Tupeane mawazo wapendwa

Maty mpendwa kuna mambo hayavumiliki , me wifi yangu hadi alitaka kufa na ujauzito kwa pressure mume ana nyumba ndogo 3 na zote ni wadada wa mujini na familia ya kiume inajua, mume anarudi manane ya usiku hadi apige round nyumba ndogo zote. Wazaz wanamwambia avumilie. Hamjali kamtelekeza na mtoto wa miaka 4. Hapo kuna uvumilivu tena???
 




Sasa hivi kushindana kumekua kwingi, kila mmoja kwenye ndoa anataka kua mbabe. Longi ilikua binti anafundishwa uvumilivu wa kila kitu katika ndoa, sasa hivi mkaka atapata wapi mtu wa kumbabaisha na akababaishika? Kitu kingine ni ile ya wote wawili au mmoja wapo kukosa busara ya kumappreciate mwenzio kwamba hata kama humpendi ana nafasi muhimu ya mme/mke. Guys kwa upande wangu nimepata mume ambae ndio ana kasoro lakini ananiheshim, anajali ndoa yetu na mahitaji ya ndani na nje (hata kama tunasaidiana), anajali na kupenda maendeleo ya watoto wetu - kunapotokea tatizo lazima ni fight mana c kazi ndogo kuanza tena kua katika market ya dating. Na hasa hapa Bongo IT IS HARD FOR MEN TO BE MEN na IT IS HARD FOR A WOMAN TO BE A WIFE.
 
ndoa za Dot.Com ni ngumu kuzihandle, tuvumilie tu!
 
Huyo mwanaume alibadilika ghafla au ndo aliolewa na player akitumaini kumbadilisha?
Na kama alibadilika baada ya kuoa ameshajiuliza ni kwa nini?

 


ha ha ahaha nimecheka mpaka machozi ya furaha yamenitoka, ASANTE KWA KUNIONGEZEA UHAI NA AFYA YANGU,,,kumbe sikukosea kukumiss kwenye hii thread nzuri ya MATY....yaani napiga picha kama nakuona unavyojifanya umekasirika sana,kumbe nia yako mume aendelee kukubembeleza zaidi....kubebembelezwa kuna raha bwana asikwambie mtu....na hasa ukibembelezwa na kiumbe kinaitwa mwanaume, raha yake haisimuliki ilivyo nzuri....safi sana nyumba kubwa umeonesha ni jinsi gani unaujua utamu wa kubembelezwa na mume.....lol
 
Mi mwenzangu najivumilia tu milima mabonde mafuriko elninyo nimo tu, mbele kwa mbele huko tutajua


SAFI SANA GAGA, MUNGU AZIDI KUKUZIDISHIA MOYO WA UVUMILIVU.
MANAKE IMEANDIKWA,
TUNAYAWEZA YOTE KATIKA YEYE ATUTIAYE NGUVU.

Ila pia mwambie MUNGU asante kwasababu unakutana na magumu na yanayovumilika...lol
 
ULICHOANDIKA NI KWELI KABISA MATY....siku hizi ndoa ikidumu zaidi ya mwaka bila kuvunjika...ni jambo la kwenda kwenye nyumba ya ibada kutoa sadaka ya shukrani,elimu na pesa walizonazo wanandoa ndo zinazowapa mabichwa na confidence ya kitoto ya kuvunja ndoa zao..bila kukumbuka kuwa walishaweka ahadi ya kuvumiliana kwenye shida na raha hadi kifo kitakapowatenganisha...:angry:
 
Mie kwa kweli uvumilivu siwezi nikishindwa nasepa zangu isiwe tabu ung'ang'anie ya nini ilhali mtu ameshakuchoka?
 


Hakika sweetdada umelonga mwanakwetu, hata mimi nilizoea kusikia wanasema Nyumba ni mwanamke.
Na je mwajua kuwa ndoa kwa wingi zimeanza kuvunjika kuanzia miaka ya 80 na kuendelea?! kabla ya hapo mama zetu walikuwa wavumilivu na wanyenyekevu kwa kiwango cha juu sana. Hapa swali ni je akina mama wa sasa waweza kurejea hali hiyo ya zamani?
 
mimi yalinikuta na naapa sitakaa nioe tena hapa duniani,nina 40years old,wanawake wakiwa na kazi na pesa wanakuwa na kiburi ambacho hakuna mwanaume wa kuzuia,na kama unaona mwanamke mwenye pesa anaishi kwenye lindoa la matatizo ujue hapo kuna kitu,labda huyo mwanamama ana kahuruma na watoto,thats all,dunia inabadilika na hii ndio hali halisi:frusty::frusty::frusty::frusty::frusty::frusty:
 
usichoke hiyo ndio reality watu wanavamia ndoa kwa kuangalia vitu vya ajabu ambavyo sio endelevu kama vile pesa, umaarufu, nk so mambo yakiharibika na mapenzi yameisha. kingine hakuna mafunzo ya namna ya kuishi ndani ya familia. wadada wengi wa sasa wanajilemba lakini hawana elimu ya kuishi na familia wanajua ndoa ni ...............tu kumbe kuna mambo mengi ya ziada. Mi naona wazazi inabidi wawaelimishe watoto wao namna ya kuishi na mume/mke.
 


suzy habari yako imenishangaza ,,
mungu atusaidie kuzijenga ndoa zetu katika misingi imara ,pasipo kila mmoja kujiona yeye ndio yeye
 

pole topthinker naamini umeumbwa uishi kwa amani na furaha ,samaki mmoja kioza sio wote ndugu:amen:
 
The topic is hot...Ndoa yangu bado changa so naobserve na kulearn... Thanx Maty kwa kuanzisha hii thread... Okey, 2endelee...
Usiogope mwali doa zote sio lazima ziwe na matatizo, ila ujue pia kila siku sio jumapili. jiweke imara ili hata kama yakikupata matatizo ujue unakabiliana nayo vipi. Meanwhile enjoy you marriage
 

mnaona ni sawa kwasasa may b coz hayajawafika, kupigania ndoa ya mwanaume mwenye kimada sio shughuli ndogo, ombeni yacwafike, coz kuna mawili, mume kashalowea huko au atarudisha fikira nyuma na kujirudi....ni kheri mkiweza kuhimili hiyo mikiki mikiki, kwa wengine tulikaribia kukata tamaa, unamuonea mwanaume kinyaa haswa kila dk unahic limetokea huko, bac hamu nalo huna hata chembe, kuirudisha hali ya kumtamani tena nayo ni shughuli pevu...pweehhh ningekuwa mtawa mie japo ningemic hii mitikicko ya lyfe....lol
 
Dah! mawazo yenu niliyoyapata hapa inaonyesha ndoa ni ngumu sana asee

Maty,hivi kuna mtu alikuchapia eti ndoa
rahisi? lol huyo mkimbie kwa spidi ya tsunami! ndoa shughuli,ndoa inataka moyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…