Tupate uthibitisho wa tuhuma zinazomkabili ASP Jumanne shahidi Na. 8 wa Jamhuri kesi ya Mbowe

Tupate uthibitisho wa tuhuma zinazomkabili ASP Jumanne shahidi Na. 8 wa Jamhuri kesi ya Mbowe

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2019
Posts
762
Reaction score
6,984
Naomba kwa mwenye usahihi wa tuhuma zinazoelekezwa kwa shahidi Na. 8 atusaidie kuziweka hapa for future reference lakini pia kusaidia familia yake kujua kijana wao huko kazina anatumikia umma au anajitumikia. Hadi Sasa zipo tuhuma tatu nzito dhidi yake ambazo Ni:

1. Anatuhumiwa kumwekea mtuhumiwa wa Kwanza kwenye kesi ya Mbowe Bastola katika lengo lakufanikisha kubambikiwa kesi. Taarifa hizi Ni kwa mujibu wa mtuhumiwa wakati anajieleza wakati wa pingamizi

2. Akiwa OC CID Arusha anatuhumiwa kupokea mgao wa fedha za unyang'anyi zilizoporwa na Sabaya. Taarifa hizi ni kwa mujibu wa shahidi kwenye kesi iliyopelekea sabaya Kufungwa

3. Anatuhumiwa kushirikiana na aaskari wenzake kumwekea Prof mmoja pembe za ndovu kwenye mzinga na Kisha kumkamata profesa huyo na kumweka ndani akidai atamfungulia mashtaka ya uhujumu uchumi jambo lililopelekea Profesa kuwapa yeye na Askari wenzie milioni Mia Moja kufukia kesi hiyo. Baadaye taarifa zilivuja na profesa kuhojiwa na vyombo vya habari na kukiri kukamatwa na Askari wa upelelezi USA RIver ambapo Bw. Jumanne ndiye alikuwa mkuu wa upelelezi. Ni vigumu kumtenganisha OC CID na upelelezi ofisoni kwake na kumbuka yeye ndiye aliyelekeza mzee huyo kuwekwa mahabusu na kuruhusu vijana wake kwenda na mtuhumiwa Hadi benki kuchukua fedha.

Wakati tunajadili tuhuma hizo, taarifa zinadai alisimamishwa kazi kwa tuhuma zilizokuwa zinamkabili japo Hadi Sasa TAKUKURU awajachukua hatua yoyote dhidi yao. Aidha hakuna uchunguzi wowote uliofanywa kuhusu uhusika wake kwenye uhalifu wa Sabaya.

Hawa tuseme ndio wakubwa wa nchi hii, wanakupa kipigo wanapigiwa makofi kwa kazi nzuri.

Mwenye kupingana na taarifa hizi au Mwenye ilufafanuzi zaidi karibuni, Mimi haya Ni kwa mujibu wa yaliyopo mitandaoni na hapa ni mtandaoni twende kazi
 
Shida kubwa iliyotokea ni kwa Mamlaka za Tanzania kuamini kwamba Ole Sabaya anaweza kuratibu kesi ya Ugaidi dhidi ya Mbowe , Hiki ni kiwango cha chini sana cha akili.

Huyu Jumanne ni miongoni mwa Askari wenye kashfa za kibwege sana ! lakini eti kaaminiwa .

Naona aibu sana kuwa Raia wa Tanzania
 
Very low IQ. Yaani kama Ole Sabaya ndio alikuwa Think Tank wa CCM unaweza kuona hao wengine wana viwango gani.
Ole Sabaya ndio alitegemewa na ccm kumuua Mbowe kimwili au kisiasa , ndio maana alikuwa haogopi hata kurekodiwa kwa CCTV Camera , nina zaidi ya video 25 za Sabaya akifanya Uhalifu waziwazi huku akilindwa na Polisi wa Sirro .

Iko siku isiyo na jina hata huyo Sirro atafungwa kifungo cha aibu sana
 
Yaani aibu ya serikali naiona Mimi. Mtu kama Profesa Maeda kuwekewa pembe za ndovu kwenye mzinga na Jumanne, ili mradi tu atoe hela zake za kiinua mgongo.
Kasimamishwa kazi, lakin leo mtu huyohuyo ndo Shahid wa Jamhuri.. naona aibu mimi
CCM haina uwezo tena , imekwisha kabisa , imekongoroka
 
Ole Sabaya ndio alitegemewa na ccm kumuua Mbowe kimwili au kisiasa , ndio maana alikuwa haogopi hata kurekodiwa kwa CCTV Camera , nina zaidi ya video 25 za Sabaya akifanya Uhalifu waziwazi huku akilindwa na Polisi wa Sirro .

Iko siku isiyo na jina hata huyo Sirro atafungwa kifungo cha aibu sana
Duuh He was a GodFather among Hooligans
 
Back
Top Bottom