Tupeane mawazo wapendwa

Tupeane mawazo wapendwa

Nani kichwa cha familia?

Mme anasugua kichwa mwanamke na watoto watapishana vp chooni?

Bila yeye watoto trip za chooni zinapungua kwa siku mara moja.

NIKWELI MUME NI KICHWA CHA NYUMBA,

ILA hilo la mume anasugua kichwa mwanamke na watoto watapishana vp chooni SIYO KWELI KUWA KARNE HII ETI NI MWANAUME TU ANAEWAJIBIKA KUIHUDUMIA FAMILIA YAKE, BALI NI MUME NA MKE WOTE KWA PAMOJA WANAWAJIBIKA KUIHUDUMIA FAMILIA.
TRIP ZA WATOTO KUPISHANA CHOONI ZINACHANGIWA NA PANDE ZOTE MBILI SIYO BABA TU, LABDA KAMA NI SINGLE FATHER.....

FIDEL PUNGUZA MFUMO DUME, MKE NA MUME WOTE WANATAKIWA KUPENDANA,KUSIKILIZANA,KUTHAMINIANA,KUJALIANA,KUDEKEZANA,
KUVUMILIANA,KUBEMBELEZANA,KUSHAURIANA,KUKUBALIANA,KUKOSOANA,KUSIFIANA,
NA MENGINE MENGI.
LAKIN SIYO WEWE MWANAUME UMEKAA TU ETI UNASUBIRI MKE AWAJIBIKE KWAKO WAKATI WEWE HAUWAJIBIKI KWAKE....aaah FIDEL vibaya hivyo hata MUNGU HAPENDI.....

Bye.
 
hili post ukichanganya na hayo ma lips mie kwisha habari yangu. naomba nikuwe msomaji tu kwenye hii sred

Kloro inabidi ubandike hizi lips kwa wall yako..ha ha Eniwe, haya maisha inabidi mtu utafakari mara mbili mbili maamuzi unayochukua kuambatana na jinsi maisha yanavyokuendea. Hakika nitavumilia kinachovumilika laa sitowezi kuishi na mume kwa roho ya chuki, hasira na uadui sababu ya watoto. Ndio mana nikisikia watu wameachana najua si jambo rahisi!!

Unaweza ukawajali watoto wakawa na msingi imara kimaisha kwa kulelewa na mzazi mmoja au walioachana..kila mtu na package yake katika maisha haya!!..mwingine unaweza kuwa kwenye ndoa hajali hao watoto kabisaa mpaka watoto wanaelewa hali ya nyumbani na kuathirika kimalezi!!

Siyo kwa vile kuna kitu uvumilivu basi mtu uvumilie mpaka uvumilivu wenyewe unakwambia enaf! Life hii imejaa scenario nyingi..

Upande mwingine
Maisha ya ndoa na changamoto zake ukipata mtu ambaye mnaelewana vizuri, kuwasiliana hata mkikwaruzana, kusikilizana, kujali familia, na mambo yote mazuri hapo safi kabisa..tena kama mwanandoa mwenzio ni kama besti frendi wako inapendeza siyo cheo cha mke na mume hamtaniani wala kuwa huru kila mmoja wenu..Tatizo ni kukutana na mtu wa aina hiyo, naona mara nyingi hasi zinakutanaga na chanya!!
 
Yeah..ni kweli..
DEFINITION ya upendo ni nini??
Kama kweli anakupenda, maana yake atakulinda, atakuwa tayari kufanya chochote kwa ajili yako..UPENDO is a two way traffic (lakini ni jukumu la mwanaume zaidi).. (wanaume wanaambia na vitabu vya dini, PENDENI wake zenu, na wanawake wanaambiwa, MUWATII waume zenu)

mwanaume kama hawezi KUPENDA, ndoa itakuwa matatani,
na mwanamke kama hawezi KUTII ndoa itakufa tu..(tunaweza kutumia busara zetu, akili zetu, na mambo mengine, lakini kama hayo mambo hayatelekwezi, usitegemee ndoa itakuwa nzuri)
unatakiwa utafute mwanaume atakaye-KUPENDA na utakaye-MTII.
Mpendwa hapo umenena sawa,na ndivyo hata biblia inasema mwanaume anapaswa kumpenda mkewe na vilevile wanawake wawatii waume zao
 
kuachana sio dili but sometime inabidi, kupata muda wa kufikiri na kuheshimu maamuzi....... D knob
 
True that!Mmoja anaweza kuweka juhudi kwenye kujenga mwingine kubomoa!Hapo hamtafika popote zaidi ya kuishia kuishi maisha ya kukomoana!

Kloro inabidi ubandike hizi lips kwa wall yako..ha ha Eniwe, haya maisha inabidi mtu utafakari mara mbili mbili maamuzi unayochukua kuambatana na jinsi maisha yanavyokuendea. Hakika nitavumilia kinachovumilika laa sitowezi kuishi na mume kwa roho ya chuki, hasira na uadui sababu ya watoto. Ndio mana nikisikia watu wameachana najua si jambo rahisi!!

Unaweza ukawajali watoto wakawa na msingi imara kimaisha kwa kulelewa na mzazi mmoja au walioachana..kila mtu na package yake katika maisha haya!!..mwingine unaweza kuwa kwenye ndoa hajali hao watoto kabisaa mpaka watoto wanaelewa hali ya nyumbani na kuathirika kimalezi!!

Siyo kwa vile kuna kitu uvumilivu basi mtu uvumilie mpaka uvumilivu wenyewe unakwambia enaf! Life hii imejaa scenario nyingi..

Upande mwingine
Maisha ya ndoa na changamoto zake ukipata mtu ambaye mnaelewana vizuri, kuwasiliana hata mkikwaruzana, kusikilizana, kujali familia, na mambo yote mazuri hapo safi kabisa..tena kama mwanandoa mwenzio ni kama besti frendi wako inapendeza siyo cheo cha mke na mume hamtaniani wala kuwa huru kila mmoja wenu..Tatizo ni kukutana na mtu wa aina hiyo, naona mara nyingi hasi zinakutanaga na chanya!!
sred klosed
 
Dear maty yaani leo umegusa mtima muhimu sana katika maisha yetu ya sasa. Kusema ukweli hal hii inatisha na kwa bahati mbaya sana ndio kwaaanza inakamata chati kwa kasi. Sometimes nasema bila kumtanguliza MUNGU katika ndoa na maisha yetu, mambo kama haya ni inevitable kabisa. Na kama ulivyosema ndoa za wenye viwango flani vya elimu mamb ndo huwa magumu zaidi kuliko ndoa ambazo wanaume ndo wenye elimu au mali kuliko wanawake. Kwenye ndoa ambayo wenzi wote wana viwango sawa vya elimu au kipato mara nyingi kuna mambo ambayo katu hayatavumilika na pande yoyote kati yao. Mf. Katika ndoa kama hii kwa wale wanaume wenye tabia ya kunyanyasa wanawake kwa kisingizio kuwa ni mkewe na hapaswi kuuliza, hoji au kufuatilia mambo anayoyafanya yeye kama mume ni wazi akileta ubabe kwa vitu ambavyo ni obvious mke atapata kichwa kuwa asimbabaishe.
hali kadhalika mke anawezakuwa ndo chanzo cha matatizo especially kama naye akikinga mkono kiganja kinajaa....... anawezajikuta analeta hadithi za usawa mpaka kwenye kugawa dozi............jana nilikupa leo nami napumzika (utadhani akitoa anayefurahia ni mpewaji tu). Sasa kwa mwanaume mwenye mke wa hivi ni lazima hatakubali na ataona ni bora atafute amani huko inakopatikana.

Ni tofauti na nyumba ambayo mke ni msomi, mume msomi but kila mtu anajua na kutimiza wajibu wake kama mume/mke na kama Baba/mama. Hawa wataishi kwa amani pamoja na kuwepo kwa migongano ya kawaida, heshima inatawala zaidi na kila mtu anatambua thamani ya mwenzie. Kinyume cha hapo ni kutengana.
wa maisha halisi ya w

Darling maty...........when worse comes to worse sometimes ni bora mkatengana kuliko kuwakuza watoto katikati ya uwanja wa vita. Madhara yake ni makubwa kuliko yale wanayoyapata kwenye utengano kwani huko unawezakupanga mpangilio maalumu. Kulea watoto ndani ya ndoa yenye migongano kila kukisha (sisemi ile ya kawaida) but sometimes watu wanakuwa na irreconciliable issues ambazo nyingine wanashindwa kabisa kuzicontant na kutozionyesha kwa watoto. Mfano kupigana, kutukanana, kunyanyasana n.k. madhara ni makubwa sana kisaikologia kwa watoto wanaokulia ndani ya familia za aina hizo na usijeshangaa mtoto akakua na yeye kuwa violent au na tabia za ajabu kwa familia yake........ni effect aliyoipata wakati anakua na ameichukulia ndivyo ndoa zilivyo au zinavyotakiwa ziwe. Mtoto anayekuwa kwenye familia ambayo mama yake haeshimiwi, ananyanyaswa na mama huyo kukaa kimya naye atachukulia kuwa ndivyo mke mwema anavyopaswa kuwa...so mkewe akiwa tofauti tu ni tatizo. The same kwa watoto wa kike, kama baba ananyanyaswa, anatukanwa au anapigwa watategemea kupata wenzi wenye nidhamu kama baba yao.

So I dont think kuwa mara zote kutengana ni kuwadeprive watoto amani. ila tu kuwe na zingatio kubwa katika kujaribu kuwaelewesha why hali imekuwa kama ilivyo (epuka kuonyesha ubaya wa mwenzi wako kwa watoto)

Maty unauliza maswali mengii............. kuhusu kama ni suluhisho ninawezasema ndio na hapana. Itategemea unapoamua kuachana na mwenzi wako umejipangaje kukabili maisha yako ili usijikute kwenye wakati mgumu utakaokufanya ujutie maamuzi yako. Lakini vile vile kabla hujaamua "mimi sasa basi" ni vema ukachukua muda mzuri wa kukaa na kutafakari ili kujidhihirishia kuwa unachukua uamuzi sahihi na changamoto zake unazijua vema na una mikakati ya kukabiliana nazo. Epuka kuamua kwa hasira. Itakuumiza mwenyewe.

Kuhusu kuoa/olewa tena...............uhmmmmm inategemea na kama uliamua kuufungua tena moyo wako kwa mwingine na kama maamuzi yako ya kuolewa/oa yalishirikisha experiences ulizozipata kwenye ndoa yako ya mwanzo. Usikurupuke kwa kuwa tu kuna jamaa kakutamkia anakupenda na wewe ukataka kumdhihirishie mtalaika wako kuwa "yeye alipokuwa akisema wa nini, kuna walokuwa wanajiuliza watakupata lini" utaumbuka.

Usinisahau kadi ya mwaliko mamito

Huwa najiuliza mara nyingi lakini nakosa jibu zuri, naomba nipate mawazo tofauti tofauti, inaweza kutusaidia wengi wetu.

Wanandoa wengi hasa wa miaka ya sasa, wakikorofishana korofishana baada ya muda wanachoamua ni tuachane bwana kila mtu ataanza nataka niishi kwa amani, nahitaji furaha mimi maisha yenyewe mafupi haya. Ukute hiyo ndoa baba msomi ana kazi nzuri na mama vile vile ndio balaa, kila mtu anasema usinibabaishe ninaweza kumudu maisha.

Hapo kuna watoto mmezaa, lakini kila mtu utamsikia napenda kuishi kwa amani, ni vipi kuhusu watoto? Je hao hawatakiwi kuishi kwa furaha na amani wakiwa na baba na mama? Hivi hamuwezi kukaa mkazungumza na kuelewana ili mlee watoto pamoja badala yake mnafikiria kuachana?

Hivi kuachana ni suluhisho la matatizo yako? Na je ukiachana na mwenzio ndio kusema hutaki kuoa/kuolewa tena? Na je ukioa/olewa halafu huyo mwingine akawa na matatizo pia pengine kuliko uliyoyakimbia mwanzo utaachana nae pia? Au utavumilia?

Tushirikiane kupeana mawazo wandugu

Kumradhi,
...sijui kwanini mmeweka kigezo cha usomi kwenye mada hii.
Inahusiana vipi, labda mimi sijaelewa.

Apart from that, binafsi naamini zipo irreconcilable differences ambazo
mkijilazimisha kuishi pamoja, matokeo yake ni uadui ambao mmoja wenu
huenda akajipatia hata maradhi kutokana na msongo wa mawazo.
 
Happnines is within you, you have never been happy since you born? Unataka huyo mwanamke au mwanaume afanye muujiza gani kuja kukufurahisha wewe ambayo hujawahi kufurahi?

Hivi tunapozungumzi ndoa kuna watu wanaelewa kweli? Sometimes watu wanafanya utani na maisha ya watu wengine. Unaolewa leo kesho unakuwa na jeuri ya kusema eti funga kilicho chako urudi kwenu? Kwa nini? wewe ni nani kusema hivyo? Its the right tine to cast those DIMONS, jengeni utamatuni wa kusoma vitabu vihusuvyo maisha, how to behave, mwenzio akikosea basi wewe rekebisha siyo na wewe kesho ufanye kosa lake kwa excuse kwamba naye alifanya hukusema.

Hawa watoto waliorundikana mitaani tutamwambia nini Mungu wetu? Women I urge to learn how to pray, nyien ndo wamama wa nyumbani, vinara, na madereva wa nyumbani. Chochote kinachotokea nyumbani watu watakutangalia wewe, hata mumeo akikutwa anafanya upuuzi barabarani wanasema hivi kweli ana mke yule? That means wewe ungeshakemea tabia hiyo kirahisi na si kumwacha akafanya anavotaka.

Kumbukeni mke na mume ni watu wawili waliokutana ukubwani, kila mtu amekuwa na tabia yake toka huko alikotoka, kukemea tabia ya mwenizo itoke unahitaji upako wa hali ya juu, maombi ya kufunga na kukesha ukimaanisha kurudisha kile kilichopotea. Ebu fikiria, kama unaachana na mumeo ni nani aliyemwema? THERE IS NO PERFECT MAN IN THIS EARTH, we all learn thorough our mistakes. Usichukulie kosa la mwenzako kuwa chanzo cha tatizo ongea mpaka Yesu atokeze kuachana NO. Nyie mnaotaka kuishi maisha ya raha, amani na starehe nyingi bila kubanwa kwa taarifa yako "If you never been happy since you born who do you think can make you happy" Utazunguka milima na mabonde, unatafuta amani na furaha kwa mtu baki wakati wewe mwenyewe hujifurahishi au kujipa amani"

Wanawake oneni mbali, fungukeni macho, mlilie Mungu akutengenezee njia naamini anatenda, mwaminifu, hana ubaguzi. Alikujua kabla hujatoka tumboni mwa mama yako.

NI changamoto ila kuachana siyo SULUHU. Take precautions GIRLS. Be blessed.
 
....
Apart from that, binafsi naamini zipo irreconcilable differences ambazo
mkijilazimisha kuishi pamoja, matokeo yake ni uadui ambao mmoja wenu

huenda akajipatia hata maradhi kutokana na msongo wa mawazo.



Hizi differences ila wengi wanazisema, mimi najua moja tu ya kucheat (anyway wengi wetu tunaisamehe pia). Hizi nyingine ni zipi?
Tufunguane macho please tusijeishia kwenye uadui na watu tunaodhani kuwapenda.
 
Kumradhi,
...sijui kwanini mmeweka kigezo cha usomi kwenye mada hii.
Inahusiana vipi, labda mimi sijaelewa.

Apart from that, binafsi naamini zipo irreconcilable differences ambazo
mkijilazimisha kuishi pamoja, matokeo yake ni uadui ambao mmoja wenu
huenda akajipatia hata maradhi kutokana na msongo wa mawazo.

Pole Mbu hapo kiwango cha elimu nimeweka kwenye post yangu kwa kuwa mtoa mada amekizungumzia kama mojawapo ya sababu za kuvunjika kwa ndoa nyingi au chanzo cha matatizo . Ndio nikawa najaribu kumwelewesha kuwa inategemea na hulka ya mtu na ulimbukeni wake... kuna waliosoma na kusoma awe mwanamke au mwanaume lakini akijua jukumu lake kama mama/baba au mme /mke mambo yanakuwa swari tu.....si kila ndoa za wasomi zina matatizo spo tunarule out variable ya usomi a.k.a. kiwango cha elimu katika kuexplain matatizo au kuvunjika kwa ndoa.
 
Nafikiri huwa wanakosa roho za uvumilivu ingawa hakuna sababu ya kuvumilia maumivu.
 
hivi mpaka mnaoana hukujua si chaguo lako?tuache tamaaa ndoa zitadumu

Mike1234 hili ni swali zuri sana......mimi nafikiri si vema kutumia sentensi au sababu hii eti hakuwa chaguo lako .......nafikiri ULIMCHAGUA ndipo ukamwoa unless umechaguliwa na wazazi ndo unawezasema hakuwa chaguo lako. Hii ni lame excuse kwa kweli. Uko sahihi pia kuwa tamaa zimetuzidi, unacho ndani but unaona kilichoko nje ndo kizuri zaii ........ni kama mpenzi wa chipsi............. akikaangiwa nyumbani katika hali ya usafi hazinogi anatamani chipsi vumbi......................Jamani ndoa si lelemama

Hovi hatujiulizi jinsi tu ilivyo ngumu kumlea mtoto uliemzaa mpaka akakuelewa sembuse mtoto wa binadamu mwingine ambaye mmekutana akiwa na meno yake 32 kamili?? kama hakuelewi hatokaa akuelewe hata umbembe mgongoni kila siku asubuhi
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Lazima mtendeane Haki jamani mwenzio ana kiu wewe ndo kwanza unajifunika blanketi unataka hiyo kiu akaitoe wapi?

Sasa ndo hapa unaona umuhimu wa nyumba ndogo mzee anaamua kujitafutia kiform iii kiwe angalau kinampa massage.

Fide ulishawahi hata siku moja kujiuliza why mamsap anatoa sababu ya kuchoka?? Jamani kina baba msijisahau.........kupata huduma kwahitaji maandalizi, mbona mkiwa mwahitaji huduma za hospital au benk huwa mwajiandaa?? Hata huduma hii pia mnatakiwa kuandaa vizuri mazingira.....wewe umeamka asubuhi kama ndo umejaliwa kupata "breakfast' basi indicate kuwa hata jioni unatarajia.........sio kukaa kimya na kusubiri ifike jioni 'ugonje sahani' kama ishara ya kutaka chakula ..la hasha............sifia....baada ya ;breakfast' kama umebahatika chombeza hata kwa neno moja aumawili ...I cant wait menu ya jioni........ ni signal tosha kwetu sie kuwa leo bwana anahitaji kunifurahisha na mie nijiandae........asa wengine unahudumiwa asubuhi unagumia tu husemi hata aksante kwa kahawa..........afu ukirudi usiku na mipombe yako unageuza tu sahani upande wako...jamani sometimes na sie tunajisikia vibaya...hakuna tofauti na bosi wa ofisini anavyokutreat na mikazi yake ....ndo hapo mwapata visingizio vya nimechoka n.k.
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Nnunu nimeshaingia kazini. Nachoweza kusema kuhusu nyumba ndogo si kuwa inarekebisha nyumba kubwa ila inafanya husband arudie vows. Maana nikigundua kuna kimada mziki wake ni lazima urudie maneno yote mazuri ulonambia toka tuna date mpaka unaapa kanisani. Haa. Mwanzo wife anakuwa na hasira, baada ya muda anashukuru nyumba ndogo kwani amefufua mapenzi katika ndoa. Kwa experience yangu wanaume wakibambwa wanarudisha descipline na mapenzi yana double! Na hii si kurekebisha nyumba kubwa ila inamfanya mume nae atie akili. Unafikiri ni rahisi ku divorce mke alokuzalia watoto wanaokufanya nawe uitwe kidume.

Mimi nina experience ya ndugu yangu yaani mume wake alicheat alafu yeye mwenyewe cheater ndo kaita kikao cha wana familia kwani anaogopa ndoa isije vunjika.

Inawezekana mkikaa bila hawa vicheche ku interrupt ndoa yenu ndoa ikawa boring. Hizo ndo challenges zenyewe. Ila sasa kilichoharibu maradhi!


Maty usiogope kuingia kwenye ndoa kiasi hicho,
kwa sababu siyo kila ndoa ina matatizo makubwa sana ambayo hayazungumziki na kutafutiwa ufumbuzi.

UKIPATA MTU MNAYEKUBALIANA KUITENGENEZA NDOA YENU VIZURI basi aah raha mstarehe kila kikwazo kinapojitokeza hamuiti tatizo bali mnaita changamoto, na maisha ya ndoa yataendelea kuwa ya raha bin mstarehe.

Nimesoma comments za wana JF wote lakin SIJAONA comments YA NYUMBA KUBWA naona leo hayupo on line,

Yeyote atakayemwona NYUMBA KUBWA amwambie nina RB yake haraka sana naomba achangie hii thread....lol, pia nataka anipe ufafanuzi wa ile comment ya FIDEL aliyosema ,
eti nyumba kubwa inarekebishwa na nyumba ndogo,
hata sijui atasemaje katika hili.....lol.
 
Kipato ni matokeo. Wengi wanaoana wakiwa hawana kitu zaidi ya Elimu. Baada ya muda ndo unakuta mmoja kajaaliwa zaidi ya mwingine. What is money by the way. How can you compare those papers with LOVE?

Nunga mkono hoja kwa kuongezea usemi wa wahenga:- MAFAHALI WAWILI HAWAKAI ZIZI MOJA

Halafu napendekeza kwamba wapenzi wachaguane kwa vigezo vya tofauti za kipato, yaani wahakikishe mmoja awe nacho na mwingine awe mlalahoi ili kujenga heshima, kwa hiyo mama akiwa nacho achague baba hohehahe, na baba akiwa nacho achague mama hohehahe na wahakikishe hali hii haibadiliki. si inasemekana eti ukiona watu wawili wanapatana basi mmoja ni mjinga, lazima kuwe na Mr. au Mrs. yes ndio mambo yaende sawa, mnaonaje hiyo?
 
Hizi differences ila wengi wanazisema, mimi najua moja tu ya kucheat (anyway wengi wetu tunaisamehe pia). Hizi nyingine ni zipi?
Tufunguane macho please tusijeishia kwenye uadui na watu tunaodhani kuwapenda.

...mnh FA wala sikutajii! ...Mw'mungu akupitishilie nazo mbali uishi na mumeo mpaka kifo kitapowatenganisha.
Mimi na Mwj1 twajua kilichotukumba, tuacheni hivi hivi, LOL!

The topic is hot...Ndoa yangu bado changa so naobserve na kulearn... Thanx Maty kwa kuanzisha hii thread... Okey, 2endelee...

Mkare, there's no need to learn/go deep on this topic, observe 10 commandments, na mtangulize Mw'mungu ndoa yako itasimama. Thread hii haina mantiki ya kuzijenga ndoa. Ni dongo letu sie 'wajane!' acha tupambane nalo!
 
Nafikiri huwa wanakosa roho za uvumilivu ingawa hakuna sababu ya kuvumilia maumivu.

...hapo sasa,...!

Unajua mambo haya yasipokukuta, huoni justification yeyote ya kuachana.
"Kitanda usichokilalia," ni ngumu kujielezea/kueleweka pale utaposema 'enough is enough!'.

...acha tu niendelee kubugia popcorn zangu hapa 😛op2:...si muda mrefu
atakuja mtu hapa na post yake 'keshatendwa!' haoni tena thamani ya maisha.
 
Back
Top Bottom