Tupeane Uzoefu: Biashara gani ilikushinda?

Tupeane Uzoefu: Biashara gani ilikushinda?

Kwanini Unasema Mpunga ni pasua kichwa!
Kwenye kununua, ina hitaji uzoefu sana kwenye kuchagua mpunga mzuri!! Hata ndoo zenyewe za kupimia sio hizo unazojua wewe zipo special za kupimia, ndoo hizo huuzwa hadi laki 2!!!kwa ndoo moja tupu. Ila siku hizi sehemu nyingi wanazishitukia kwani ukipima ndoo saba, kwa kutumia hiyo ukija kupima kwenye ndoo za kawaida unakuta karibia ndoo kumi!!!!
 
Katika hustle za maisha huwa watu tunajaribu Biashara mbalimbali ili kuweza kufanikisha malengo yetu lakini wengi wetu huweka mitaji mikubwa pengine pesa za kukopa na mwisho wa siku changamoto zikiwa nyingi tunakata tamaa na kuacha.

Mimi binafsi nakumbuka nilianza biashara ya kuuza saa na viatu vya kike lakini changamoto kubwa ikawa ubora wa zile bidhaa. Aisee nilipata malalamiko mengi sana nikaamua kuacha. Laiti ningejua ningeboresha ubora wa zile bidhaa tu pengine leo ningekuwa na mtaji mkubwa sana.

Karibuni tushirikishane kuhusu biashara gani ulianzisha, changamoto ulizopitia na ulizitatua vipi au uliacha?

Uzi huu unaweza kuwa mwanga kwa watu wengine pia.
Kilimo cha Uyoga; aliyenipa mbegu aliniingiza cha like kumbe simu..... Mwaka wa tano huu natafutwa na polisi
 
Niliwekeza hela nyingi kwenye bando nikakuza account instagram aaah nilipiga hela za matangazo kama kichaa yani kwa mwezi laki mbili kitu kidogo sana nikajikusanya nikanunua cm ya maana mfukoni nikabaki cna kitu hacker akafanya yake mbaka leo roho inauma sanaa[emoji2363][emoji2363]

Lkn nimeanza na account mpya mambo co mabaya nasogea


Sent using Jamii Forums mobile app
Tunaomba mbinu ya kukuza account mimi nina followers kama 5000. na sijui naikuza vipi maana imenichukua mitatu kuwapata hao follower

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom