Tupe Experience yako siku ya kwanza kuendesha gari HighWay safari ilikuwaje

Tupe Experience yako siku ya kwanza kuendesha gari HighWay safari ilikuwaje

Me Dar to Mwanza, sikuka cheti ata kimoja.

Ninavotoka Dar nikasema max speed itakua 80kph. Aisee usijidanganye.

Uko njiani kuna barabara zimenyooka ova rula, nikawa nagusa 160kph kwenye Runx.

Ninavorudi nilikua 120 nikala basti. Mingu huyu, acheni tu.
 
Mimi toka Dar hadi musoma aisee nilikuwa mwoga hatari spidi niliyokuwa naenda nayo ni 40/50 yaani nikifika 60 naona kama naenda mtaroni,break zilikuwa kila wakati halafu nikajichanganya kupita barabara yaarusha nilitumia siku 3.

Utakua ulipigiwa horn za kutosha na kupigwa mataa mengi sana, kwa mwendo huo highway!!!
 
Mimi toka Dar hadi musoma aisee nilikuwa mwoga hatari spidi niliyokuwa naenda nayo ni 40/50 yaani nikifika 60 naona kama naenda mtaroni,break zilikuwa kila wakati halafu nikajichanganya kupita barabara yaarusha nilitumia siku 3.
Wewe hutufai asee yan speed 60 kwenye highway ndio maximum? 😂😂 hiyo ni speed ya kuendeshea katikati ya mji mkuu.
 
Sana tulipofika geti la ngorongo kuna dereva wa basi akanifuata kuniuliza mbona break nyingi sikumjibu kwasababu ukweli nilikuwa naujua mwenyewe maana nilikuwa leaner.
Utakuwa umetumia petroli lita mia kwenda tu
 
Dar Masasi nilidamka saa kumi na moja nilitumia siku nzima mpaka mishale ya saa kumi jioni. Nilifika miguu imevimba na mabega yanauma utadhani nililibeba mgongoni. Gari ni gx 100.
Daaaah,umefika nyumbani kwetu mkuu,Masasi moja hiyooooo,big up sana,na wewe ni wa huko huko nn au mishe tu za nchini?
 
Aisee ni story ndefu,nilikuwa nimeagiza gari nje ya nchi,nikawa katika kujipanga kwenda kuifuata jamaa yangu ambae kwao wana gari akaniambia anauwezo wa kuendesha,kwa hiyo tukapanga safari usiku wa safari jamaa ananiambia haioni leseni(alikuwa hana kumbe)na mimi nimeshakata tiketi ikabidi tuondoke,nikajakugundua kumbe pia sio mzoefu wa kuendesha kwa hiyo mimi nilikuwa na leseni ikabidi ndio niwe dereva tegemeo ingawa sina uzoefu na highway,kwa hiyo unaweza kuelewa kwanini nilitembea speed hiyo.

[emoji23]so kilichotokea ni bora hata angebaki maana kazi uliifanya yote wewe? Ila speed 60 mwendo wa kinyonga sana
 
Me kwa mara ya kwanza nilitoka Arusha to Dar nikiwa na familia, natumia Runx speed ya 80 -120. Sijui ujasiri ulitoka wapi aisee na road kulikuwa na mvua, nakumbuka nilitoka sa12 nikafika Dar sa9 mchana. Ninampango wa kwenda tena December hii pamoja na familia tena.
Kuna mdau hapo juu kasema yeye alitumia Runx speed kali hadi ikabast. Kwa anayejua recomended speed kwa gari kama hii ukiwa highway ni kiasi gani maana wengine ufundi wa magari hatuujui sana kama nikipata shida huko road.
 
Me kwa mara ya kwanza nilitoka Arusha to Dar nikiwa na familia, natumia Runx speed ya 80 -120. Sijui ujasiri ulitoka wapi aisee na road kulikuwa na mvua, nakumbuka nilitoka sa12 nikafika Dar sa9 mchana. Ninampango wa kwenda tena December hii pamoja na familia tena.
Kuna mdau hapo juu kasema yeye alitumia Runx speed kali hadi ikabast. Kwa anayejua recomended speed kwa gari kama hii ukiwa highway ni kiasi gani maana wengine ufundi wa magari hatuujui sana kama nikipata shida huko road.
Angalia kwenye matairi ya gari yako yanakuaga na recommendations za maximum speed.
 
[emoji23]so kilichotokea ni bora hata angebaki maana kazi uliifanya yote wewe? Ila speed 60 mwendo wa kinyonga sana
Ndio kila jambo lina faida na hasara zake,faida ni kwamba baada ya pale nilipata ujasiri wa kuendesha highway nikawa sihitaji dereva ninapokwenda safari ndefu.
 
Dar Masasi nilidamka saa kumi na moja nilitumia siku nzima mpaka mishale ya saa kumi jioni. Nilifika miguu imevimba na mabega yanauma utadhani nililibeba mgongoni. Gari ni gx 100.
Utadhani umetembea kutoka Mwanza hadi DSM kumbe hapo Masasi tu
 
Mimi safari yangu ya kwanza ilikuwa ni kutoka Kigoma-Morogoro.Hapo ni baada ya kupata uzoefu wa Mwezi mmoja wa kuendesha gari baada ya kujifunza kupitia tutorials za youtube.Nilitoka Kigoma saa 12 asubuhi.Kutokana na uoga niliokuwa nao,nilipanga kwamba nitatembea maximum mwendo wa 70km/hr.
Nilikuwa na kigari changu,Carina Si nikiwa nimepakia abiria wanne,mkononi nina leseni yenye umri wa wiki 1 tu.Aisee,asikwambie mtu,nilijikuta huko njiani nime-gain confidence ya ajabu,mwendo ulikuwa ni 150,160....nikipunguza sana ni 100/120.Nilikuwa sitaki kuona basi au lorry mbele yangu,ni mwendo wa kuzikata tu.Nilijikuta saa 10 jioni niko dodoma city,nikapumzika kama nusu saa.Saa mbili usiku nikapaki chuma Moro.
 
Mimi safari yangu ya kwanza ilikuwa ni kutoka Kigoma-Morogoro.Hapo ni baada ya kupata uzoefu wa Mwezi mmoja wa kuendesha gari baada ya kujifunza kupitia tutorials za youtube.Nilitoka Kigoma saa 12 asubuhi.Kutokana na uoga niliokuwa nao,nilipanga kwamba nitatembea maximum mwendo wa 70km/hr.
Nilikuwa na kigari changu,Carina Si nikiwa nimepakia abiria wanne,mkononi nina leseni yenye umri wa wiki 1 tu.Aisee,asikwambie mtu,nilijikuta huko njiani nime-gain confidence ya ajabu,mwendo ulikuwa ni 150,160....nikipunguza sana ni 100/120.Nilikuwa sitaki kuona basi au lorry mbele yangu,ni mwendo wa kuzikata tu.Nilijikuta saa 10 jioni niko dodoma city,nikapumzika kama nusu saa.Saa mbili usiku nikapaki chuma Moro.

hapa ni Mungu tu alikufikisha salama yani uzoefu wa kuendesha wiki moja na njiani ulikuwa unatembea 150km/h na unashindana hadi na mabasi [emoji23]! Vipi abiria hawakugundua wewe Learner?
 
Back
Top Bottom