho?

Ushauri:-
Vijana wakiume wenye nguvu na akili, karibuni kwenye biashara acheni mambo ya kukimbia risk.

Njoo mjitose muone utamu wa biashara.

Hapa nilipo nataka kuuza hicho kuwanja/beach plot ili nifanye biashara ya kuwa wakala mkubwa sanaa wa gas za kupikia huu mkoa.

Let's think about risk vijana, mbona tuna wazee wetu waswahili wametufungulia njia, wakina R.I.P Mengi, Ruge, na Vunja Bei wangekuwa na akili hizi za kukimbia risk LEO WANGEKUWA WAPI, UNGEWAJUA WEWE KWA HAYA MAFANIKIO WALIYOYAPATA?

HEBU KIMBIENI NJOO KWENYE BIASHARA tukusanye pesa.

Akili hiyohiyo ya kusoma soma kwenye mabond huko na mashare ili upate high RR basi hiyohiyo akili na mbinu njoo uiapply kwenye biashara vijana.

#YNWA
Una ujinga wa kiwango cha juu sana.
Wewe unafanya nini Faida Fund?
 
Back
Top Bottom